Alhamisi, 27 Februari 2014

UWIANO WA UJUZI NA UHARIBIFU WA DUNIA

Ujuzi tunaweza kuufafanua kwa namma kuu mbili
(a) Ni maarifa au uwezo wa kufanya jambo fulani anaokuwa nao mtu
(b) Hali ya kutambua kitu fulani au kuwa na ufahamu uliopatikana kwa uzoefu.
Ninaposema uwiano wa ujuzi na  uharibibu ninamaana ya uwezo au uzoefu ulio ndani ya binadamu juu ya kitu fulani ambao wakati mwingine unatumika vibaya na kufanya mambo kuharibika badala ya kuwa bora.Ndugu yangu ujuzi ni muhimu sana kwa maisha ya binadamu,kwasababu hakuna lolote linaloweza kufanywa bila ujuzi .katika mada hii naomba niongelee jinsi ujuzi unavyoweza kutumika kuleta uharibifu unaoweza kuiangamiza dunia na kuifanya isiwe mahali panapofaa kwa maisha ya binadamu tena.

1. LENGO LA KUTAFUTA UJUZI NA MATAMANIO YA BINADAMU
(A) LENGO LA KUTAFUTA UJUZI
Lengo kuu la kutafuta ujuzi ni kuutumia katika kujiendeleza na kuiendeleza dunia na sio kuibadilisha kwa maana ya kuifanyia mabadiliko kutoka hali yake ya asili.
*Ujuzi unatakiwa utumike kurahisisha maisha na kumfanya mwanadamu kuishi raha mstarehe
*Ujuzi unatakiwa kwaajili ya kuunda zana za kurahisisha kazi na kuzikarabati.
*Ujuzi unatakiwa kurejesha au kukarabati kila uharibifu unaotokea katika mwili wa binadamu.
*Ujuzi unatakiwa kutumika kuboresha na kukarabati kila uharibifu unaotokea katika dunia.
kilakitu kinachoharibika huwa kinahitaji ukarabati au kurejeshwa katika hali yake ya mwanzo kabla ya uhalibifu. Tutambue kuwa dunia imefanywa kuwa hai kutoka na utimamu wa vijenzi vyake na inahitaji ukarabati kila inapopatwa na uharibifu ,naam ukarabati wa kila uharibifu na si uharibifu flani flani tu kama ambavyo tumekuwa tukifanya; mfano kupanda miti kwa lengo la kupunguza hewa ya okaa huku tukisahau kuwa kuna gesi nyingine tulizozalisha kutokana na kemikali zilizosambaa hewani kimakosa au kwa makusudi.Gesi hizo ni pamoja na zile zinazotokana na uteketezaji wa kemikali hatari na madawa yaliyokwisha muda wake.

Wakati mwingine hatujali hata mashimo tunayoyaacha mara baada ya kumaliza kuchimba madini. Isitoshe hatujui hata tutafanya nini na pengo kubwa litakalobaki ardhini baada ya kuyamaliza maji yote tunayochimba kwa shughuli zetu za kila siku hasa za viwanda kutokana na kutokuwa na mkakati wowote na wenye uwiano wa kurejesha maji tunayoyatoa.

Nashindwa hata kufikiri ni namna gani tunaweza kuiokoa mito yetu inayopokea maji yanayotoka katika mashamba yetu yaliyojaa kemikali na sumu za kila aina zinazotumiwa kila kukicha kwaajili ya kupata mazao bora ukizingatia kuwa mashamba huwa juu na mito huwa chini.Pia unaweza ukatafuta jibu wewe mwenyewe kwamba maji yenye kemikali kutoka viwandani huwa yanakwenda wapi? ,bila shaka ni ardhini na je? ni nani ameshawahi kutushirikisha tumsaidie kuzitoa hizo sumu ardhini ili tuchimbe maji ya kunywa na kwaajili ya kutengeneza bidhaa nyingine tunazokunywa.


Kusudi la kuifanyia dunia ukarabati ni kuhakikisha inabaki katika hali yake ileile ya asili . Ujuzi wetu unapaswa kuhusika moja kwa moja katika uendelezaji wa asili ya dunia au kukarabati uhai wa wake na kama ni vinginevyo huwenda dunia isifae tena kwa maisha na kuwa ni mahala pa shughuli nyingine tofauti na maisha ya binadamu .kumbuka uhai wa dunia ndiyo uhai wa kila kiumbe hai ndani yake kama sisi tutakufa dunia itaendelea kuishi na kama dunia ikifa sisi hatuna uwezo wa kuishi.Ni wazi kuwa kutumia ujuzi wetu kunusuru na kuendeleza maisha ya dunia ndiyo kufanya maisha yetu yazidi  kuendelea juu ya uso wa dunia yenyewe.

(B) MATAMANIO YA BINADAMU
Haya ni matarajio makubwa ya binadamu yenye shauku ya kutaka kuwa na maisha bora na rahisi sana katika kila jambo.kwasababu hii binadamu asiye na tafakari anataka kutumia mbinu rahisi zinazopatikana kwa muda mfupi ili awahi kupata mahitaji yake bila kujali athari za matokeo ya hatua aliyochukua.Inafanana kabisa na mfano wa mwenyenyumba aliyeuza nyumba yake na kwenda kulipia hoteli ya kifahari ambayo alionjeshwa utamu wa usingizi wake siku moja kabla.Aliishi kwa muda na baada ya pesa kuisha kila mtu anafahamu kilichofutia.

2. MUUNDO WA DUNIA NA TABIA ZAKE.
Dunia imeundwa kwa vijenzi vingi ikiwamo
(a) Atmosphere (hewa), inajumuisha gesi zote pamoja na unjevunyevu uliopo juu ya uso wa dunia.Hewa kavu ndiyo inayochukua sehemu kubwa ikiwa na wastani wa 78.09%.Gesi zinazojulikana kuchukua nafasi kubwa juu ya uso wa dunia ni nitrogen 78.084%(78) oxgen 20.946%(21),argon 0.9340%(0.9),carbon dioxide 0.035%(0.03) na nyinginezo zinazochukua nafasi ndogo.Kiasi cha unyevunyevu katika hewa kinachukua wastani wa 1%.hili eneo ndilo lenye kazi kubwa ya kuimarisha uhai wa viumbe pamoja na kufyonza na kuchuja mionzi ya jua hivyo kupunguza makali yake katika uso wa dunia.Kwa ujumla eneo hili linachukua umbali wa hadi km 400 kutoka katika uso wa dunia lakini 80% ya eneo hewa iko ndani ya km16 (10ml) kutoka katika uso wa dunia.

(b) Hydrosphere (maji) inajumuisha bahari,maziwa ,mito,na maji yaliyokusanyika juu ya uso wa dunia.eneo hili ndilo linalochukua sehemu kubwa ya uso wa dunia kwa kiasi cha 70%.Ni eneo muhimu kwa maisha ya binadamu pamoja na viumbe hai wengine waishio katika uso wa dunia.linasaidia kusharabu 90% ya mionzi ya jua inayotua juu ya uso wa dunia .Eneo hili linasifa kubwa ya kuwa katika mwendo kwa muda wote kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo upepo.

(c) Biosphere (viumbe hai) inajumuisha eneo lote la anga na la uso wa dunia linalokaliwa na viumbe hai.Kwa wastani ni eneo lote linaloanzia 10km kutoka hewani hadi chini kabisa ya bahari.Hili nalo ni muhimu kwa maendeleo ya dunia kwa sababu linawezesha viumbe hai kuishi na ambao ni moja ya nguzo muhimu ya ikologia katika uso wa dunia.

(d) Lithosphere (tabaka la juu la ardhi) inajumuisha tabaka lote gumu la juu la ardhi na miamba na la chini ya bahari.Linakadiriwa kuwa zaidi ya km 100 kwenda chini.eneo hili linaundwa kwa sehemu kubwa kutokana na mchanganyiko wa oksijeni na silikoni (silicate SiO2) na kemikali nyinginezo ni oksijeni ( oxygen) 46.6% (47),silikoni(silicon) 27.7% (28),alumini (aluminum) 8.1% (8),chuma( iron) 5%,kalisi(calcium) 3.6%(4),sodiamu 2.8%(3),potasiamu 2.6%(3) na magnesi(magnesium) 2.1%(2) .Hili ndilo tabaka jembamba,gumu,kavu,lenye nguvu,lililoshikamana sana,la kunyumbuka kuliko matabaka mengine.

(e) Mesosphere (mentle) (tabaka la kati la ardhi) inajumuisha eneo lote la kati ya lithosphere na barysphere .Lina wastani wa km 2900 kwenda chini na jotoridi kwa wastani wa juu kiasi cha 3000 Centigrade. Kwaasili ni eneo linaloundwa kwa miamba dhaifu yenye mkusanyiko wa oksaidi na salfaidi.

(f) Barysphere (tabaka la chini la ardhi) inajumuisha tabaka la chini kabisa la ardhi .tabaka hili limegawanyika katika sehemu kuu mbili ( dense core) tabaka la ndani lililoshikamana sana na (outer core) tabaka la nje tepetevu. Yote mawili yana wastani wa nusu kipenyo kisichopungua km 3000 kuelekea katika kitovu cha katikati ndani ya dunia.Eneo la nje linawastani wa jotoridi la 3900 Centigrade na la ndani lina wastani wa 4800 Centigrade yote yakiundwa zaidi na kemikali za chuma na nikeli huku la ndani likiwa katika hali ya chembechembe angavu na la nje likiwa katika hali ya utepetevu.

*Ieleweke kuwa kwa asili dunia haina tabia ya kuchukuliana na vitu vyenye kuleta uharibifu dhidi ya vijenzi vyake.
* Dunia haina tabia ya kuchukuliana na taka zozote zinazotokana na uzalishaji wa kubuniwa na binadamu.
*haina tabia ya kushirikiana na vitu visivyokuwa vya asili ila vitu visivyo vya asili huitegemea dunia.
Mwenendo wa dunia unategemea uasilia wa muundo wake na tabia zake. kila kinachoonekana duniani katika hali yake ya asili kinahusika moja kwa moja kuendeleza uhai wa dunia.Sina hakika kuwa mpaka sasa tunaishi katika dunia yenye ulemavu mkubwa kiasi gani, unaotokana na uharibifu wa shughuli za binadamu. pia Inawezekana tunaishi katika dunia iliyokwisha kufa siku nyingi.

Mpaka sasa hakuna anayejishughulisha na kurudisha asili ya maisha ya dunia zaidi ya kuona jitihada kubwa za kupambana na tabia za asili za dunia.Kibaya zaidi unavyozidi kupambana na tabia za asili za dunia ndiyo unaifanya kuwa hatari zaidi kwa siku za usoni.

Katika ujuzi wetu tunaoupata inatupasa kutazama kwa makini kama unahusika katika kuendeleza uhai wa dunia na kama sivyo basi tuna pokea ujuzi batili wenye nguvu ya uharibifu na punde utatulea kihama ambacho hata hatukuwahi kukitarajia wala kukisikia masikioni mwetu.

3. KWANINI MWANADAMU NDIYO MWARIBIFU NA.1 WA DUNIA?
Swali hili lina majibu mengi lakini nitajibu kwa uchache kama ifuatavyo:-
(A) Ni rahisi mno kuharibu kitu chochote kuliko kukiunda au kukirejesha katika hali yake ya asili.

(B) Ameambukizwa uharibifu kutoka kwa waliotangulia.
kila kukicha binadamu anaamka na mawazo mapya ya tengeneza milipuko .tukitazama movie tunaona milipuko,tukitazama taarifa za habari tunaona milipuko ,milipuko katika masherehe makubwa ,milipuko migodini,milipuko jeshini nk.bila shaka hata huyu binadamu atakaye amka kesho naye atakuja na mlipuko mwingine mpya bora kuliko huo wa kwanza.

(C) bidhaa zenye uharibifu zinafaida kubwa ,
umeme utokanao na mitambo ya nyuklia ,viwanda ,magari ya mafuta ya petrol ,uchimbaji wa madini,silaha za kivita kama maroket ,mabomu ya nyuklia nk ,madawa ya kuuwa wadudu,mbolea za mashambani ,madawa ya aina mbalimbali,simu za mikononi na vifaa vingine vya kielectronic ambavyo hata vikichakaa haijulikani vitatupwa wapi na hata vikiangamizwa mabaki ya maangamizi yake haijulikani yanakwenda wapi.

mfano mwaka 2007 mwezi May India iliripotiwa kuangamiza (E-West) yaani electronic west(vifaa chakavu vya kielekroniki) tani zipatazo 146,000 wakati taasisi moja huko Marekani ijulikanayo kama (environmental protection agency) wakala wa utunzaji wa mazingira kama sijakosea Kiswahili chake ikiripoti kuangamizwa kwa computer 600 kilasiku katika mji mmoja tu wa California. Ilibainika kuwa wastani wa 70% ya kemikali zisizotakiwa katika ardhi yake zinatokana na bidhaa hizo ikiwamo (Dioxins) ambayo kwa sehemu kubwa huundwa na chlorine itokanayo na( chloranited plastics PVC)mchanganyiko wa chlorine na plastiki .Katika fact sheet iliyotolewa na shirika la afya duniani (WHO) mwezi may 2010 inadaiwa kuwa kwa tafiti zilizofanywa kemikali hizi zipo kila mahali.Ilielezwa kuwa binadamu ana weza kudhurika zaidi kupitia mafuta yaliyo katika nyama, samaki,na vyakula vilivyo na kemikali hizi ambapo madhara yake ni kupata matatizo ya uzazi ,kansa,mfumo wa kinga ya mwili, na kuingilia homonsi. Hiyo ni kwa mujibu wa miaka kadhaa iliyopita kwa hali itakavyokuwa sasa unaweza ukajijibu mwenyewe.

kwa huku kwetu tumeshuhudia uangamizwaji wa bidhaa feki kila kukicha zikiwamo tvs,cds,redios,subwoofers,dvds deck,nk ambavyo vyote vinahatari kwa ardhi ambayo tunaitumia kwa shughuli za kilasiku.

(D) ujinga wa kutojua wajibu wake.
binadamu ndiye kiumbe pekee mwenye wajibu wa kujibu kila kinachotokea katika dunia na kama si hivyo hakuna maana ya kuwepo kwa binadamu katika dunia.Kupitia ujuzi wako unatakiwa kuhakikisha kuwa unawajibika kwa uhai wa dunia na si familia yako tu kwa kufahamu kuwa, hakuna kiumbe kingine kitakacho tetea uhai na kukarabati uharibifu wa wake zaidi ya binadamu.

Katika kila ujuzi tunaochagua kuufanya kuwa maalumu kwa maisha yetu kunauwezekano wa kuisaidia dunia katika kuimarisha uhai wake na si kama tunavyofahamu au kufundishwa.Tumezoea kusikia kuwa kuna bwana mazingira bwana misitu nk. Lakini hawa hawatembei na mazingra haya na kumgawia kila mtu punde panapokucha na kuyarudisha jioni,bali mazingira haya ni mali yetu sisi na ndiyo tunayoyatumia kufanyia shughuli zetu za kila siku.

kila unaposimama iwe baharini, nchi kavu, angani,chini ya ardhi panakuhusu wewe. Binadamu unayemwona mbele yako yeye ni nyongeza tu katika shughuli nzima ya kuiendeleza uhai wa dunia, lakini aliye muhimu kabisa ni wewe.Wewe ni mjuzi katika kutengeneza simu ya mkononi ,umesha piga picha na kuona mwisho wa hiyo simu? Na je umeshapima matokeo baada ya matumizi yake katika uharibifu wa dunia utakaojitokeza?je umechukua hatua gani baada ya kugundua mapungufu ? muundaji wa( magari ,meli ,boti ,treni,ndege,maroketi,setilites pamoja na mtumiaji, vivyohivyo kwa mrutubishaji wa nyuklia , mtengenezaji wa mbolea ,mchimba madini, maji ardhini ,gesi, mafuta,mkulima unayefyeka misitu na kugeuza mashamba,mfanyabiashara wa bidhaa chakavu ,wajenzi wa majengo marefu na mafupi, mwananchi mkata mkaa,na wengineo , unashughulikiaje swala la uhai wa dunia kupitia huo ujuzi wako?.

Naomba nitamke kuwa ukitaka kuokoa maisha yako yaangamize kwa kuokoa dunia na ukitaka kuyaangamiza yaokoe kwa kuangamiza dunia. Jitihada ya kwanza katika ujuzi tulionao binadamu ni kujitambua kisha kuendeleza uhai wa dunia na si kuibadilisa kama tunavyojaribu kufanya, kwa kuwa kufanya hivyo kutaifanya dunia kuwa kitu kingine kabisa na si kwa matumizi ya binadamu wajao.Ila kwa makusudi! binadamu wakati wa kupasiana ujuzi tunaacha kupasiani jukumu hili kubwa la kuimarisha au kuendeleza uhai wa dunia na badala yake mkakati mkubwa tunauweka juu ya kurahisisha mijongeo ,ulinzi,mawasiliano,upatikanaji wa chakula,mavazi,matibabu,makazi,nk.Sasa ni wakati wa kuwajibika kwa uhai wa dunia, isije ikawa ilishatufia bila sisi kujua na kujikuta tukitumia nguvu kubwa kujiendeleza na baada ya muda ikashindwa kuhimili uharibifu na kutuangamiza sote pamoja nayo.

(E) kurahisisha maisha
Binadamu ndiye kiumbe mwenye shughuli nyingi duniani tofauti na viumbe wengine lakini ndiye anayependa rahisi kuliko viumbe vyote .Hutumia kila kiwezekanacho kila ujuzi kurahisisha kila anachofanya katika maisha yake ya kilasiku. Ikumbukwe kuwa hata kama maisha yatarahisishwa vipi kwa kutumia ujuzi wetu ,lakini kama urahisi huo unatokana na kuharibu sehemu flani ya dunia, basi tujue kuwa hatujarahisisha maisha bali tumeongeza ugumu mara dufu kwa sababu uharibifu wa dunia wa namna moja hujibu kinyume chake kwa namna zaidi ya moja.

Kwa mfano teknologia ya matumizi ya mkaa hapo awali ilionekana kama ni mkombozi wa mwanadamu katika kuhifadhi nishati ya joto. Lakini ili uipate ni lazima uharibu misitu na ukiharibu misitu utakuwa umesababisha kukosekana kwa mvua kutokanako na kukosekana kwa unyevunyevu unaohifadhiwa na misitu na vievile utasababisha kuongezeka kwa hewa ya okaa (caborn dioxide) itakayo zorotesha tabia nchi kwa kupandisha joto hivyo kuathili kilimo kwa kukosa mvua,upatikanaji wa maji,kupoteza wanyama kwa kukosa uoto wa asili, na mengineyo.Bila shaka sisi sote ni mashuhuda wa haya na tunaona dunia inavyoweza kujibu zaidi ya mara moja kwa kosa moja tu la matumizi yetu mabaya ya ujuzi tulionao.

Kwa kuto yatambua hayo tutakuwa tukionyesha wazi kuwa hatujajitambua na kwasababu hiyo hatutatofautiana na mababu wa zamani ambao walihamia huku na kule katika kupigania uhai wao pasipo kujua lolote kuhusu uhai wa dunia, na matokeo yake waliambulia kunyang’anyana rasilimali chache zilizowagawa kwa ujinga wa kutotambua wajibu wao mkuu.

4 . USHAHIDI WA UHARIBIFU WA DUNIA
Kuna ushahidi mkubwa sana wa uharibifu wa dunia unaotokana na matumizi ya ujuzi wa hali ya juu,kati na chini alionao binadamu. Ili nisikuchoshe nitataja maeneo machache yaliyoweza kuharibiwa
(a)   UHARIBIFU WA HEWA
Hewa imeharibiwa kwa namna tofautitofauti na kuleta matokeo ya moja kwa moja au yasiyo ya moja kwa moja kulingana na kiwango cha uharibifu kwa uwiano wa  eneo husika.
Kiwango kikubwa cha uharibifu  wa hewa kimesababiswa na ongezeko la kaboni daioksidi (co2) ambayo kwa takwimu za mwaka 2007 imechangiwa kwa 94% kutokana na mafuta asilia ya petrol ,makaa ya mawe na gesi.Chembechembe nyingine huingia moja kwa moja katika hewa kama ilivyo kwa salfa oksaidi (so2), chembechembe nyingine za ardhi (crustal materials) na chembechembe za kikaboni.

Gesi nyingine hujitengeneza zenyewe katika tabaka la ozoni pale zinapochanganyika na oksijeni kwa kuunguzwa na mionzi ya jua.Sio lengo langu kufundisha ECOLOGIA bali ni kukupa walau ushahidi wa kinachotokea kwa ufupi.

Kwa mtindo huu kumekuwa na gesi aina kadhaa ambazo zimeingia katika hewa na kuifanya kuwa si salama tena ,mfano wa gesi hizo ni:-kwa kiingereza..
CARBON MONOXIDE (CO) huchangia kuzalisha  kaboni dioksaidi na tabaka ozone na madhara yake ni kupunguza kiasi cha oksijeni kinachotakiwa katika mwili, ongezeko la joto na wakati mwingine huleta matatizo ya moyo na maumivu ya kifua .

AMMONIA  (NH3) huchangia ongezeko lake kwenye maji ya mito na maziwa na uharibifu wa madini ya naitreti (nitrate) katika maji ya ardhini.Ikiunganika na baadhi ya kemikali huleta matatizo ya kiafya .

VOLETILE ORGANIC COMPAUND (VOC2) huchangia ongezeko la kabon daioksaidi na kuongeza joto ,tabaka ozone ,madhara kwa tabia nchi , mabadiliko ya mazingira,kansa kwa binadamu na matatizo mengine makubwa ya kiafya.

MERCURY  (Hg) madhara yake hayana tofauti na yale yanayotokana na mchanganyiko wake katika maji kama ilivyoelezwa katika matokeo ya uharibifu wa dunia.

OZONE (03) Huathili ukuaji wa mimea  kwa kuzuia mimea kujitengenezea chakula,pia huzuia kwa kiasi Fulani mimea kupokea kaboni daioksaidi na kuifanya kudhoofika.Kwa binadamu hupelekea kupatwa magonjwa ya mapafu,kukohoa na kupumua kwa shida na athma (asthma)

PARTICULATE MATTER (PM) zinaweza kuathili muundo wa chembechembe za ardhi. Chembechembe kadhaa huakisi mionzi lakini nyingine kama kaboni nyeusi husharabu joto na kuongeza joto duniani.


LEAD (Pb) huharibu mimea na wanyama pori, pia hufanya ongezeko katika ardhi na kuchangia uharibifu wa viumbe ya nchi kavu na majini.
Pamoja na hewa nyingine za sumu zenye madhara kwa binadamu ,zote hutokana na mabadiliko makubwa ya matumizi ya ujuzi wa binadamu.
(b) MAJI
maji yameharibiwa kwa shughuli za kiviwanda
kemikali na madini kama arsenic, mercury, chromium, nickel, barium, cadmium, cobalt, selenium , vanadium, mafuta ya petrol ,cyanides,thiocyanides,phenolic,fluorides(,radioactive substances kemikali zenye mionzi hatari) vimetumika kwa wingi viwandani na wakati mwingine kutiririshwa katika mifereji au mito au ardhini na hivyo kuathiri maji ya ardhini na baharini.kwa Tanzania imewahi kutokea huko North Mara mwaka 2010 wakati ambapo mecury ilitiririswa katika mto kutoka mgodi wa uchimbaji dhahabu na kuharibu maji kabisa.

Huko India ukaguzi wa maeneo yenye viwanda (SUVEY OF INDUSTRIALIZED ZONE) ulionyesha kuwa maziwa makubwa ,vyanzo vya mito mikubwa maji yake hayafai kwa kunywa vile vile katika maeneo ya viwanda maji ya ardhini hayafai kwa matumizi ya kunywa binadamu.Fikiri kuhusu mafuta aina zote yanayomwagika ardhini,baharini na kwingineko yanakwenda wapi.


maji yameharibiwa kutoka majumbani
kutokana na unyunyiziaji wa madawa ya kuua wadudu na vimelea,sabuni na kemikali nyingine tunazotumia kuogea na kusafishia vitu vinginevyo,sumu zinazotumika kuua mbu na wadudu wasumbufu zinyunyiziwazo katika mifereji ya maji taka.Sumu zitokanazo na maji ya kuzima moto ambayo yote huishia ardhini na kuharibu maji , sisi sote tumekuwa mashahidi wa hayo.

maji yameharibiwa kutoka mashambani
kwa kilimo cha kutumia kemikali kama zinc, copper, manganese (Mn),
sulphur (S), iron, (B),chumvi chumvi za phosphates, nitrates, urea, potassium, nk zinafaa kwa kiwango flani lakini kiasi kinachoingia katika maji ni maradufu ya mahitaji ya viumbe hai na kugeuka kuwa hatari kwetu.

Maji yameharibiwa kutoka meneo mengine
Kuna compounds cyanides( zinazopatikana katika sumu za kuua wadudu na wanyama aina ya panya) thiocyanides, phenolic compounds, fluorides, radioactive substances kemikali zenye mionzi hatari kama za uraniamu na kadhalika( mfano huko fukushima Japani), ambazo ni hatari kwa maisha ya binadamu na wanyama zimepatikana katika maji.Matumizi ya kemikali za kuuwa wadudu zimetumika kwa wingi mashambani bila kujali kuwa hata maji yanaathilika aidha kwa kutiririkia mtoni na katika maziwa au kuzama katika ardhi na kuathili maji yaliyo ardhini.

maji yameharibiwa kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari
joto linapoongezeka kina cha bahari kinaongezeka na kina cha bahari kinapoongezeka maji huja ardhini na yakisogea ardhini ardhi hufyonza chumvichumvi kali zilizomo ndani yake na hivyo kuathili kilimo,maji kwa matumizi ya binadamu ,wanyama na mitambo.

(b) Uharibifu wa mali na majengo
Kutokana na mafuriko,majanga ya moto ni matukio ya kawaida kabisa katika kipindi cha miaka 40 iliyopita ambapo zaidi ya visa 100,000 vimeripotiwa ikiwa ni zaidi ya hekta milioni kumi.Hali hii inatokana na ukame ambao husababishwa na kutoweka kwa kiasi kikubwa cha unyevunyevu na ukosefu wa mvua juu ya uso wa dunia.

(c) kushuka kwa tabaka la ardhi (Land subsidence)
tukio hili hutokana na kutoa maji ya ardhini pamoja na gesi kwa muda mrefu mfano katika meneo ya kaskazini mwa Itali Revenna ambayo baada ya vita vya pili vya dunia ilikuwa inashuka kwa kiwango cha 110mm kwa mwaka. Mfano mkubwa wa tukio hili ni mji wa Venice ambao umekuwa na hatari nyingi zinazotokana na kushuka kwa ardhi kunakotokana na utoaji wa maji kwa kiasi kikubwa ardhini. Mbaya zaidi ni kwasababu mji huu uko ufukweni mwa bahari nchini Itali .
                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                            











  Matukio kama hayo yameripotiwa katika miji ya Bangkok ambayo katika kipindi cha miongo mitatu tangu mwaka 1978 imeripotiwa kushuka kwa 1m katika maeneo kadhaa.Pia mji wa Kolkata na mingineyo .Nishukuru kwa serikali ya Beijing kwa kuanza kuchukua hatua za kusitisha matumizi ya baadhi ya visima vya maji ya ardhini kama ilivyoripotiwa katika mtandao wa http://europe.chinadaily.com.cn/china/2012-02/28/content_14707333.htm . Tathmini iliyofanywa kupitia mamlaka husika mwaka 2009 zimeonyesha kupitia visima vikubwa vya maji ya ardhini 10,000 vimeweza kufanya ongezeko la ushukaji wa ardhi kwa zaidi ya mm 137 kwa mwaka katika maeneo ya mijini na vijijini Beijing.

5. MATOKEO YA UHALIBIFU WA DUNIA
A. KUONGEZEKA KWA KINA CHA BAHARI
kwa mujibu wa (MILLENNIUM ECOSYSTEM ASSESSMENT) wahanga wakubwa ni wale wanaoishi miji iliyo karibu na bahari .Sababu kubwa ya kuongezeka kwa kina cha bahari ni kutanuka kwa bahari kutokana na kuongezeka kwa joto yaani (themal expansion) wanafizikia wanajua hili wanaweza wakafafanua kwa undani lakini kifupi ni kwamba mada inapopata moto hutanuka.hivyo hata kwa maji ya bahari joto linapoongezeka duniani maji ya bahari huanza kupoteza density yake yaani ule mgandamizo wake hupungua na kuanza kujiachia hivyo kuchukua nafasi kubwa zaidi, na kama hali ya joto itabaki ile ile basi na maji yatabaki katika hali hiyo hiyo mpya hayatarudi katika hali yake ya kwanza, kwasababu hiyo tutashuhudia kuongezeka kwa kiwango cha maji.

IPCC (INTERNETIONAL PANEL ON CLIMATE CHANGE) imewahi kutoa tathmini ya ongezeko la jumla la kina cha bahari la 2cm hadi 7cm katika kipindi cha karne iliyopita kupitia kutanuka kwa bahari (THERMAL EXPANSION).
wakati mwingine kina cha bahari huongezeka kutokana na kuyeyuka kwa barafu kutoka katika maeneo mbalimbali ya dunia kutokana na kuongezeka kwa joto.IPCC imewahi kuripoti ongezeko la 2cm hadi 5cm katika kipindi cha karne iliyopita kupitia ongezeko hili.

(i) Njia nyingine inayosababisha kina cha bahari kionekane kinaongezeka ni ( relative sea level rise)
Ni uwiano  wa kimo cha bahari na ardhi ambapo inaweza kutokea kama bahari ikipanda kutokana na kupanda na kushuka kwa ardhi.Katika maeneo fulani fulani kama maeneo ya mwambao wa Norway na sehemu flani ya kati ya Atlantik katika mwambao wa marekani mashariki.maeneo haya yanatabia ya kupanda na kushuka kutokana na joto. Wakati barafu inapopata moto na kupungua uzito ardhi ya chini hupanda na bahari kuonekana imeshuka na barafu inapoongezeka uzito matokeo huwa kinyume chake.

(II) Matokeo ya kuongezeka kwa kina cha bahari
Tathmini iliyofanywa na IPCC (INTERNETIONAL PANEL ON CLIMATE CHANGE) ni kwamba kina cha bahari kitaongezeka kwa wastani wa 20cm na 86cm ifikapo mwaka 2100 na haitaishia hapo bali ongezeko litaendelea kwa kadri siku zitakavyozidi.

ongezeko la futi moja (30cm) la kina cha bahari linaweza kuathili wastani wa 4500cm (150 futi)kwenda ndani ya ardhi.hii inamaana gani ? ni kwamba maji ya bahari yanapopanda kwa wastani wa futi moja basi yatasogea mbele kiasi ya wastani wa futi 150 ili yaweze kukaa katika utulivu wake wa kawaida na .Endapo yataongezeka kwa 90cm tutegemee kusambaa mara tatu zaidi . Kuendelea kwa kitendo hiki kutapoteza majengo mengi,fukwe nyingi,maeneo ya kuzalia viumbe vingi vinavyozaliana katika fukwe hizo.

Kutokana na utamaduni wa binadamu kupambana na tabia za asili za dunia badala ya kuirejesha dunia katika hali yake ya mwanzo, maeneo mengi ya kingo za fukwe yanajengwa vizuizi vya maji kitu kitakacho pelekea kupotea kwa maandhali nzuri ya fukwe kwa kukosa hali yake ya asili punde maji yatakaposogea katika kingo hizo. Maeneo mengi yameshaathirika tayari.Lakini tutambue kuwa kufanya hivyo ni hatari sana kwa siku za usoni pale maji yatakapofanikiwa kubomoa kingo hizo.

Hatari nyingine ni kwamba kina cha bahari kinapoongezeka uwezekano wa mafuriko yatokanayo na gharika huongezeka .ORGANIZATION FOR ECONOMIC CO-OPERATION AND DEVELOPMENT  2007 (OECD) inataja miji 136 yenye bandari ambayo ina wakaazi zaidi ya milioni moja na iko katika hatari ya kupatwa na mafuriko yatokanayo na gharika.Tathmini za mwaka 2005 kwa miji kumi yenye hatari ya mafuriko iliyo na mali zenye uwezekano wa kupotea kwa mafuriko zenye thamani ya dola 3000 bilioni( $3000 bil ) ambayo ni sawa na wastani wa 5% ya pato lote la dunia kwa wakati huo. Miji hii kumi yenye hatari zaidi ni pamoja na Miami,greater New York,New Orleans,Osaka-kobe, Tokyo, Amsterdam, Rotterdam, Nagoya, Tampa-St Petersburg na Virginia Beach. Miji hii ina kiwango cha 60% ya hatari ya miji yote lakini ikitoka katika nchi kubwa tatu tu: USA, Japan na Netherlands.

(B) KUONGEZEKA KWA JOTO DUNIANI
kwa mujibu wa repoti ya IPCC (INTERNATIONAL PANEL ON CLIMATE CHANGE) 2001ni kwamba joto liliongezeka duniani kwa kiasi cha 0.6 0 C (10 fahrenheit)tangu 1861.Inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2100 joto litaongezeka kwa kiasi cha juu cha 5.8 0C.

Pamoja na kuongezeka kwa hewa nyingine hewani kama METHANE,na NITROUS OXIDE lakini kwa asilimia kubwa kuongezeka kwa hewa ya okaa CARBON DIOXIDE ndiko kuliko leta mabadiliko makubwa ya hali joto.Hewa hii huzalishwa kwa njia nyingi haswa zinazotokana na shughuli za kilasiku za binadamu.Shughuli zenyewe zinaweza kuwa ni viwanda ambavyo vingi hutumia nishati ambazo zikiungua huzalisha carbon ambayo inapoingia hewani hujiungamanisha na hewa ya oxygen na kugeuka kuwa carbon dioxide.Vyombo vya usafiri vikiwamo magari yanayoongezeka kila kukicha,na vyombo vingine vya majini na angani, hivi vyote vimekuwa vikichangia ongezeko la CARBON. Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu na binadamu nae anachangia kuongezeka kwa hewa hii ya okaa bila kuwasahau wanyama .

Hewa hii ya carbon dioxide inatabia ya kusharabu nishati ya joto na kuihifadhi kwa muda kabla ya kuiachilia tena duniani au nje ya dunia hivyo kufanya kiasi cha joto kuongezeka kila baada ya muda.

Matokeo ya kuongezeka kwa joto
* kuongezeka kwa kwa kina cha bahari kama ilivyoelezwa awali,kutokana na kuyeyuka kwa barafu au kutanuka kwa bahari.
*kupungua kwa uoto wa asili na ukame
baada ya kuongezeka kwa joto mvua za msimu zimepungua na wakati mwingine kukosekan hali iliyosababisha maeneo mengi kugeuka kuwa jangwa ,misitu ya asili kupungua kama si kwisha kabisa.Mazao mengi hayawezi kustahimili ukame hivyo kusababisha ukosefu wa chakula maeneo mengi.
* mafuriko katika baadhi ya maeneo kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari na wakati mwingine mvua zisizokuwa na utaratibu.
*kuyeyuka kwa barafu na hivyo kudhoofisha utalii.Milima kama ya atlas na kilimanyaro ni mifano iliyopungua barafu yake kwa kiasi kikubwa.

(c) KUONGEZEKA KWA MAGONJWA
Kutokana na kuongezeka kwa joto vimelea vingi vinavyoishi kwenye joto vimeweza kuzaliana kwa wingi na kusababisha hali mbaya ya kiafya duniani.Mfano mzuri ni ugonjwa wa malaria ambao unatokana na mbu anyeishi zaidi katika maeneo yenye joto.
Njia nyingine ni magonjwa yatokanayo na matumizi ya kemikali hatari na madini mabalimbali yatumiwayo viwandani na mashambani .Madini na kemikali hizi tunapozinywa au kuzila kwenye maji au katika chakula zimekuwa na madhara makubwa kwa uhai wa binadamu mfano wa kemikali au madini yenye madhara ni kama ifuatavyo:-

ZINC-wastani wa kiwango cha juu kabisa ni kwa mama mjamzito ni 25mg kwa siku ,zaidi ya mg 165 husababisha matatizo ya kibofu,kutapika nk.

COOPER-zaidi ya 470mg ni sumu

BARIUM-zaidi ya 100 mg ni hatari kwa afya ya binadamu

IRON zaidi ya mg 10 katika kila kilogram inaweza kuathili mishipa ya damu,matatizo ya kupumua haraka,presha mbaya ya damu,usingizi,vilevile kuongeza uzalianaji wa bacteria na virusi mwilini ambavyo hutegemea zaidi madini haya kwa maisha yao.

MERCURY ni sumu na zaidi ya mg 100 inaweza kusababisha maumivu ya kichwa,maumivu yasiyo ya kawaida,kuhara,kuharibika kwa chembe nyekundu za damu,matatizo ya ubongo na mfumo wa fahamu,kiharusi,kubadili mfumo wa uzazi,kupoteza kumbukumbu nk.

ARSENIC ni sumu kwa samaki na wanyama na binadamu zaidi ya 25mg inaweza kusababisha kuhara,kutapika,kichefuchefu,kuwashwa kwa pua na koo,kututumka kwa ngozi na hata kifo.Inaweza kusababisha kansa ya ngozi,ini na mapafu na matatizo mengineyo.

KEMIKALI ZENYE MIONZI zinaweza kuharibu tishu za seli za mwili,kuharibu mfumo wa uzazi,ikiwa mama atapatwa na mionzi hii mibaya inaweza kuzuia kwa kiwango kikubwa ukuaji wa ubongo na tishu zinazohusiana na utengenezaji wa mifupa kwa mototo atakezaliwa.kunamadhala mengine mengi yanayotokana na kemikali nyingi tunazozalisha kwasababu mbalimbali ZA kurahisisha maisha yetu.

6. MASWLI NILIYONAYO JUU YA KINACHOENDELEA DUNIANI
(1) vizazi vinavyokuja vitaikuta dunia iliyohai au itakuwa haifai tena kwa matumizi ya binadamu)

(2) kama dunia haitafaa kwa maisha ya binadamu je tutahamia wapi?(3)kweli kitu kinachoitwa( evolution of man ) mageuk o ya binadamu ni mageuko ya mwili tu au pamoja na fikra? kama ni pamoja na fikra mbona uharibifu bado unaendelea? Na kama ni lazima utokee mbona hakuna marejesho ya kinachoharibika? kama yapo mbona dunia haitambui marejesho hayo? Na kama dunia haitambui marejesho mbona binadamu aliyeendelea anachukua hatua zilezile zinazoshindwa?

(3) Ni kweli haiwezekani kuiendeleza dunia bila kuiaribu kwa upande mwingine.?

(4)Hii milipuko mikubwa kabisa inayobuniwa kila kukicha na wataalamu wa hali ya juu wanaotufundisha sisi tunaokuja nyuma yao itamlipua nani? Je binadamu? Kama ni binadamu ili abakie nani duniani?la kama si binadamu je ? Ni dunia ? kama ni dunia binadamu atakwenda wapi? Kama ni sehemu tu ya dunia je! wale binadamu waliokosa mahala pao hawatakuja kwetu na kuwa mzigo wetu sote?Kama hawatakuja kwetu je?nani atawahudumia kule waliko wakingali hawana dunia iliyo hai?

(5)hapo mwanzo binadamu aliharibu mimea na wanyama wenzake kwa chakula,kisha akaanza kuharibu miamba na kutengeneza zana za mawe,kisha akaongeza na moto kuchoma misitu kutafuta chakula, kutumia moto akachoma chuma kupata zana bora zaidi,akaongeza na madini mengine kupata vito na mapambo,tukaja na sisi tukaongeza na nyuklia ,kuzalisha umeme milipuko,vipuli nk.,kwa mpango huu wa kuharibu ili kupata kitu tumeharibu bahari ,uoto wa asili,anga,tabia nchi nk kwa kunufaika na viwanda ,mafuta,vyombo vya usafiri nk. ?je vitu hivi havitaisha ? kama vikiisha vizazi vijavyo vitapata wapi cha kuharibu kwaajili ya kuendeleza maisha yao?bado ujuzi huu wa kuaribu hiki kutengeneza kile unatija katika dunia yetu ?bado dunia itaendelea na uhai wake?je tumeshawahi kufikiri kuzalisha bila kuharibu sehemu ya dunia? Kama haiwezekani je?ni bora kuendelea kuharibu na kubaki na dunia iliyokufa au tuboreshe fikra zetu kwanza?kama tunaogopa kuangamia kwa kuzidiwa na mahitaji yanayotuzunguka, kwa uharibifu wa kila kukicha tena kwa kutumia ujuzi wa hali ya juu hatutaangamia kutokana na mrejesho wa dunia kwa uharibifu wetu?

                                   (6) Ufumbuzi
ni wakati sasa wa wanadunia kuamua kwa dhati kuchukua hatua za makusudi kwa kuamua kubadilisha fikra ya kuharibu na kuunda kwa kufikiria kuunda bila kuharibu.


Jumamosi, 15 Februari 2014

VIGEZO 12 VYA KUPATA UDHAMINI WA KIELIMU

Watu wote tunafahamu kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha na ukiikosa unahatihati ya kunyanyaswa na ulimwengu. Hata hivyo imekuwa vigumu sana kuipata kutokana na gharama na ukizingatia wakati wa kusoma mambo ya kifedha huwa magumu au huwa hayawezekani kuyafanikisha kirahisi.Wengi hujikuta wakisoma kwa msaada wa watu wengine wakiwamo ndugu ,walezi ,viongozi wa kidini ,wakisiasa , taasisi mbalimbali zikiwemo NGO’S, serikali nk.
       pamoja na gharama za elimu kuwa juu bado sio sababu ya kuikosa .kwa kuwa kuna njia nyingi za kuipata elimu mradi kama una nia ya dhati.leo nataka niiongelee hii njia ya udhamini ambayo ndiyo inayotumika na wengi katika kujiendeleza au kujipatia elimu.
Kitu cha muhimu unachotakiwa kufahamu ni kuwa elimu ni lazima bila kujali unamudu gharama au la!chamsingi ni kutafuta njia ya kuipata iwe kwa kutumia udhamini au njia nyinginezo.Endapo unataka kutumia njia ya udhamini unatakiwa kufahamu kuwa lazima uwe na vigezo vitakavyofanya uweze kupata udhamini wa elimu yako.
        Bila kukuchukulia wakati tutaangalia vigezo 12 vinavyoweza kumshawishi mdhamini yeyote kuchukua fedha yake aliyoipangilia kwa shughuli nyingine na kuamua kugharamia masomo yako.
Tazama vigezo vifuatavyo ili uweze kuona kama unaweza kuwa navyo kadhaa na kama sivyo uanze kuvijenga sasa.

(1) UFAULU
 Naweza kusema ufaulu ni kigezo namba moja kwasababu wengi wa wanaodhamini elimu hata bila kutazama vigezo vingine huwa wana tumia kigezo hiki kwa sehemu kubwa. Sababu kubwa ya wadhamini wengi kutazama kigezo hiki ni kutaka kujihakikishia kuwa hawatapoteza fedha yao kwa kumgharamia mtu ambaye hatofanya vizuri au kufeli mwishoni mwa elimu yake.kwasababu hiyo ni muhimu kuutafuta ufaulu mzuri ili kukidhi kuingia katika udhamini wa kundi hili.

(2) NIA
hiki ni kitu kingine cha muhimu sana wanachokiangalia wadhamini bila kujali ni ndugu, taasisi au walezi. Na kinachozingatiwa hasa ni nia ya dhati ya kutaka kuendelea kusoma.Bila kujali kuwa unaufaulu wa kiasi gani katika masomo yako bila nia itakayoonekana wazi wazi kwa mdhamini wako ya kutaka kuendelea na masomo ni vigumu kutoa ushawishi wa kutosha kupata udhamini.Inakupasa kuonyesha nia kuwa huna masihara au si majaribio katika uamuzi wa kusoma uliouchukua.


(3) UTAYARI
Utakubaliana na mimi kuwa kunatofauti kubwa kati ya nia na utayari nikiwa na maana kuwa unaweza kuwa na nia na usiwe tayari.kigezo hiki kinaweza kukuongezea nafasi ya kupata udhamini kwa kuwa wadhamini wengi hupenda kujihusisha na watu walio tayari.Utayari huu utaonekana pale ambapo utaonyesha kuwa tayari kuanza masomo hata kwa kupatiwa mahitaji machache .vilevile utayari wako utathibitika pale ambapo utaonekana ukipunguza shughuli zisizoendana na mambo ya kielimu na kuanzisha shuguli zinazoendana na mambo ya kielimu ,mfano kama muda wako mwingi ulikuwa ukiupoteza kwenye; michezo ya pull table,kusafiri kusalimia ndugu ,kutali,kujirusha( starehe),kucheza karata ,bao,drafti,kutazama movie,bongo flavana mengineyo na badala yake ukaanza kusoma ,vitabu ,majarida ,novel,kutazama vipindi vya kuelimisha runingani,kusoma makala zinazoelimisha kwenye mtandao na magazetini,kuhudhuria semina mbalimbali za kuelimisha,na mambo yanayofanana na hayo.

(4) UTHUBUTU
Hiki ndicho kigezo ambacho kinaushawishi mkubwa sana kwa wadhamini wengi wa maswala ya kielimu.Uthubutu unaweza kuonekana kwa kuanza kufanya jambo litakaloashiria moja kwa moja kuwa umekwisha amua kusoma tena unataka kusoma nini.Unaweza kuonyesha hivyo kwa kuchukua form ya masomo kutoka chuo kinachotoa masomo husika au kujiunga na masomo kwenye chuo husika.Hata hivyo unaweza kuthubutu kuanza masomo kwa njia nyingine ambayo si rasmi ilimradi yatakuwa ni masomo asilia ya kile ulicholenga kukisoma.

(5) UWAZI
Mdhamini yeyote hupenda kumdhamini mtu muwazi afanyaye mambo yake katika dhamira iliyo ya kweli.Katika hili ukweli ndiyo kigezo kikuu cha kumshawishi mdhamini kugharamia masomo yako.Itakulazimu kuwa mvumilivu kuruhusu taarifa zako muhimu kuwa wazi kwa anayekudhamini .Taarifa zote zinapaswa kuwa za kweli ili kutojenga mashaka ya kutapeliwa kwa mdhamini wako hasa kama mdhamini si wa familia yako. Kumbuka kuwa kama taarifa zako zitakuwa hazielewekieleweki au ni za uongo itakuwa ni vigumu kwa mtu yeyote kuwa tayari kuhairisha mipango yake kwa ajili ya elimu yako.Epuka kuficha mambo ambayo yataleta wasiwasi kwa mdhamini wako endapo yatagundulika au kujitokeza baadaye.Mfano wa mambo ambayo yanaweza kukuletea matatizo ni pamoja na ;-

*julisha hali yako halisi ya kiuchumi hata kama sio mbaya sana au kama unaye mdhamini mwingine anayeshughulikia jambo flani katika elimu yako.kufanya hivyo hakutakuwa na athali kwako pale endapo mdhamini wako mkuu atabaini uhalisia wa uwezo wako wa kiuchumi.

*julisha gharama halisi za mahitaji yako na gharama halisi za malipo yote ya chuo au shule unayosoma kwa mdhamini wako.Kufanya hivyo kutasaidia kutomsumbua mdhamini wako kubadilisha bajeti ya udhamini mara kwa mara na kukuona kuwa ni kero.Wakati mwingine imewafanya baadhi ya wadhaminiwa kuona haya baadaye kusema ukweli wa gharama walizoficha awali kwa kuhofia kuwasumbua wadhamini wao na kujikuta wakitumbukia kwenye uongo kitu kinachowatia shaka wadhamini wao juu ya matumizi yao .

(6) UNYENYEKEVU
Hakuna mtu au taasisi yeyote inayotaka kumsaidia mtu yeyote asiyeonyesha au asiye na dalili za unyenyekevu.Unaweza kuonyesha unyenyekevu kwa kuchuliana na changamoto zinazotokana na ucheleweshwaji wa malipo kutoka kwa mdhamini au namna yeyote ya maudhi yanayotoka kwa mdhamini.Namna yeyote ya ubishi ,na lugha za kulazimisha zinaweza kumfanya mdhamini kujitoa au kutokuwa na moyo wa kuendelea na udhamini.

(7) TABIA NJEMA
pamoja na mambo mengineyo lakini tabia njema inaushawishi mkubwa wa kumfanya mtu yeyote kudhamini masomo yako bila hata kutumia nguvu nyingi ya ushawishi.tabia njema inaweza kuwa ni pamoja na lugha njema ,ushiriki katika shughuli za makundi mema ya jamii,kuimarisha amani na utulivu katika mitaa unayoishi,kusaidia wenzako kufikia malengo mema,kuwasaidia watu walio na umri mkubwa,kusalimia kwa adabu watu waliokuzidi umri,kutumia lugha ya kistaarabu,mivao ya kimaadili na yanayofanana na hayo.bila kuwa hata na ufaulu wa hali ya juu unaweza kupata udhamini kutoka mahala popote kwa kigezo hiki cha tabia nyema.

(8) BIDII
Bila shaka hata wewe unapenda mtu mwenye bidii.Mdhamini hatatilia shaka kukudhamini katika masomo yako kama tu utakuwa na dalili zinazoashiria kuwa unabidii katika mambo ufanyayo.Epuka kukaa bila kujishughulisha na lolote katika jamii kwasababu miongoni mwao ndimo anamotoka mdhamini wako.Hakikisha kuwa unakuwa mtu wa kimipango na unaisimamia kikamilifu ili kupata majibu yake.Hii inaweza kuwa ni kuazisha darasa la kufundisha watoto na kuhakikisha kuwa wanafanya vizuri,kuanzisha bustani ndogo ya mboga au matunda mahala unapoisha na kuhakikisha unavuna matunda yake.Azisha kitu hapo mtaani kwako na kukisimamia kikamilifu ili kitoe majibu kitu kitakachofanya kila mtu kukubali kuwa unaweza kujisimamia hivyo hata akikudhamini hutamwangusha.

(9) UVUMILIVU
Mdhamini huwa na furaha zaidi kushirikiana na mtu mvumilivu ambaye anaweza kuyakabili mazingira magumu na kuyamudu .Mazingira magumu yanaweza kujitokeza katika maeneo ya masomo na kusababisha masomo kuwa magumu kiasi cha kuyahairisha.Mtu mvumilivu anaweza kuendelea na masomo hata katika maeneo yasiyo na amani ya kutosha,baridi kali,joto kali,upungufu wa mahitaji, maeneo yenye ubaguzi wa rangi nk.

(10) UMAKINI
Umakini unatakiwa kwa kila mtu lakini kwa mtu anayetaka udhamini wa masomo inaweza kuwa kigezo kikubwa cha kukubalika kirahisi.Mtu anaweza kuonekana kuwa makini endapo atakuwa akipangilia mambo yake kwa ustadi,kukaa katika ratiba ,kutimiza appointment(mfano akiahidi kitu anatimiza kwa wakati,akiitwa anafika kwa wakati),namna anavyoweza kufanya uchaguzi wa vipaumbele vyake;( mfano hachanganyi mapenzi na elimu),anavyoweza kuchagua watu wa kushirikiana nao,anavyoweza kuenenda na wakati;mfano nini afanye wapi na wakati gani nk.

(11) UTULIVU
Unaweza ukahisi kama natoa mafundisho ya kidini lakini huu ndiyo ukweli kuwa utulivu nao ni kigezo cha kumfanya mdhamini yeyote kukukubali.Mtu mtulivu anapendwa kwasababu huwa hana papala akitumia fulsa moja kwa wakati,hujaribu jambo moja mpaka mwisho kabla ya kuhamia katika jambo jingine,hutafakari kila jambo analotaka kulifanya kabla ya kuchua hatua,huwa hana hadithi mbaya ya maisha yake (haambatani na matukio ya skendo ) shida zake huzifahamu watu wachache aliowachagua yeye.

(12) KIPAJI
Kwa kiwango kikubwa wadhaminiwa wengi wanavipaji na vimekuwa ndiyo kigezo kikubwa cha kupata udhamini wao.Ili mtu aweze kuonekana wa pekee ni namna anavyotumia kipaji chake katika maisha yake ya kila siku.Kadili kipaji kinavyokuwa ndivyo upekee unavyozidi kuonekana na kuzidi kutambulika na watu.Unaweza kutambua kipaji chako na kukitumia katika maisha yako ya kilasiku na si punde tu.Kipaji kikidhihirika kinaweza kukufanya kuwa bidhaa adimu.Kwa kuwa watu wote hupenda bidhaa adimu hivyo hawataacha ipotee bure,nawe unaweza kutumia kipaji chako kuwavutia watu kukudhamini katika masomo yako.Kama hujui kama unakipaji gani unaweza kutembelea kwa kubofya hapa  ambapo utaona kurasa inayosema( nifanye nini kabla ya kujiendeleza kielimu) kisha utatazama katika kipengele cha ( utatambuaje kipaji chako.)

Alhamisi, 13 Februari 2014

HISTORIA FORM I &II +QT


                                      Table of Contents
INTRODUCTION TO HISTORY ........................................................................................1
SOURCES OF HISTORICAL INFORMATION............................................................... 2
WAYS TO DETERMINE DATES.................................................................................. 3
EVOLUTION OF MAN TECHNOLOGY AND ENVIRONMENT................................. 4
DEVELOPMENT OF ECONOMIC ACTIVITIES AND THEIR IMPACT ....................5
DEVELOPMENT OF SOCIAL AND POLITICAL SYSTEM.......................................... 6


         1   What is history?    History is the human past activities or is the study of human transformation in different times according to his nature and surroundings.
{Nini maana ya historia? Historia ni shughuli za kibinadamu zilizopita au elimu inayohusu  mabadiliko ya kimaumbile ya binadamu katika  nyakati tofauti tofauti  kutokana na asili ya mazingira yake na yale yanayomzunguka.}

what is the importance of studying history{Nini umuhimu wa kujifunza historia?}

(i)History helps us to know our past:  { historia hutusaidia kujua tulikotoka}
 by knowing our past we will be able to improve the present and plan for the future{kwa kujua tulikotoka tutaweza kuboresha hali yetu ya sasa na kujipanga kwaajili ya siku zijazo}

(ii) History helps us to understand mans struggle in mastering his environment{ historia hutusaidia kuelewa jitihada za binadamu katika kabiliana (kudhibiti) na mazingira yake}

(iii)History helps us to know technological changes in human life.{historia hutusaidia kujua mabadiliko ya kiteknologia katika maisha ya binadamu}  Example from

 Stone Age to Iron Age.  {zama za mawe hadi zama za chuma}
(iv) History helps us to understand the relationship among people in deferent period and environment. {historia hutusaidia kuelewa uhususiano wa watu katika vipindi tofauti tofauti na mazingira tofauti tofauti.}

(v) History helps us to gain knowledge in solving the conflicts in the society{historia hutusaidia kupata ujuzi wa kutatua migogoro katika jamii .}

(vi) History helps us to make research in deferent problems in our society.{historia hutusaidia kufanya utafiti katika matatizo tofauti tofauti katika jamii}

       (2.0) OUTLINE FIVE SOURCES OF HISTORICAL INFORMATION {elezea vyanzo vitano vya historia}

(i) Oral tradition{ njia asili ya masimulizi }
(ii) Museums{majumba ya makumbusho} 
(iii)Historical sites{maeneo ya kihistoria}  
(iv)Archives {nyaraka} 
(v)archaeology{akiolojia au elimu kale}

(i)Oral tradition {njia asli ya masimulizi }
Oral tradition is the source of history which involves the passing of information .i.e. by talking and listening_.{njia asili ya masimulizi ni chanzo cha kihistoria kinachojumuisha upsianaji wa taarifa sanasana kwa kuzungumza na kusikiliza.}
         (i.a)Advantages of oral tradition{manufaa ya njia asili ya masimulizi}

   (1)Oral tradition helps to get information which is not recorded in written document.{njia asili ya masimulizi hutusaidia kupata taarifa ya kile ambacho hakikurekodiwa au kuwa katika hali ya maandishi.}

  (2)It is easier and cheaper method of getting historical information than any other method{ni njia nafuu ya kupata taarifa za kihistoria kuliko njia nyingine yeyote}

(3) It includes both literate and Illiterate people{inahusisha watu wa aina zote wenye elimu na wasio na elimu.}

         (i.b)disadvantages of Oral tradition {madhara ya njia asili masimulizi }

  (1)The Original information may be distorted due to change of narrators.{taarifa asilia zinaweza kubadilika kutokana na kubadilika kwa wasimulizi.}

  (2)It needs much of attention of the listener.{inahitaji umakini mkubwa sana wa msikilizaji }

  (3) most of narrators use their languages; therefore other people may not understand.{wasimulizi wengi hutumia lugha zao ,hivyo watu wengine wanaweza wasielewe}

  (4)In most cases the stories narrated are of few past generation and not those of our great –great fathers{katika visa vingi vya hadithi zilizosimuliwa ni za vizazi vichache vilivyopita na si! za mababa wa kale.}

(ii)  Museums are  the areas established especially for preserving different historical information and object. Examples of museums are the national museums of Tanzania and Kalenga museum in Iringa  {majumba ya makumbusho ni maeneo yaliyoanzishwa mahususi kwa lengo la kutunza taarifa za kihistoria pamoja na vielelezo.}mifano ya makumbusho ni makumbusho ya taifa ya Tanzania na makumbusho ya kalenga iringa}

      (ii.a)advantages of museums {manufaa ya majumba ya makumbusho}
  (1)they help people to get historical information{husaidia watu kupata taarifa za kihistoria}

  (2)they describe culture of particular society{husaidia kuelezea utamaduni wa jamii Fulani}

  (3)they attract tourism.{huvutia utalii}

           (ii.b)disadvantages of museums{madhara ya majumba ya makumbusho}
 (1) Some of museums are located far away from reach of ordinary people{baadhi ya makumbusho yako mbali na hayawezi kufikiwa na watu wa kipato cha kawaida}

 (2)Many people can not afford museums fees{watu wengi hawawezi kumudu gharama za makumbusho}

(3) IIIiterate people can not afford {watu wasio na elimu hawawezi kumudu}

             (3.i)Four ways of determining dates in History
(a)recalling events: This is the way of remembering important events like famine ,floods and so on. {kukumbuka matukio: hii ni njia ya kukumbuka matukio muhimu kama njaa,mafuriko na mengineyo.}

(b)Chronology: It involves arrangements of events according to their order of occurrence.{(wendo au utaratibu wa kupanga miaka na matukio)huhusisha upangaji wa matukio kutokana na mfurulizo wa utokeaji wake}

(c)by studying language  e.g the words Rahim and Marahaba  remands us the coming of Arabs in Est Africa Cost{kwa kujifunza elimu ya lugha }mfano wa maneno kama Rahimu na marahaba yanatukumbusha ujio wa waarabu katika Afrka Mashariki}

(d)Carbon 14 : is the scientific way of dertemining dates of remains of plants and animal died over past 5000 years ago .{carbon 14:ni njia ya kisayansi ya kutambua au kubaini umri wa masalia ya mimea au wanyama waliokufa kiasi cha zaidi ya  miaka 5000 iliyopita}

      ( 3.ii) How Historians divide time in dating historical events {namna gani wanahistoria hugawanya wakati katika kupangilia tarehe za matukio ya kihistoria}

The following are the categories of determining time in history{yafuatayo ni makundi ya ubainishaji wa wakati katika historia}

(1)A day –is a duration of twenty four hours{siku- ni kipindi cha masaa ishirini na nne}

(2)A week –is a duration of seven days{wiki-ni kipindi cha siku saba}

(3)A month is a period of four weeks{mwezi-ni kipindi cha wiki nne}

(4)A Year –is a period of twelve months {mwaka-ni kipindi cha miezi kumi na mbili}

(5)A decade-is a duration of ten years{muongo-ni kipindi cha miaka kumi}

(6) A century-is a duration of hundred years {karne-ni kipindi cha miaka mia moja}

(7) A millennium –is a duration of thousands years{millennia-ni kipindi cha miaka elfu moja}

(8) A generation is the everage defences in age between a child and or her parents .{kizazi-ni wastani wa tofauti ya umri kati ya motto na wazazi.}

      (3.iii)  what is the meaning of the following {nini maana ya haya yafuatayo}  

(1)   A D-means the year of the LORD (ANNO DOMINO){A D-inamaanisha mwaka wa bwana}

(2)B C-means years before Christ{B C- inamaanisha miaka kabla ya krito}
(3)HIJRA Is the moslems starting date (the time Mohamed fled from mecca to medina.{(hijra ni tarehe ya kuanza kwa mwaka wa kiislamu)ni wakati ambao Mohamed alikimbia kutoka mecca kwenda madina }

       (3.iv)   Describe three ways used to show chronological order events ,period and age.{elezea njia tatu zilizotumika kupangilia matukio wakati na umri}                                                                                                           
A TIME CHART{chati ya wakati}



TIME GRAPH  {grafu ya wakati} 

                                                                                         
                                                                                       
C TIME LINE



(4.0) EVOLUTION OF MAN. TECHNOLOGY AND ENVIRONMENT. {mageuko ya binadamu.teknologia na mazingira}

 (4.1) Two theories that attempt to tell (explain) the original of man  {thiologia   aina mbili zinazo jaribu kusema(kuelezea) asili ya binadamu}

(1.i)creation                       {  uumbaji}    
(1.ii)evolution of man     { mabadiliko ya kimaumbile}

       (1.i) EVOLUTION OF MAN      {mageuko ya binadamu}
Evolution of man is gradual change of man from lower stage to better stage adapted to environment.{mageuko ya binadamu ni mabadiliko(akimaumbile) endelevu ya binadamu kutoka katika hali duni hadi bora yaliyoendana na mazingira}

(1) The first family of man was called PRIMATES  {familia ya kwanza ya binadamu iliitwa PRIMATES}

(2) The transition of man from using four limbs is called bipedalism {mpito wa binadamu  kutoka katika kutumia miguu mine unaitwa bipedalism}

(4.2)  Four stages of man evolution include;  {hatua nne za mageuko ya binadamu zinajumuisha,}

(1)           Primates e.g apes and chimpanzee they walked by four limbs and they had low mental ability {primates, mfano nyani na sokwe walitembea kwa kutumia miguu minne na kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri}

(2)         (AUSTRALOPITHECUS AFRICANS 
           (a)zinjanthropus 
            (b)homo habilis

(3)         HOMO ERECTUS:( an up straight walking man)(mtu aliyeweza kusimama wima)

(4)         HOMOSAPIENS (The highest stage in mans evolution){hatua ya juu katika mageuko ya binadamu}









(4.3) The skull of the one eariest man was discovered 1959 {fuvu la mmoja wa wanadamu wa kale zaidi lilivumbuliwa mnamo mwaka 1959}


(4.4) The skull of the eariest man was discovered  Dr. Louis Leaky  {fuvu la binadamu wa kale zaidi lilivumbuliwa na Dr.Louis leaky}

(4.5)  the skull of the early man was discovered in olduvai George {fuvu la binadamu wa kale zaidi lilivumbuliwa Olduvai George.}

(4.6.0) What is the Stone Age? {Zama za mawe ni nini?}

It was  the historical period where man made and used the stone tools technology{ni kipindi cha kihistoria wakati ambapo binadamu alitengeneza zana kwa kutumia technologia ya mawe}

(4.6.1) Three stages of stone age {hatua tatu za zama za mawe}

(1)Early stone age  {zama za mawe za kale } 
(2)middle stone age {zama za mawe za kati}  
(3)then late or new stone age  {zama za mawe za mwisho}

(1)early stone age the first phase of stone age which existed between 1,750,000 BC and 750,000 BC.{zama za mawe za kale hatua ya kwanza ya zama za mawe zilikuwako kati ya 1,750,000 kabla ya kristo na 750,000 kabla ya kristo.}

(1.0) five characteristics of early stone age {tabia au sifa za zama za mawe za kale}
(i)            man was able to make and use simple stone tools {binadamu aliweza kuunda na kutumia zana rahisi za mawe}

(ii)        The tools made were heavy and  blunt  which were chopping and peddle tools {zana zilizotengenezwa zilikuwa nzito na butu ambazo zilikuwa zimechongoka na pana}

(iii)     The main activities of man were hunting and gathering.{shughuli kuu za binadamu zilikuwa ni kuwinda na kukusanya}

(iv)          Man had no permanent settlement{binadamu hakuwa na makazi ya kudumu}

(v)             Man ate raw food because there were no fire yet  {binadamu alikula vyakula vibichi kwasababu bado kulikuwa hakuna moto}
                                       
       (1.1)three areas in east Africa where chopping and peddle tools were found .{maeneo matatu katika Afrika mashariki ambapo zana za kuchongoka na pana zilipatikana }

(i)were {zilikuwa} Olduvai George 
(ii)Nsongezi   
(iii)Olorgesailie
        (2) Middle stone age {zama za kale za kati}
It was the second phase of stone age which existed between 750,000 and 50,000 BC. {ni hatua ya pili ya zama za mawe ambayo ilikuwako kati ya miaka 750,000 na 50,000 kabla ya kristo.}

             (2.1) The important change during the middle stone age was discovering of fire{mabadiliko muhimu wakati wa kipindi cha zama za kati za mawe yalikuwa ni kugundulika kwa moto}



(2.2) five uses of fire to man are;-{matumizi matano ya moto kwa binadamu yalikuwa ni:-
(i)              Man used fire to warm up himself {binadamu alitumia moto kujipa joto yeye mwenyewe}

(ii)           Man used fire to roast and chase wild animals
{binadamu alitumia moto kuivisha na kufukuza wanyama wa mwitu}

(iii)        Man used fire to fall down big trees and clearing the bushes{binadamu alitumia moto kuangusha miti mikubwa na kusafisha vichaka}

(iv)         Fire provided light at night{moto ulileta mwanga wakati wa usiku}

(v)            Man used fire to chase wild animals {binadamu alitumia moto kufukuza wanyama wa mwitu}

(3)    the late stone age  {zama za mwisho za mawe}

  It was third phase of the stone age which stated from 50,000 to the first millennium.{hii ni hatua ya tatu ya zama za mawe iliyoanzia miaka ya 50,000 mpaka millennia ya kwanza.}
         (3.1) five characteristics of late stone age {tabia au sifa za zama za mawe za mwisho}

(i)            Tools were improved  {zana ziliboreshwa}

(ii)        Man started to live in permanent settlement  {binadamu alianza kuishi katika makazi ya kudumu}

(iii)     Man started cultivation of crops {binadamu alianza kupanda mazao}

(iv)      Man started to domesticate animals   {binadamu alianza kufuga wanyama}

(v)         Man started activities like painting and drawing {binadamu alianza shughuli za  kunakshi na kuchora}

( 4.7.0)                                IRON AGE    {zama za chuma}
Was the period when man discovered and started to make and use Iron tools {ulikuwa ni wakati ambao binadamu aligundua na kuanza kutengeneza na kutumia zana za chuma}

(4.7.1)   the advantages of Iron discovery.   {Manufaa ya ugunduzi wa chuma}

(i)      There were improved tools compared to the stone age{zana ziliboreshwa kulinganishwa na zana za mawe}

(ii)           Iron tools made cultivation of crops easier{zana za chuma zilifanya upandaji wa mazao kuwa rahisi}

(iii)        Iron increased production{chuma kiliongeza uzalishaji}

(iv)         It led to presence of surplus{ilipelekea kuwepo kwa ziada}

(v)            It promoted trade (barter trade){iliamsha biashara (biashara ya mabadilishano)
(vi)         It led to population growth {ilipelekea kuongezeka kwa idadi ya watu}

(vii)      It led to specialization e.g. people could become witch
 {doctor,Rainmakers,traders (barter trade){ilipelekea ufanyaji kazi maalumu mfano mtu aliweza kuwa mganga wa kienyeji, mtengeneza mvua,mfanya biasha (biashara ya mabadilishano)

(viii)                     It influenced the beginning of political institution like Kinship,state organization and so on.{ilvutia kuanzishwa kwa taasisi za kisiasa kama udugu,tawala za ushirikiano wa dola  na mengineyo}

(ix)      It led to increase of defence and security {ilipelekea kuongezeka kwa ulinzi na usalama}

(4.7.2) The famous early iron sites in East Africa {maeneo maarufu ya mwanzo ya chuma Afrika mashariki}

(i)              Karagwe 
(ii)ugweno in same district(ugweno katika wilaya ya same 
(iii)the western shores of lake Victoria (magharibi mwa fukwe za ziwa viktoria}

                                                            Topic  3
      (5.0)  DEVELOPMENT OF ECONOMIC ACTIVITIES AND THEIR IMPACT {Maendeleo ya ya shughuli za kiuchumi na (athari) matokeo  yake}

(5.1)    Development is the progressive change from lower stage of life to advanced one{maendeleo ni mabadiliko endelevu kutoka hatua duni ya kimaisha hadi iliyo ya hali ya juu}

(5.2)    Three economic activities practiced by man in pre-colonial societies were{shughuli tatu za kiuchumi zilizotekelezwa na binadamu katika jamii za ukoloni wa awali:-

 (i) Agriculture    {kilimo}   
(i)Trade        {biashara}    
(i)industry    {uzalishaji mali}

(5.3)   four types of agriculture practiced  during the  pre-colonial East Africa societies were;- {Aina nne za kilimo zilizo tekelezwa mwanzoni mwa ukoloni Afrika mashariki zilikuwa:,

(i)              Parmanent crop cultivation    {kilimo cha mazao ya kudumu}
(ii)           Mixed farming            {kilimo  mchanganyiko}
(iii)        Shifting cultivation        {kilimo cha kuhamahama}
(iv)         Pastoralism       {ufugaji}

 (5.4) Difference between shifting and permanent crop cultivation  [Tofauti ya kilimo cha mazao cha kuhama hama na cha kudumu}

(i)  Shifting cultivation is the type of cultivation where by people moved from one place to another (in shifting cultivation people cultivate short time crops like maize and millet){ Kilimo cha kuhamahama ni kilimo ambacho watu walikuwa wakihama kutoka eneo moja hadi jingine(katika kilimo cha kuhamahama watu walilima mazao ya muda mfupi kama mahindi na mtama)}

(i)  Permanent cultivation is the type of cultivating permanent crop (in permanent cultivation people grow banana and coffee){kilimo cha kudumu ni kilimo cha kulima mazao ya kudumu(katika kilimo cha mazao ya kudumu watu walipanda migomba na kahawa.)}

(5.5)    four areas in East Africa where permanent cultivation was practiced{Maeneo manne katika Afrika mashariki ambayo kilimo cha kudumu kilitekelezwa :-
(i)     KILIMANJARO 
(ii)KAGERA  
(iii) KENYA HIGHLAND 
(iv)BUGANDA

      (5.6)   Mixed farming ;-Is the type of agriculture that involve crop cultivation and animal keeping.{KILIMO MCHANGANYIKO; ni aina ya kilimo ambayo inajumuisha upandaji wa mazao na ufugaji wa wanyama.}

(5.7)   Example of three societies which practiced mixed farming in Tanzania {mifano ya jamii ambazo zilitekeleza kilimo mchanganyiko Afrika mashariki }

(i)SUKUMA   
(i)FIPA  
(i)SANGU
Pastoralizsm;-pastoralism is the type of agriculture which involves livestock keeping  {ufugaji ni aina ya kilimo inayo husisha utunzaji wa mifugo}

(5.8)  five examples of the pastoral societies in Africa {mifano ya jamii za kifugaji katika afrika:-

(5.9)  Examples of three societies that practiced mixed farming in Tanzania{mifano ya jamii tatu zilizotekeleza kilimo mchanganyiko }
(i)KEREWE 
 (ii) MAKUA 
 (iii)YAO
(5.10)  Four examples of handchraft industries in pre-colonial Afrika {mifano minne ya viwanda vidogo vya uzalishaji mali  mwanzoni mwa uloloni Afrika}

(i)              Salt making industries  {viwanda vya utengenezaji chumvi}
(ii)           Cloth making industries   {viwanda vya uzalishaji nguo}
(iii)        Iron industries         {viwanda vya chuma}
(iv)         Gold mining industries {viwanda vya uchimbaji dhahabu} 

(5.11)   three Areas were gold was found in Africa {Maeneo matatu ambayo dhahabu ilipatikana katika Afrika}

 (i)gold coat  
(ii)Shona area 
(iii)Mwanemutapa

(5.12)   People who specialized in Iron work were called BLACK SMITHS {watu waliokuwa wakifanya shughuli za chuma kama shughuli maalumu waliitwa black smiths.(wakiwamaanisha mfua chuma}

(5.13) Three societies which involved themselves in iron work in pre-colonial Afrika were;- {jamii tatu zilizojihusisha na shughuli za chuma mwanzoni mwa ukoloni afrika zilikua:-

(i)              Fipa of sumbawanga in Tanganyika{wafipa wa sumbawanga Tanganyika }

(ii)           Nubia people of sudan  {watu wa nubia wa sudani}

(iii)        Shona of southern Rhodesia{washona wa rodesia ya kusini}

(5.14) the first common type of trade existed in pre-colonial Africa was BARTER  TRADE{Aina ya kwanza maarufu  ya biashara iliyojitokeza mwanzoni mwa ukoloni Afrka ilikuwa ni biashara ya mabadilishano}


(5.15)  THE  MEANING OF THE FOLLOWING ;-{maana ya yafuatayo
(I) part lineal society      {jamii ziliegemea kwa bwana au baba }.                       (I)matrilineal societies    {familia zilizoegemea kwa bibi au mama}
Artlineal society was the society in which clan heritage was based on the father {jamii ziliegemea kwa bwana(baba) ni jamii ambazo hazina ya ukoo iliegemea kwa baba}

E.g. Children belong to the father’s clan  {mfano watoto walikuwa ni mali ya ukoo wa baba}

MAtrilinieal  society was the society in which clan heritage was based on mother’s  clan eg.children belonged to mothers’ clan e.g  among MWERA and YAO people{Jamii zilizoegemea kwa bibi ( mama)  zilikuwa ni jamii ambazo hazina ya ukoo ilikuwa ikiegemea zaidi kwa mama}

(5.16)   Barter trade ;{biashara ya mabadilishano}(-was the system of exchanging goods with other goods){ilikuwa ni biashara ya kubadilishana bidhaa kwa bidhaa}

(5.17)  two major types of trade developed in pre-colonial African societies were;  {Aina kuu mbili za biashara zilizoendelea katika jamii za mwanzoni mwa ukoloni}

(i)              Local trade  {biashara za kawaida}
(ii)           Region trade{biashara za kikanda} (long distance trade){biashara ya masafa }

  (5.18)         DEFENITION OF LOCAL TRADE  {ufafanuzi wa bishara ya kawaida}

(i)              Local trade was the trade which involved exchange of goods within society or community eg pastoralists could exchange cattle with crops like maize and millet.{biashara ya kawaida ni biashara iliyohusisha ubadilishanaji wa bidhaa ndani ya jamii au jumuia. Mfano wafugaji waliweza kubadilishana na mazao kama mahindi na mtama.}

(ii)           Regional trade (long distance trade) was the trade which involved  people from different (far regions eg the people of East Africa and those from Central Africa.{biashara ya kikanda (biashara ya masafa) ni biashara iliyohusisha watu kutoka maeneo tofauti tofauti ya mbali.mfano watu wa Afrka masharika na wale wa Afrika ya kati.}

(5.19)  Examples of three East African societies that participated in long distance Trade and the goods exchanged were;-  {mifano mitatu ya jamii za afrika mashariki  zilizoshiriki katika biashara za masafa na mabadilishano zilikuwa;}
(i)              Yao             
(ii) Nyamwezi      
(ii)           Kamba  
 ,they exchanged ivory slave and  copper with cloth,porcelain and ornaments from ASIAN Trades{zilibadilishana pembe za ndovu,watumwa,na shaba kwa kupata nguo,vitu vya mng’ao (kaolini) na mapambo kutoka wafanya biashara wa asia}
(5.20)    The effect of long distance trade(LTD) to the people of East Africa {matokeo ya biashara masafa (LTD)kwa watu wa Afrika mashariki }

(i)                The exploitation of African wealth through unequal exchange{unyonyaji wa thamani ya bidhaa za kiafrika kupitia ubadilishanaji usio na usawa}

(ii)             It promoted slave trade
(iii)        It led to growth of kingdoms like Buganda and Mirambo empire{ilipelea kukua kwa falme kama ya Buganda na himaya ya mirambo}

(iv)         The rise of Swahili language in the interior of East Africa.{kuinuka  kwa Kiswahili ndani ya ukanda wa Afrika mashariki}

(v)            It led to growth of towns like Ujiji.{ilipelekea kukua kwa miji kama ujiji}

(vi)            Spread of Arab culture in East Africa eg  building and wearing styles.[kusambaa kwa utamaduni wa kiarabu katika afrika mashariki  mfano majengo na uvaaji.}

(vii)      Intermarriage between Africans and Arabs.{mwingiliano wa kindoa kati ya waarabu na waafrika.}

(viii)   Disintegration of families due to slave trade {kuvunjika kwa familia kutokana na biashara ya utumwa}

(5.21)   Define Trans Saharan Trade.   {fafanua biashara kupitia Sahara}
  Trans Sahara  trade was the trade conducted across the Sahara desert before 8th century between western Sudan and North African societies.{biashara ya kupitia sahara ilikuwa ni biashara iliyofanywa kupitia njangwa la sahara kabla ya karne ya nane.}

(5.22)  Examples of goods exchanged during trans sahara trade.{mifano ya bidhaa zilizobadilishwa wakati wa biashara ya kupitia sahara}

(a)  Gold,{dhahabu}  cola nuts,{mbegu za kola (mimea yenye kemikali ya kafeni)}   food stuff ,[vyakula}  Ivory,  {pembe za ndovu}  bee wax {nta}  and Ostrich feathers from north Afrika.{na manyoya ya mbuni kutoka afrika kaskazini}

(b)                        Salad and animal skins from North Africa {saladi{mfano wa kachumbali} na ngozi za wanyama kutoka afrika ya kaskazini}

(c) Cotton ,{pamba}Silk{ Hariri}  ,Guns{silaa}, Cloth {Nguo} ,beads{shanga} ,and Horses from Europe and Asia {na farasi kutoka ulaya na asia.}

(5.23)   The effect of trans Sahara Trade includes  {matokeo ya biashara ya kupitia sahara  ni pamoja na}:-

(i)                Growth of towns like  Gao Timubuktu and walato  {Kukua kwa miji kama Gao,Timbuku na Walato.}

(ii)             The rise of some of Empires like Mali Ghana and {Soghai {Kuinuka kwa baadhi ya himaya kama Mali,Ghana na Songai.}

(iii)           Introduction of Arabic administrative system in West  Africa {Kuingia kwa utaratibu wa utawala wa kiarabu katika Afrka Magharibi.}

(iv)            Unequal trade .  {Biashara isiyokuwa na usawa}

(v)             Intermarriage and emergence of  mulattoes  
               {Mwingiliano wa kindoa na dharula za uchotara}

(vi)         Development of education for instance there were Quranic  schools and Timbuktu Univesty was established.{Maendeleo ya elimu mfano kulikuwa na shule za kiislamu na chuo kikuu cha Timbuku kilianzishwa }

(6 .0)  THE DEVELOPMENT OF SOCIAL AND POLITICAL SYSTEM {maendeleo ya kijamii na mifumo ya kisiasa}

(6.1)   Five major types of social organization emerged in Africa by 16th century {Aina kuu nne za ushirika wa kijamii zilizopatikana Afrka katika karne ya 16}

(i)              Clan  |kinship organization {ushirika wa kikoo/kidugu

(ii)           Age set organization {ushirika wa kirika }

(iii)        Ntemiship organization  {ushirika wa  kitemi}

(iv)         State of kingdom  {utawala wa kifalme}

(v)            Sultanate   {usultani}

(6.2)  CLAN ORGANIZATION :It was the social organization which consisted of several blood related families  {ushirika wa kikoo: ulikuwa ni ushirika wa kijamii uliotokana na familia kadhaa zenye damu moja}

(6.3) The function of clan Head were;-{kazi za mkuu wa koo zilikuwa;}

(i)              To control clan properties like land and forest  {kusimamia mali za koo kama mashamba na misitu}

(ii)           To control all religious ceremonies {kusimamia sherehe zote za kidini {kiibada}

(iii)        To decide and settle disputes arose among the clan members {kuamua na kutuliza mabishano au mashindano yaliyoibuka miongoni mwa wanaukoo}

(6.4) two types of clan organization  {aina kuu mbili za ushirika wa koo}
(i)              Part lineal clan organization  {ushirika wa koo zinazoegemea kwa baba(bwana)}

(ii)           Matrliineal clan organization  {ushirika wa koo zinazoelekea kwa mama(bibi)

(6.5)  Age set organization;-was type of social and political organization which based on age and sex It was mainly practiced among pastoral societies.  {ushirika wa kirika: ulikuwa ni aina ya ushirika wa kijamii na kisiasa ambao uliegemea katika umri na jinsia,ulitumiwa zaidi na jamii za kifugaji}

(6.6) five examples of pastoral societies with age set  organization {Mifano mitano ya ya jamii za kifugaji ambazo zilikuwa na ushirika wa kirika }

(i)              Maasai
(ii)           Nyakyusa
(iii)        Kikuyu       
(6.7)  An example of distribution of duties according to age and sex are:-{mifano ya mgawanyo wa majukumu kutokana na umri na jinsia }

   (a)          Children of up to 8 years were non –producers  {watoto chini ya miaka 8 walikuwa si wazalishaji}

    (b)         Youth group between the age of 8 to 18 years Their responsibilities were to graze animal and milking cattle while assisted by women {kundi la vijana umri kati ya miaka 8 na 18 walikuwa na jukumu la kuchunga kukamua maziwa wakisaidiwa na wanawake}

    (c) Moran group of age 18 to 35 were the soudiers of the society   {morani kundi la miaka 18 hadi 35 walikuwa asikari wa jamii}

    (d)         Elders group ,aged 35-75 they were to control livestock and other communication properties  {kundi la wazee miaka 35 hadi 75 walikuwa wasimamizi wa mifugo vifaa vingine vya mawasiliano}

               They were leaders of spiritual matters {walikuwa viongozi wa maswala  ya kiroho}

               They were to maintain peace and orders in the society {walikuwa wakidumisha amani na amri katika jamii}

(6.7)     Four function of morani  in age set  system of maasai  {kazi nne za morani katika mpangilio wa kirika kwa wamasai}

(i)              To defend the community against the enemies  {kulinda jumuia dhidi ya maadui}

(ii)           To seach for water and pasture for the animal  {kutafuta maji na malisho kwaajili ya wanyama}

(iii)        To increase the number of cattle by seizing cattle from other societies {kuongeza idadi ya ng’ombe kwa kuteka au kukamata ng’ombe kutoka jamii nyingine}

(iv)         To help to collect tributes from the traders passing through maasai land {kusaidia kukusanya ushuru kutoka kwa wafanya biashara waliokuwa wakipita katika ardhi ya wamasai}

(6.8) Ntemiship organization. {uhirika wa kitemi}
Ntemiship was the type of social and political organization practiced among Nyamwezi,  SUKUMA and Kimbu people by 1300 AD.{utemi ilikuwa ni aina ya ushirika wa kijamii na kisiasa ambao ulitumika kati ya Wanyamwezi,Wasukuma na Wakimbu kati ya miaka 1300 baada ya kristo.}

(6.9)   Responsibilities of  Ntemi  {majukumu ya mtemi}
(i)            To control all political matters  {kusimamia maswala yote ya kisiasa}

(ii)        To divide the land  i.e KUTEMA  {kugawanya ardhi mfano KUTEMA}

(iii)     To devece  and settle conflicts in the society {ku…..na kutatua migogoro katika jamii}

(iv)      To control religious matters like giving sacrifice to the spirits  {kusimamia maswala ya kidini kama kutoa sadaka kwa mizimu}

(v)         To collect tributes from his people   {kukusanya kodi kutoka kwa watu wake}

(6.10)   State Organization   {utawala wa dola}
State is the community which defined territory with full control of its government .{Dola ni jumuia ambayo imejitangazia eneo likiwa na serikari yake kamili}

State organization started around 15th  century due to the development of iron technology.{ushirika wa kidola ulianza katika karne ya 15 kutokana na maendeleo ya tecknolojia ya chuma}

(6.10)  form of the state organization and political leaders  (Title) in East Africa  {muundo wa shirika za kidola na majina ya viongozi wa kisiasa katika afrika mashariki}

Examples:- { mifano}
(a)              Among hehe ,  Sangu  ,and    Bena  political  leaders was called MTWA{miongoni mwa wahehe,wasangu,na wabena kiongozi wa kisiasa aliitwa Mtwa}

(b)              In Kagera political reader was OMUKAMA {kagera kiongozi wa kisiasa aliitwa OMUKAMA}

(c) In Buganda political leader was called  KABAKA  {Buganda kiongozi wa kisiasa aliitwa KABAKA}

(d)              In Rwanda and  Burundi political leader was called MWAMI {Rwanda na burundi kiongozi wa siasa aliitwa MWAMI}

(e) Along the coastal area political leader was called MWINYI  {Maeneo ya mwambao kiongozi wa siasa aliitwa MWINYI}

(6.11)   Four feudal relations developed in East Africa  {aina nne za uhusiano wa kikabaila zilizoendelea  (kuendelezwa)  Afrika Mashariki}

(i)     UBUGABIRE 
(ii)    NYARUBANJA
(iii)   MVUNJO  
(iv)    UMWINYI

(6.12)   FACTORS FOR STATE FORMATION {vigezo vya kuundwa kwa dola}
(I)              Good leadership  like MIRAMBO of nyamwezi empire {utawala bora kama wa Mirambo katika himaya ya wanyamwezi}

(II)          Good climate  e.g  presence of rainfall and soil fertility  {hali ya hewa nzuri mfano uwepo wa  mvua na ardhi yenye rutuba}

(III)       Trade e.g long distance Trade like trans sahara  trade.{biashara ya masafa mfano biashara ya kupitia sahara} 

(IV)       Iron Technology  {tecnologia ya chuma}

(V)           Wars  conguest {mateka wa vita}

(6.13)  what were the factors for the rise of Buganda kingdom ?  {vigezo vipi vilikuwa ndo sbabu ya kuinuka kwa ufalme wa kabaka}

(I)              geographical factors eg rainfall and fertility.{vigezo vya kijiografia kama mvua na rutuba}

(II)          Strong leadership of kabaka {nguvu ya utawala wa kabaka}

(III)       Decline of bunyoro gave rise to BUGANDA kingdom {kufifia kwa bunyoro kuliinua ufalme wa kabaka}

(IV)       Conquest  {mateka}

(V)           Tributes from the people within the kingdome { ushuru kutoka miongoni mwa watu wa ufalme}

(6.14)  Differentiate between centralized state and non centralized state {tofautisha kati ya dola kuu  na dola isiyo kuu }
Centralized state is the state of which includes large area  ruled by king with many tribe  while non centralized state includes small area ruled by the chief with only one tribe.{dola kuu ni dola inayo jumuisha eneo kubwa linalotawaliwa na mfalme likiwa na makabila mengi na dola isiyo kuu ni dola inayojumuisha eneo dogo linalotawaliwa na chifu likiwa na kabila moja.}  
      kwa maswali au maoni au kutumiwa masomo haya kwa format ya pdf tumia anwani na simu iliyopo katika blog.