Jumatatu, 31 Machi 2014

TAASISI MUHIMU ZINAZOSIMAMIA ELIMU TANZANIA


                                KUTEMBELEA BOFYA JINA LA TAASISI

MoEVT Ministry of Education and Vocational Training (Wizara ya elimu na Mafunzo ya ufundi)

CA Continuous Assessment   (sio rasmi)

CBO's Community Based Organisations    (Taasisi ya maswala ya Kijamii)

CSEE Certificate of Secondary Education Examination   (mtihani wa kumaliza elimu ya sekondari)

EFA Education For All      (Elimu kwa Wote  bank ya dunia)

EMAC Educational Materials Approval Committee    (wizara ya elimu)

ESDP Education Sector Development Programme   (sekta ya mpango wa maendeleo ya elimu bank ya dunia 

ESR Education for Self Reliance  (Elimu ya kujitambua)

ETP Education and Training Policy (chanzo wizara ya elimu  MoEVT)

MoEC Ministry of Education and Culture    (wizara ya elimu na utamaduni  Nje)

NECTA National Examination Council of Tanzania   (Maraza la Mtihani la Taifa)

NGO's Non Governmental Organisations<-( twaweza)  ( haki elimu hapa)

NSGRP National Strategy for Growth and Reduction of Poverty
Mpango wa Maendeleo na Kutokomeza Umasikini)

SEDP Secondary Education Development Programme (mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari)

TIE Tanzania Institute of Education  (Taasisi ya Elimu Tanzania)

UNESCO United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization   (shirika la kimataifa)

TCU Tanzania Commission for Universities   (Tume ya Vyuo vikuu Tanzania)

NACTE National Council for Technical Education   (Baraza la elimu ya ufundi tanzania)

IAE     Instituti of Adult Education    (Taasisi ya Elimu ya Watu wazima Tanzania)

TLSB Tanzania Libraly service board   (Bodi ya Huduma za maktaba Tanzania)

HESLB  Higher Education Student Loan Board   (Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Tanzania)

Jumapili, 30 Machi 2014

ORODHA YA VYUO VIKUU TANZANIA

           BOFYA KUTEMBELEA

KALENDA YA MWAKA MZIMA YA SEKONDARY 2014 HII HAPA

TERM YA KWANZA

 First-quarter (robo ya kwanza) :Tuesday 14th  Jan. ‘14 - Friday   21st   Mar.’14   49   (10 weeks)

Mid-term Break (likizo ndogo) : Saturday 22nd Mar ‘14 - Sunday 30thMar ‘14            (1 week)

 2nd  Quarter  (robo ya pili) :       Monday 31st Mar ’14 -Friday 6thJune ‘14          46    (9 weeks)

Holidays  ( Likizo): Saturday 7th June ‘14    -    Monday 7th   July ‘14                          (4 weeks)

                                                                                                                                  95

TERM YA PILI

3rdQuarter (Robo ya tatu)  : Tuesday 8th  July  ‘14 -   Friday 19th  Sept ’14           51    (10 weeks)

Midterm Break (likizo ndogo) : Saturday 20th  Sept. ’14 - Sunday 28thSept. ’14            (1 week)

4thQuarter   (Robo ya nne):         Monday 29th  Sept.’14 - Friday 5th Dec. ’14       49    (10 weeks)

Vacation: (mafunzo)     Saturday 6th December‘14- Monday 12th   Jan. ’15                   (5 weeks)

                                                                                                                                  100

                                                        Total working days (jumla ya siku za kazi)  = 195
                                                        (1 week =5 working day) ( wiki 1= siku 5 za kazi)

PUBLIC HOLIDAYS  2014  (SIKUKUU ZA KITAIFA  2014 )
 
 January  ..          .....                         ..                    ..                      ..              ..     1st   New Year (Wednesday)

                                                                                                             12th Zanzibar Revolution Day(Sunday)
                                                                                                                                             (mapinduzi ya Zanzibar)

                                                                                                             13th* Maulid Day (Monday)
                                                                                                                   ( sikukuu ya maulidi)


APRIL  ..                     ..                       ..                  ..                    ..    7th Karume Day (Monday)
                                                                                                                     (siku ya karume)

                                                                                                               18thGood Friday (Friday)
                                                                                                                        (ijumaa kuu)

                                                                                                                21stEaster Monday (Monday)
                                                                                                                  (jumatatu ya pasaka)

                                                                                                                26thUnion Day (Saturday)
                                                                                                                   (sikukuu ya muungano)


MAY.         ..               ..               ..               ..                      ..               .1st Workers Day (Thursday)
                                                                                                                     (siku ya wafanyakazi)


July      ..                ..                 ..                ..            ..          ..                 7th Saba Saba Day (Monday)
                                                                                                                      (sikukuu ya sabasaba)  


                                                                                                                                  28/29thEid-el-Fitr (Monday & Tuesday)
                                                                                                                 (sikukuu ya Eid-el-fitr)


AUGUST           ..                      ..                          ..                                     8th Peasant’s Day (Friday)
                                                                                                                        (sikukuu ya wakulima)


October                ..                         ..                          ..             ..                 4th Eid-el-Hajj (Saturday)
                                                                                                                        (sikukuu ya Eid-el-Hajj)

                                                                                                                       14thNyerere’s Day (Tuesday)
                                                                                                                          (siku ya Nyerere)


December     ..                      ..                            ..                   ..                    9th Independence Day (Tuesday)
                                                                                                                        (siku ya uhuru) 

                                                                                                                                               25thChristmas Day (Thursday)
                                                                                                                                                (sikukuu ya krismasi)

                                                                                                                                                26th Boxing Day (Friday)
                                                                                                                                                 (krismasi ya pili zawadi)
                                
                                 CHANZO TOVUTI YA MKOA DAR ES SALAAM
                                                         MASOMO MEMA

Ijumaa, 28 Machi 2014

JINSI TUNAVYOWEZA KUTUMIA MITAALA TZ KUKUZA VIPAJI NA.2

Baada ya kutazama katika hatua ya kwanza ya mada yetu ya jinsi ya kukuza vipaji kupitia mitaala yetu sasa twende hatua ya pili katika mtaala wa elimu ya sekondari.

MAENEO AMBAYO NI UFUNGUO WA KUJIFUNZA (KEY LEARNING AREAS)

Mtaala hapa umefafanua maeneo ambayo mwanafunzi ataelimishwa ili aweze kupanua uelewa wake na hivyo kumfanya kuwa na uwezo wa kuamua kuchagua kuendelea na elimu ya juu na fani atakayo.Na ili kuyafanikisha hayo mtaala umetaja maeneo matano ambayo ndiyo kama ufunguo katika kujifunza nayo ni ;-

A.Lugha (languages)
B. Sayansi asilia (Natural science)
C. Teknologia (Technology )
D. Sayansi ya jamii (social science)
E. Biashara na sanaa za ubunifu (business and aesthetics)

Hapa sasa ndipo panapokwenda kujibu maswali mengi yaliyotapakaa katika jamii.Mtaala umefafanua vizuri sana kwa kuainisha kila somo litakalofundishwa shuleni na eneo linalohusika.
Tuanze na ;-

A.LUGHA;

hapa mwanafunzi atafundishwa lugha ya Kiswahili,Kiingereza,kifaransa,na kiarabu.Kupitia lugha mwanafunzi atajenga uwezo na kuimarisha mbinu za mawasiliano na kumfanya kujiamini na kukidhi mahitaji ya nchi na dunia.

B. SAYANSI ASILIA NA TEKNOLOGIA;( NATURAL SCIENCE)
Hapa mwanafunzi atasoma masomo yafuatayo

1.baiologia (Biology)
2. chemia (Chemistry)
3. Fizikia (Physics)
4. Hisabati ( Mathematics)
5 Mawasiliano na masomo ya kompyuta ( Information and Computer Studies)
6. Elimu ya ufundi ( Technical Education)
7. Kilimo (Agriculture)
8. Uchumi wa nyumbani ( Home Economics)

Kupitia masomo haya mwanafunza atapata msingi bora wa kuanza kushirikiana na mazingira yake kwa kutumia miongozo ya kisayasi na kiteknologia.Mwanafunzi ataanza kuunda bidhaa za kitecnologia kupitia mtaala huu wa elimu ya sekondari.Haya yameainishwa katika sehemu ya mtaala huo.

C. SAYANSI YA JAMII (SOCIAL SCIENCE)

Masomo yafuatayo yanahusika hapa-

1.History
2. Geography
3 Civics

Kupitia masomo haya mwanafunzi atapata nafasi ya kujifunza elimu ya uraia,yaani haki na wajibu wake,ataweza kujitambua na kuendana na jamii,uchumi, siasa, utamaduni na mabadiliko ya kiteknologia yanayochukua nafasi ndani ya jamii na nje ya jamii husika.

D. MASOMO YA BIASHARA (BUSINESS STUDIES)

Hapa mwanafunzi atapata fursa ya kujifunza masomo yafuatayo-

1.Commerce
2.Book-keeping

Katika masomo haya mwanafunzi atapatiwa msingi katika maswala ya usimamizi wa maswala ya fedha (financial Management), kupangilia (planning), masoko ( marketing), Manunuzi (purchasing), mahusiano ya jamii ( public relations) na Ujasiriamali (entrepreneurship).

E. SANAA (AESTHETICS)

Mwanafunzi atasoma masomo yafuatayo-

1. Sanaa za uchoraji,uchongaji na ufinyanzi ( Fine Arts)
2. Sanaa za maonyesho (Theatre Arts)
3. Elimu ya viungo na michezo (Physical Education)
4. Muziki ( Music)

Kupitia masomo haya mwanafunzi ataweza kujifunza mambo ya msingi ya kimaisha ikiwa ni pamoja na ya ujumla na yale ya ujuzi wa kipekee ambayo ni ya muhimu sana katika namna mbalimbali za kimaisha.Hii itawatia moyo wanafunzi kuonyesha vipaji vyao na thamani  yake na kuitambua sanaa pamoja na utayari katika maisha yao.maelezo haya yametoka katika sehemu ya maelezo ya mtaala huo ulio katika lugha ya kiingereza.

Pia kuna masomo ya ziada ambayo mwanafunzi anaweza kuyasoma kufuatana na mzingira fulani kwa kadiri atakavyohitaji.Mfano wale wa shule za sekondari za ufundi wanaweza kusoma somo la ENGINEERING SCIENCE wakati masomo ya EDITIONAL MATHEMATIC, BIBLE KNOWLEDGE na ISLAMIC STUDIES, yanaweza kusomwa na mwanafunzi yeyote kutoka katika shule yeyote ya sekondari.

Kwa ufupi ukiutazama mtaala huo japo una mambo mengi ambayo sijapata nafasi ya kuyasemea lakini kwa sehemu hii tu inaonyesha kujibu maswali mengi yaliyokuwa yakiulizwa na wengi.

Wengi wamekuwa wakisahau kuwa elimu ya msingi na sekondari ni elimu ya awali inayomuandaa mwanafunzi ama kuendelea na elimu ya juu au kujitegemea.Vilevile elimu hii lazima iwe na upana katika mfumo unaokidhi mahitaji ya nchi katika kujitegemea na pia kukidhi mahitaji ya dunia.Mwanafunzi awe na uelewa wa mambo yanavyokwenda na mabadiliko yanayotokea duniani kote sio nchini kwake tu.

CHANGAMOTO ZA MITAALA NA UTATUZI WAKE

Pamoja na kwamba hatujapata nafasi ya kuuchambua mtaala wote lakini kwa ujumla kama utapata nafasi ya kuupitia wote uko vizuri.Kinachojitokeza ni changamoto tu za utekelezaji wa mtaala wenyewe.

Maeneo machache yenye changamoto za utekelezaji wa mtaala kwa sasa viko nje ya shule husika watekelezaji wa mtaala na wakati mwingine hata serikali.

Mfano mtaala unapotaja baadhi ya rasilimari wezeshi zitakazotumika katika kutekeleza mtaala utagundua vingi havitekelezeki kwa sasa mfano;-

TEACHING LOAD AND TEACHER STUDENT RATIO (MZIGO WA KUFUNDISHA NA UWIANO WA MWALIMU NA MWANAFUNZI)

Mtaala umefafanua kuwa mwalimu kwa wastani wa juu kabisa atakuwa na vipindi visivyozidi 30 kwa wiki,vipindi visivyopungua sita (6) kwa siku sawa na masaa manne (4) ya kufundisha.Mtaala unatakiwa ufafanue wazi nini cha kufanya endapo kutatokea upungufu na kufanya malengo ya mwalimu kutotimia.

Mtaala umeeleza kuwa mwalimu anatakiwa afundishe idadi ya wanafunzi 40 katika darasa moja jambo ambalo mpaka sasa halijafanikiwa.Kutokana na upungufu mkubwa wa walimu na majengo. mtaala ulitakiwa kutoa mapendekezo juu ya hatua zinazotekelezeka endapo kutatokea upungufu wa walimu.Kufanya hivyo kutasaidia kupunguza tatizo lolote linalosabishwa na upungufu wa walimu,kuliko kusubiri tathmini za mwisho zitakazoamua nini cha kufanya tukiwa tumeshapoteza sehemu kubwa ya wahitimu.

SCHOOL FACILITIES (VIWEZESHI VYA SHULE)

Mtaala umejieleza kuwa rasilimari wezeshi za shule zita toka moja kwa moja selikarini,selikari za miji,na wamiliki wa shule binafsi.Rasirimali wezeshi hizo ni pamoja na;-
PHYISICAL RESOURCES (rasilimali zinazoonekana)

Pametajwa ujenzi wa madarasa,maabara,maktaba,chumba cha mawasiliano (kitakachokuwa na computer,photocopy mashine,fax,internet connection,printing mashine,scanning mashine)mabweni ,jiko na chumba cha matibabu au dispensery kwa shule za bweni.

A . MADARASA

Mtaala umetoa ufafanuzi kuwa chumba cha darasa kinatakiwa kiwe na ubao wa kuandikia , vifaa vya kukalia na kuandikia vilivyotimia.Hili bado ni changamoto na mtaala ungepaswa kutamka wazi kuwa endapo vifaa hivi havitapatikana ni njia gani mbadala inaweza kutumika, kunusuru matokeo yeyote yanayosababishwa na watoto kutokuwa na vifaa vya kukalia na kuandikia.Ninapendekeza kuwa kuanzishwe kodi maalumu kwa watu wote wanaosomesha watoto wao kwenye shule za gharama na nje ya nchi.kodi hii itumike kufidia upungufu utakaojitokeza katika viwezeshi hivyo.Pia wazazi wenye kipato cha kati walazimike kupeleka vifaa hivyo ili vilivyopo vitumike kwa wasiojiweza.Na ukizingatia zoezi hili sio la kila siku basi baada ya muda mfupi tutakuwa tumemaliza tatizo.

B.MAABARA

Maabara imeelezwa kuwa iwe imekamilika ikiwa na vifaa vyote muhimu kwa majaribio ya kisayansi.Maabara hizi hazipatikani kwenye shule nyingi na badala yake napendekeza kuwa maabara za shule jirani zitumike kusaidia wanafunzi wa shule zisizokuwa na maabara.Kuhusu gharama za usafiri kama ni mbali wazazi watachangia kama wanavyochangia kwanye mavazi nk.Hata hivyo shule zinaweza kuwa na miradi ya kujitegemea itakayochangia gharama za usafiri.

C.MAKTABA

Zimetajwa kuwepo kila shule zikiwa na vitabu vyote vya kiada na ziada.mpaka sasa shule nyingi hazina maktaba.Wananchi wahamasishwe kuzijenga kama walivyojenga shule na watu binafsi wapewe fursa ya kuwekeza kama miradi ya kimaendeleo.wanaweza kuwekeza kwa mtindo wa hisa kama mradi wa kijiji au kikundi cha uwekezaji.Watawekeza vitabu kwa kuwalipisha wanafunzi wa shule zinazowazunguka kiasi kidogo cha fedha ikiwa kwa mwaka au hata kwa siku na fedha hiyo itawawezesha kujikwamua kiuchumi.

D. MABWENI NA NYUMBA ZA KULALA WALIMU.

Hayo yametajwa na mitaala kuwa ni muhimu katika shule za bweni.changamoto iliyopo shule hizi ni chache na zilizopo haziko kwenye viwango .Ninapendekeza kuwa wanafunzi wachaguliwe kulingana na mahala wanakotoka.Na utaratibu wa kupata huduma nyingine ambazo hazipo utumike utaratibu ambao nimependekeza awali.

E.KUMBI

Imependekezwa kuwa kuwepo na kumbi zitakazokuwa zikitumika kwa shughuli mchanganyiko .Kwa shule ambazo hazina kumbi napendekeza kuwa zitumie madarasa kwa dharula.


Pia imeelezwa kuwa kumbi hizo zitatumika katika baadhi ya michezo ya ndani.Napendeleza kuwa kuwepo na darasa moja maalumu liyakalokuwa likitumika katika shughuli za michezo ya namna hii ili kukidhi hitaji la wahusika kabla ya kuwa na ukumbi rasmi.

F.VIFAA VYA MAWASILIANO (ICT FACILITIES)

Vifaa kama computer , mashine za fotokopi,scanner,internet,nk navyo vimezingatiwa katika mtaala.Ninachopendekeza vifaa hivi view ni lazima kwa kila shule kutokana na umuhimu wake. Kwa mujibu wa unyeti wa shwala husika ninapendekeza kuwepo na wazabuni watakaokuwa na mkataba na wizara ya elimu kwaajili ya kutoa huduma hii endapo shule itakuwa haina vifaa hivi.

Kitendo cha kuendelea kusubiri pasi na kuchukua hatua ya kupeleka vifaa hivi mashuleni tutaendelea kubaki nyuma kimaendeleo kwa kuwa majirani zetu watatumia mwanya wa ujinga na ushamba wetu kujinufaisha.

Kutumia vifaa hivi vya kisasa kujifunzia na kufundishia ndiyo njia rahisi zaidi ya kijipatia elimu na kuongeza uelewa.Kwa wale wenye uwezo mtaala ueleze wazi kuwa wataruhusiwa kutumia vifaa hivi sawa na kama ambavyo wazazi walivyoruhusiwa kuwanunulia vitabu watoto wao.kufanya hivyo kutajenga mazoea ya matumizi ya vifaa hivi kwa watoto na kuwafanya waongeze uwezo wao wa kuelewa.

Mtaala pia umetaja maswala kadhaa ambayo yanatekelezeka kama maeneo ya kupumzikia,michezo,vyoo kwa wenye mahitaji maalumu, vifaa maalumu kwaajili watoto wenye mahitaji maalumu nk.Kifupi ni kwamba hayo yote yanatekelezeka.mfano;-

A. Maeneo ya mapumziko na michezo

Kwa maeneo ya kupumzikia napendekeza sio lazima yawe majengo bali inaweza kupandwa miti maalumu yenye kivuli cha kutosha na kutumika kwa mapumziko.Katika michezo ninaimani kuwa shule nyingi zinamaeneo ya wazi ambayo yanaweza kutumika kwaajili ya michezo kwa utaratibu maalumu utakaopangwa na shule.

B. Vifaa maalumu kwa wenye mahitaji maalumu .

kwanza watu wenye mahitaji maalumu huwa ni wachache.Hivyo mitaala ieleze wazi kuwa kama serikari haitawapa vifaa maalumu vitatoka wapi kutokana na ulazima wake.

C. Vyoo kwa wenye mahitaji maalumu.

Napendekeza tubadilishe miundombinu ya baadhi ya vile vilivyopo kutatua tatizo la uhitaji wa watu wenye mahitaji maalumu.

Ninaimani kunamambo mengi katika mtaala wa elimu ya sekondari ambayo ni changamoto. lakini tukitumia nia ya dhati ya kuendeleza vipaji vya watoto wetu, tunaweza kutumia changamoto hizo kama daraja na kutafuta mbinu mbadala katika kutekeleza mtaala wetu.
Mfano katika changamoto ya muda wa kujifunza mtaala umeeleza kuwa mwanafunzi atajifunza kwa siku 194 kwa mwaka.kutakuwa na vipindi 40 kwa wiki sawa na vipindi 8 kwa siku.Masaa matano (5) ya kujifunza kilasiku.

 Kwa hesabu za haraka muda huu ni mchache sana kujifunza .Vivyohivyo bado kunasiku dharula zinazofanya wanafunzi wasitumie muda wao vizuri kujifunza.Dharura hizo ni pamoja na upungufu wa walimu,sikukuu za kitaifa,Maradhi kwa walimu na majanga.Ninapendekeza siku ya jumamosi itambuliwe na mitaala na kuongeza siku za kujifunza walau kufikia siku 236.

Sio rahisi kutaja changamoto zote ila tuzitambue kwa faida ya kuboresha mtaala wetu.Ninaimani kuwa tukitumia mtaala kwa kuzingatia rasirimali tulizonazo tunaweza kuendeleza vipaji vya watoto wetu na kuwafanya wawe na mchango katika jamii yetu

JINSI TUNAVYOWEZA KUTUMIA MITAALA TZ KUKUZA VIPAJI NA.1

kwa kuanzia nitauzungumzia mtaala wa elimu ya secondari.Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu mitaala ya Tanzania kwamba haikidhi matarajio ya mwanafunzi kwa maisha yake baada ya kutoka shule.
Mfano;-

1.watu wengi wamekuwa wakilalamikia kuwa mitaala iliyopo haimuandai mototo kuishi maisha ya kujitegemea baada ya kumaliza masomo yake.Wangependa mwanafunzi akimaliza sekondari awe mjasiriamali,mkulima nk.

2. Malalamiko mengine ni kuwa watoto wamekuwa wakisoma masomo mengi kupita kiasi ,Kitu kinachomfanya mwanafunzi kuwa na mzigo mkubwa wa mambo ya kujifunza.Wangependa kuona wanafunzi wanasoma masomo machache tu ili wayamudu.

3. Pia wamekuwepo watu wanaodai kuwa mambo ambayo wanafunzi Tanzania wanajifunza hayahusiani na maisha tunayoishi.Yaani wanajifunza mambo ambayo hatuyahitaji katika maisha yetu.

4. Wapo wanaodai kuwa eti elimu inayotolewa Tanzania bado ni ya kikoloni na siyo ya kiuzalishaji kama inavyokusudiwa.
5.Wapo wanaodai kuwa elimu ya ujasiriamali haijapewa kipaumbele katika elimu ya Tanzania.

6.Maswala ya kijamii nayo yamelalamikiwa kuwa eti hayajawekewa mkazo katika elimu ya tazania.Inamaanisha kuwa eti inawafanya watu wasiwe wanajua haki zao, wasiwe wawajibikaji,waadilifu,nk.

7.Michezo vivyohivyo imelalamikiwa kuwa haijatiliwa mkazo katika elimu ya Tanzania.Kwamba watoto hawajafundishwa michezo kama somo rasmi nk.

8.Hata maswala ya kilimo yamezungumzwa kutozingatiwa katika elimu ya Tanzania.Baadhi ya malalamiko yanadai kuwa wahitimu wengi hawapendi kufanya kilimo kwakuwa hawakufundishwa kilimo mashuleni.

Nitakubaliana na malalamiko hayo kwa sehemu ndogo sana .Lakini cha kushangaza ni kwamba malalamiko mengi yanatokana na kutoifahamu mitaala yenyewe.Cha ajabu zaidi ni kwamba hata watu wenye elimu wamekuwa wakiilalamikia mitaala kwamba ndiyo kikwazo cha maendeleo ya Tanzania.Kifupi ni kwamba malalamiko mengi sio ya kweli na hayatujengi,hivyo yanatunyima fursa ya kutumia mitaala iliyopo kikamilifu ili kuleta tija kwa taifa letu.

Kwa kuupitia mtaala wenyewe kwa ufupi ninaimani sote kama wadau muhimu wa elimu yetu Tanzania, tutagundua mambo mazuri na hatimaye kuyatumia kama mtaji, katika kuibua na kuboresha vipaji vya wanafunzi wetu.

(I) MAANA YA MTAALA
Wataalamu wa masuala haya wanadai kuwa mtaala una maana nyingi sana kutokana na dhana tofautitofauti . Taarifa ya TAASISI YA ELIMU YA MWAKA 2013 MARCH ya maboresho ya mitaala tangu mwaka 1961 hadi 2010,inadai kwamba dhana ya mtaala, ikijumuisha nadharia zake na muundo wake (models) ni eneo la taaluma lenye mitazamo (perspectives) tofauti.

Lakini taarifa ya taasisi hiyohiyo na mwaka 2005 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2013 ya mtaala wa elimu ya secondary iliyoandikwa kwa lugha ya kiingereza katika utangulizi wake inasema ( Curriculum is generally prescribed as a set of standards that guides the delivery of education by considering the following areas:) mtaala ni viwango vilivyopangwa au kuwekwa na serikari ili kuongoza utoaji wa elimu kwa kuzingatia maeneo yafuatayo;-

Maeneo hayo ndiyo yale yanayotajwa na taarifa ya mabadiliko ya mitaala tangu mwaka 1961-2010, iliyotolewa mwezi march 2013 nayo ni –

(i) Ujuzi watakaoujenga wanafunzi (competences) yaani maarifa (knowledge), stadi (skills) na mwelekeo (attitudes),
(ii) Njia za kufundishia na kujifunzia zitakazotumika katika utekelezaji wa mtaala (pedagogical orientations),
(iii) Vifaa vya kufundishia na kujifunzia vinavyohitajika,
(iv) Upimaji, ufuatiliaji na tathmini ya mtaala husika.
(v) Sifa za kitaaluma na kitaalamu za mwalimu atakayeuwezesha mtaala husika,
(vi) Miundombinu wezeshi (enabling infrastructure) kwa utekelezaji wa mtaala wenye ufanisi,
(vii) Muda utakaotumika katika ufundishaji/utekelezaji mtaala

Ili kupata uelewa mzuri kuhusu mtaala hatuna budi kugusia pia na sera ya elimu ambayo ndiyo inayozaa mtaala.

TAMKO LA SERA YA ELIMU
Mtaala wa elimu ya sekondari nchini unatokana na kitu kinachoitwa TAMKO LA SERA YA ELIMU (EDUCATIONAL POLICY STATEMENT)

Ikumbukwe kuwa kwa mujibu wa tamko la sera ya elimu ni kwamba utoaji wa elimu katika nchi ni lazima uendane na matakwa au mahitaji ya nchi husika,na vilevile mahitaji au matakwa ya dunia.Mtaala umezingatia pia mazingira ya kijamii na ya kiuchumi bila kuacha upande wa pili yaani yatakayoendana na hali kama hizo kidunia.

Chukulia kuwa kama kila nchi ingeamua kufundisha watoto wa nchi husika kwa kuzingatia mahitaji ya nchi yao tu, leo dunia ingekuwa na hali gani,kiuchumi,kijamii,kisiasa,kidiplomasia ,nk ?.Lakini kwa kuzingatia matakwa ya dunia ya leo mtaalamu yeyote anaweza kuwa msaada au kufanya kazi popote kutokana na maandalizi aliyoyapata akiwa shuleni.

Swala hili linatupa ushahidi tosha kabisa kuwa kuna umuhimu wa kutazama na upande wa pili katika maswala haya ya elimu.Tusije tukatengeneza kizazi kitakachoshindwa kuendana na dunia kwa kukosa maarifa na ujuzi utakaokifanya kiwe nyuma au kutofiti kabisa katika dunia yaleo.Haya yote yanawezekana tu pale tutakapoachana na fikra za kuzalisha wachuuzi wa kwenda china na dubai kwaajili ya maisha ya tumbo na mavazi.

Matamanio ya watu wengi ni kuzalisha wachuuzi tu na sio wataalamu.Kama unandoto za kuzalisha wachuuzi basi mtaala huu hautakufaa kabisa kwa kuwa umelenga kuzalisha wataalamu .Mwanafunzi wa sekondari lazima ajengwe katika msingi imara wa nadharia ya mambo mengi ili achague machache atakayoyafanyia kazi mbele ya safari katika maisha yake.

Ni lazima mwanafunzi atengenezwe ili kujisaidia yeye mwenyewe ,jamii inayomzunguka na kuwa na mchango katika dunia.Kumbuka kufeli na kubaki nyumbani ni bahati mbaya tu.
Kama utausoma vizuri mtaala wa sekondari utagundua unaandaliwa kwa lengo la kumfanya mwanafunzi kuwa tayari kuendelea na masomo ya juu, na endapo hataendelea basi atatumia ujuzi huo mdogo kujikimu yeye mwenyewe kufuatana na juhudi alizonazo.

Tukumbuke kuwa kama tutaamua kuwavuna na kuwatumia kwa matumizi yetu basi bado watahitaji ujuzi wa ziada ili waweze kufaa kwa shughuli za kijamii.Mifano mizuri tumeiona kwa JESHI LA POLISI,JESHI LA WANANCHI, NA JESHI LA KUJENGA TAIFA,NA BAADHI YA VIWANDA NA TAASISI.Hawa huwachukuwa vijana hawa na kuwapa mafunzo maalumu na kuwatumia kwa kazi mbalimbali na ufanisi wake sote tumeushuhudia.Asilimia kubwa ya wazalishaji wa nchi hii ni vijana waliotoka katika kundi hili.

Sasa ili kujiridhisha kuwa mtaala unazingatia mambo yote muhimu tunayoyakusudia tutazame muhutasari wa malengo ya mtaala kwa ujumla wake kabla ya kuzama ndani zaidi .
MALENGO YA MTAALA WA ELIMU YA SEKONDARI TANZANIA
Mambo haya yameainishwa katika mtaala wa elimu kama ulivyoboreshwa mwaka 2013 nayo ni ;-

1.Kuimarisha na kupanua mtazamo wa mawazo ya msingi ,maarifa , ujuzi, na kanuni zilizopatikana na kuendelezwa shule za msingi.

2.Kuboresha maendeleo zaidi na kutambua umoja wa kitaifa,utambulisho,maadili,uwezo binafsi,kuheshimu na utayari wa kufanya kazi,kutambua haki za binadamu,utamaduni,utashi ,desturi,mila, majukumu ya kiraia na wajibu.

3.Kuinua maendeleo ya uwezo katika lugha na matumizi ya ufanisi ya ujuzi wa mawasiliano katika lugha ya Kiswahili na angalau moja ya lugha ya kigeni.
4.Kutoa fursa kwa mahitaji ya maarifa, ujuzi , jitihada, na uelewa katika eneo la kujifunza lilichaguliwa.

5.kumuandaa mwanafunzi kwa elimu ya ngazi ya tatu na ya juu,ya ufundi, ufundi sanifu,na mafunzo ya kitaalamu.

6.Kuamsha hisia na uwezo wa usomaji binafsi,kujiamini na kujiendeleza katika waanzilishi wapya wa sayansi na teknolojia,taaluma,ujuzi wa kikazi,na mbinu

7.Kuwaandaa wanafunzi kuingia katika dunia ya kiutendaji.

Nimelazimika kunukuu mambo hayo ya msingi kutoka katika mtaala wa elimu ya sekondari ulioboreshwa mwaka 2013 kwasababu kwa sehemu kubwa yanajibu maswali mengi ambayo yamekuwa yakiulizwa na wengi.

Utaona tofauti kubwa sana na tulikotoka mfano mwaka 1967 malengo makuu ya mtaala yalikuwa ni;-

1. Kuwafunza watoto wajione kuwa sehemu ya jamii wanazoishi.

2. Elimu kupanda mbegu ya watu kuishi pamoja na kufanya kazi pamoja.

3. Elimu iwafanye watoto kujiona wote ni sawa kibinadamu na kuondoa majivuno ya kikabila, rangi, dini na elimu.

4. Kujenga stadi za kudadisi na kujenga moyo wa kujiamini.

5. Kuandaa watoto kwa kazi za maisha ya vijijini na wanaojitegemea.

Kwa vyovyote vile pamoja na matokeo mazuri ya mitaala ya wakati huo, ambayo shabaha yake kuu ilikuwa ni kumuandaa mototo kutumia zaidi rasirimali zilizomo ndani ya eneo lake  tuu kwaajili ya kujikwamua kiuchumi,Lakini sasa mtaala unatakiwa kumuandaa mwanafunzi kutumia rasirimali zilizomo katika dunia kwaajili ya kujikwamua kiuchumi.

Alhamisi, 27 Machi 2014

JINSI YA KUTAMBUA KIPAJI CHAKO



kama kuna swali ambalo linahusu maisha binafsi ya mtu na limekuwa na majibu hafifu sana ni swali       linalohusu kipaji.Kuna idadi kubwa sana ya watu wanaomaliza maisha yao hapa duniani bila kufahamu ni aina gani ya kipaji walichonacho.

Wengine hata hawaamini kuwa wanaweza kuwa na kipaji.Kwa sababu hiyo wamefikiri kuwa kipaji ni kwa baadhi ya watu tu na swala hili haliwahusu hata kidogo.Fikra hizo sio za kweli  hata kidogo na ningependa nikueleze wazi kuwa hata wewe unakipaji cha pekee sana.Nasisitiza tena kuwa hata wewe una kipaji Ila hujakitambua na hujakitumia.Kupitia  hii ndiyo itakuwa nafasi yako ya kuanza kufaidi matunda ya kipaji chako.


Acha kujivunya moyo kuwa umri wako umepita na huhitaji tena kusikia habari ya kipaji au habari ya kipaji ni kwaajili ya watoto wadogo tuu.Kitabu hiki kitakupa mwongozo wa kubadili mwelekeo wako katika kutumia kipaji chako bila kuathili maisha yako.

MAANA YA KIPAJI
N
eno kipaji sio neno geni kwetu hasa sisi tuliozaliwa katika miaka ya hivi karibuni.Limezoeleka sana kutokana na kuzungumzwa sana katika maeneo mbalimbali siku hizi .Chakusikitisha ni kuwa, Jinsi kipaji kinavyotamkwa ni tofauti kabisa na kinavyotumika.Kwa usemi mwingine naweza kusema kuwa kipaji kinatamkwa sana kuliko kinavyotumika.Swala hili linafanya maana ya kipaji kupotea na hivyo jamii kuishi bila kutumia nyenzo hii muhimu ya asili. IF YOU RECOGNIZE YOUR TALLENTS, USE THEM APPROPRIETLY, AND CHOOSE A FIELD THAT USES THOSE TALLENTS ,YOU WILL RISE TO THE TOP OF YOUR FIELD (Kama ukitambua vipaji vyako, vitumie kwa usahii na uchague eneo linalotumia vipaji hivyo, utainuka juu kabisa ya eneo lako).Hii ni kwa mujibu wa nukuu kutoka kwa  Ben Carson  kama alivyoandika katika kitabu chake cha think big.

Bila kujali ni kipaji cha aina gani. kipaji ni uwezo au nguvu za asili anazokuwa nazo binadamu katika kutenda jambo Fulani kipekee bila kujali kiwango cha ujuzi alionao.Uwezo huu unaweza kujitokeza katika kufikiri ,kutamka, kutenda, kuhisi nk.

kipaji si ile shughuli tuifanyayo bali ni ule uwezo wa asili tunaozaliwa nao na kujijenga ndani yetu kuwezesha kufanya aina flani ya shughuli au kitendo kwa namna ya upekee sana kuliko watu wengine.Uwezo huu huwa ndiyo mfumo asilia ndani ya vinasaba vya mtu ambao hauwezi kubadilishwa kwa kuzoelea kufanya mambo flani flani yasiyoendana nao.


kwa mimi ninayeamini uwepo wa mungu nasema hii ni zawadi ya pekee kwa kila binadamu kutoka kwa Mungu na kila mtu amejaliwa kwa namna yake ili sote tufaidiane.

DALILI ZA KUANZA KUONEKANA KWA KIPAJI

Mara nyingi vipaji vingi ambavyo ndiyo uwezo uliomo ndani yetu kuwezesha kufanya mambo kadhaa kiupekee,  huanza kugundulika wakati muda umeshapita sana.Sababu kubwa ya kutogundulika haraka kwa vipaji hivi (uwezo), ni kutokana na kipaji kujitokeza kwa namna ya mficho.Hujitokeza kwa mfano wa faili lililofungwa na kuandikwa kwa nje  uwezo wa michezo ,taaluma,ubunifu,au uimbaji bila kufafanua ni uwezo wa mchezo upi hasa au taaluma ipi au ubunifu wa nini au uimbaji wa aina gani. lakini kwa bahati mbaya ufafanuzi huo ni mpaka ufungue ndani.Kwasababu hiyo hata wengi wa wanavipaji huishia kutumikia anwani za mafaili hayo mpaka wanakufa. Wanatumikia michezo wasijue uwezo wao ni juu ya mchezo gani hasa, wengine taaluma wasijue ni taaluma gani na wengine uimbaji wasijue uimbaji wa aina gani.

Kitu ninachoomba ukitambue ni kwamba kipaji huanza kwa namna ya wazo.Wazo hili huwa halisomeki sawasawa kama ilivyo kwa faili lisilo na ufafanuzi . Nalo hukuwa taratibu kwa kadiri mtu huyu anavyochukua hatua au kulifanyia kazi. Kwa maana nyingine ningesema kulifanyia mazoezi.Mfano; kama wazo likiwa ni uwezo wa kitaaluma basi haliwezi kujitokeza na kujiweka wazi mpaka utakapochukua hatua ya kusomea au kufanya kazi katika taaluma hizo ambazo ule uwezo wako wa asili (kipaji) unajipambanua.

Kupitia shuleni huwa ni rahisi kiasi kwasababu watoto hupewa uwanja mpana kidogo wa kujaribu kuonyesha japo vipaji vichache, haswa vya kitaaluma chini ya uangalizi flani. Lakini cha kusikitisha ni kwamba hata mashuleni bado  nafasi hiyo ni finyu sana kuonyesha na kukuza vipaji vyote vilivyopo duniani.Vinavyokosa nafasi hiyo ni vile ambavyo viko nje ya mitaala kutokana na kutovitilia maanani hivyo kutengwa na mfumo wa elimu.

Katika maeneo maalumu ya kukuzia vipaji imekua rahisi kuvigundua.Kwasababu watoto au wanafunzi hupewa nafasi ya kuonyesha wanachokiweza na kisha kuwaweka katika makundi maalumu.Ni wajibu wetu kuendelea kuanzisha vituo hivi na kuwatia moyo wanaofanya hivyo. Lakini tufikirie kuanzisha vituo vitakavyoshughulika na aina nyingi za vipaji na sio aina moja tu ya kipaji kama ilivyo sasa. Kwa kuwa  vituo vingi vinaendeleza vipaji vinavyoendana na michezo.

NANI ANA KIPAJI
Ukweli ni kwamba kila mtu ana kipaji cha peke yake  ambacho kinamtambulisha yeye na kumfanya awe na mchango wa tofauti na mtu mwingine yeyote duniani.Kosa kubwa tunalolifanya ni kwamba wengi tunaishi kwa kufuata na kuigiza vipaji vya watu wengine.Inawezekana ikawa ni wewe na pengine umefanya hivyo bila kufahamu.

kwa maana nyingine ni kwamba watu wengi wanaishi kwa kutumia uwezo ambao haumo ndani yao.Wanafanya shughuli ambazo haziendani na mfumo halisi uliojengwa  ndani yao.Wanaenda kinyume kabisa na namna mfumo wa  ubongo wao,ufahamu wao,na miili yao ilivyosukwa

AINA ZA VIPAJI
Kama laiti tungeambiwa tutaje aina zote za vipaji basi ilibidi tuitishe jopo la watu watakaofanya kazi ya kuorodhesha vipaji.Ingebidi kurasa kwa kurasa zitumike ndipo tufanikiwe kutaja vipaji vyote.Hata hivyo kuna vipaji vingine ambavyo bado havijatokea navyo vimekosa fursa hiyo. Kwasababu ya kwamba wenyenavyo hawajazaliwa au mazingira hayajaruhusu vianze kufanya kazi.

Kama utakuwa makini sana utagundua kuwa kila aina ya kipaji ni cha pekee sana Hata kama wanavipaji unaowatazama watakuwa na kipaji cha aina moja. Chukulia umepewa zoezi la kuwatofautisha waandishi wa vitabu kumi kupitia vitabu vyao.Kwa namna ya ajabu sana hata kama wote watakuwa na kipaji cha uandishi wa vitabu. Hakuna siku watajikuta wote wameandika kitu kinachofanana kwa 100%, hata kama wazo litakuwa moja.Watatofautiana katika matumizi ya vitenzi ,hadithi,misemo,falsafa,nk, na kwasababu hiyo kila mmoja ataoneka ni wa tofauti na mwenzake .

Vipaji hivi Kwa mtazamo wangu nimevigawanya katika makundi kadhaa ili kurahisisha kupata uelewa wa jumla maana sio rahisi kuvitaja vyote.

Vipaji vya taaluma zote za sayansi asilia ,teknolojia na sayansi  ya kijamii.
Hapa pana vipaji vinavyomuwezesha mtu kufanya shughuli mbali mbali za kisayansi ikiwa ni ile asilia au ya kijamii. Kuna shughuli nyingi sana zinazoingia moja kwa moja katika kundi hili kwa kutaja baadhi ni:-
Hisabati,fizikia,kemia,biologia,jiografia,historia,lugha,uhandisi na ufundi wa aina zote.Pia utengenezaji wa program za kompyuta,kutumia vifaa vya kielekroniki kama kompyuta nk,ubaharia,uandishi wa vitabu na habari,uhariri wa vitau na habari,uchumi,takwimu,kilimo,uvuvi,ufugaji,uwindaji, sayansi ya tiba,uuguzi, sayansi ya anga,shughuli za maabara,sayansi ya viumbe aina zote ikiwamo vile vya bahari,mwitu na majumbani.Hata hivyo kuna uongozaji wa ndege,meli,udereva,uendeshaji pikipiki na baiskeli,

Vingine ni ualimu,utawala,uongozi,diplomasia,siasa,sheria,saikolojia,filosofia, uhubiri wa dini,ushauri nasaha,ulezi wa yatima,utunzaji mazingira,utunzaji kumbukumbu,ukutubi(maktaba)

Sio hizo tuu bali kuna shughuli nyingine za kisanii (sanaa) kama filamu,maigizo,muziki na uimbaji,ngoma za asili,usimulizi,utunzi wa hadith,uandishi wa filamu,uchekeshaji,uchoraji wa katuni na utengenezaji wa katuni za video,uhunzi,ufinyanzi,ususi,uchoraji,uchongaji,utarizi,

 Vipaji vya michezo
Hivi ndivyo vipaji vinavyomwezesha mtu kufanya shughuli za michezo mbalimbali kama ,
Mpira wa miguu,kikapu,pete,wavu,kudansi,sarakasi,mbio,kuruka kamba,ndondi,karate,bao,karata,gemu za video nk.
 vipaji vya kibiashara
Hivi ni vipaji vyote vinavyomwezesha mtu kufanya kazi zote zinazohusiana na biashara.Vipaji hivi humuwezesha mtu kufanya shughuli kama, Ujasiriamali,biashara,uwekezaji,uchuuzi,uandishi wa mchanganuo wa biashara,utunzaji wa fedha nk.
 Vipaji vya kimaumbile na hisia



Vipaji hivi Ndiyo lulu ya binadamu kwa kuwa vinatenda kazi ndani ya binadamu kuliko vinavyoonekana kwa nje.Nimeshindwa kuvipatia jina muafaka hivyo nimevipa jina la vipaji vya kimaumbile na hisia.Hapo nina maana kuwa tunavitambua zaidi kupitia maumbile na hisia za mtu husika kuliko zile shughuli anazozifanya. Licha ya kujitegemea vyenyewe mara nyingi husaidia hata vipaji vingine kufanya kazi sawasawa.

JINSI YA KUTAMBUA KIPAJI CHAKO
Niliwahi kuizungumzia mada hii ndani ya kipengele cha jinsi ya kutambua kipaji chako, katika mada inayosema nifanye nini kabla ya kujiendeleza kielimu?
 Lakini hapa nitakizungumzia kipengele hiki kwa engo tofauti kidogo ili kupanua uelewa zaidi.

Kama nilivyoeleza katika kipengele kimojawapo kilichopita kwamba kipaji hata na vitu vingine ndani yetu hujengwa vikianzia na wazo.Huu ndiyo mfumo rasmi wa maumbile ya binadamu. kwamba kilakitu ndani yetu hujiumba kupitia namna ya mawazo yasiyo wazi sana katika ufahamu wetu.Nayo hukuwa taratibu na hatimaye huwa dhahiri hata tukashiriki kikamilifu katika kuyaendeleza.

  Mtu mwenye kipaji kisichoendelezwa kwa kupewa au kujipa fursa ya kukifanyia kazi hana uwezo wa kukitambua.Hali hii ndiyo iko kwa watu wengi duniani.Ya kuwa wanavipaji ambavyo havikuwahi kupewa fursa ya kufanya kazi ili vijidhihirishe .Namna hii huwafanya kukosa hamasa ya kufanya zaidi na hivyo kilakitu kwao huwa kigumu au hakiwezekani.
Niwe muwazi kwa kusema kuwa kipaji sio ndoto kama tulivyozoea kufikiri.Bali ndoto inatakiwa ije baada ya kutambua kipaji.Mara nyingi tumezoea kuwauliza watoto wadogo watueleze ndoto zao na kuchukulia kuwa hivyo ndiyo vipaji vyao.Hapo tunakuwa hatuko sahihi hata kidogo.Mtu yeyote anaweza kuwa na ndoto ya kitu chochote au ya kuwa mtu yeyote lakini si kipaji.Nina maana kipaji hakiwezi kuja kwa kukitamani tuu.kwasababu ni kitu ambacho kipo ndani yetu tangu tunazaliwa kila mmoja kwa namna yake.Sio ajabu mtoto akatamani kuwa komandoo na akawa na ndoto ya kuwa komandoo kwasababu tu siku moja aliangalia filamu ya John comando na akaifurahia.

Kipaji hujijenga chenyewe ndani ya binadamu bila kukijengea picha yeyote.Ni uwezo wa kiasili wa kuzaliwa nao na sio wa kuhamasishwa.Hautokani na mambo yaliyokwisha kuwapo bali ni uwezo wa kipekee sana anaokuwa nao binadamu aidha katika kutenda,kuhisi,kufikiri au kusema.Kila mtu anatofautiana na mwenzake kwa uwazi kabisa hata kama wako katika kundi la kipaji cha aina moja.
Unaweza kukitambua kipaji chako kwa kuzingatia yafuatayo:-

v Wazazi au walimu wako wameshawahi kugundua uwezo wako wa jumla katika kipaji cha jumla mafano taaluma,michezo,kuzungumza,nk? Ulishawahi kujulishwa au kupata tetesi?mpaka sasa kipaji hicho kimesha jitokeza na kukufanya uwe na mahala pamoja unapofanya vizuri zaidi ? kama ndiyo tumia fursa hiyo kipaji kitatokeza.

v  Angalia mazingira ya unachofanya kama yalitokana na uwezo wako wa asili au ulijiingiza kwa kuhamasishwa na mtu,shida, au tamaa ya kutajirika haraka.Tafuta kile kinachotokana na uwezo wako wa asili ili kipaji chako kiweze kufanya kazi.

v  Angalia kama kuna ulichokuwa ukikifanya hapo zamani ambacho hata kama hukukifanya kwa ufanisi kwa kukosa maarifa lakini kilikupa upekee .Lakini kiwe kilitokana na uwezo wako wa asili na ulifanya mara kwa mara.Kiendeleze na baada ya muda kitakupa mwelekeo wa wapi uende na hivyo kufanya uwe tofauti na wengine.

v  Angalia kama unavyovifanya sasa hata bila kutumia maarifa mengi kimojawapo unakifanya kwa ufanisi mkubwa kuliko vingine vyote na kwa upekee.Hicho unachokifanya vyema zaidi ndicho kipaji chako usikidharau ukikikuza kila mtu atakiheshimu.Hata huheshimika kwa nyumba ni baada ya kumalizika ujenzi, katika msingi mtu yeyote anaweza hata akajisaidia haja ndogo.

v  Angalia katika unavyovifanya au ulivyovifanya ni kipi kilikutambulisha au kinakutambulisha na kukufanya ukubalike kipekee na sio kutokana na kiwango chako cha kisomo.Kipaji halisi hakitegemei kiwango cha kisomo, bali uwezo wa asili ndio hutawala katika kutenda jambo.Katika kiwango chochote cha elimu bado uwezo wa asili utachukua nafasi na kutawala katika utendaji na kukufanya wewe ndiyo upate sifa na sio elimu yako.

v  Jiulize kama umeshawahi kuambiwa unakipaji? Je ni kipaji gani? Umeshawahi kuambiwa mahala kwingine na hapo maneno kama hayo? Hicho ndicho unachokifanya mara kwa mara kwa ufanisi kuliko vingine?.

v  Angalia kama unachofanya unahisia nacho au unafanya kwasababu hauna kazi nyingine? Na hisia zako za ndani zinasemaje? Jali zaidi hisia zako za ndani sana zinazo husiana na uwezo wako bila kujali vitisho kwa sababu kipaji kinanguvu kuliko kitisho chochote kilichoko mbele yako.

v Orodhesha kwa umakini mkubwa mambo yote unayojikuta ukiyafanya bila hata kushurutishwa hata kama ni madogo.Tenga yale unayoyafanya kutokana na hisia mfano huruma, upendo,kuvumilia mateso ya mwili nk.Kisha yale yatokanayo na umbo lako mfano usafi,urembo nk.Utafanya hivyohivyo kwa yale unayoyafanya kwa kuzungumza,kufikiri au kivitendo.Hapo ninamaanisha  mambo kama kuandika,kuchora,kucheza,kuzungumza katika halaiki,kuhubiri dini,kubuni vitu mbalimbali,kusimamia biashara,ususi  nk.Kipe maksi kila kimoja kulingana na mara nyingi unavyokifanya.

Jiridhishe kuwa unachokipa maksi nyingi ndicho ambacho umekuwa ukikifanya mara nyingi zaidi.Kisha kichague kile ambacho umekuwa ukikifanya kipekee zaidi na kuanza kukiendeleza. Hicho ndicho kinatokana na kipaji chako.

Kama wewe hujawahi kuhisi au kusikia chochote kuhusu kipaji chako basi ni kwasababu ya kukosa nafasi ya kukionyesha.Fanya kila unachohisi kinatokana na uwezo wako wa asili hata kama kimewahi kufanywa na mtu mwingine.Pima matokeo ya mara kwa mara kwa jinsi unavyoridhishwa wewe mwenyewe,wanao kuzunguka,wanaokuongoza nk.Ni dhahiri kuwa kipaji chako ndicho kitakachokutambulisha zaidi kuliko kitu chochote.Mpaka hapo utakifahamu kipaji chako.