Ijumaa, 8 Agosti 2014

HIZI NDIZO FAIDA ZA USOMAJI WA VITABU NA MAANDISHI MENGINE


Katika mada ya JINSI YA KUSOMA KWA KUELEWA NA KUFAULU nimeeleza kwa upana kuhusu usomaji unavyoweza kubadilisha fikra zako kwa kukupatia mawazo mapya (bofya mada hiyo kusoma).Ni dhahili kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayesoma mara kwa mara vitabu na maandishi mengineyo na Yule asiyesoma kabisa.Tofauti yenyewe utaipata pale wanapo zungumza,tenda au kuamua jambo fulani.Bila shaka kila mmoja atatenda,kuzungumza au kuamua kulingana na uwingi wa taarifa alizonazo katika fikra zake na hasa hasa kama taarifa alizonazo ni sahihi.

LENGO KUU LA KOSOMA VITABU NA MAANDISHI MENGINE

Kifupi naweza kusema ni kujipatia mawazo mapya hivyo kujiongezea ukubwa wa maktaba ya taarifa katika fikra zetu.Kila mtu ana maktaba katika ufahamu wake; ukubwa wa maktaba hiyo hutegemea na uwingi wa taarifa zilizokusanywa na mtu husika.

FAIDA ZA USOMAJI WA VITABU NA MAANDISHI MENGINEYO

Faida ni nyingi sana ila nimefanikiwa kuzitaja chache na muhimu.Usomaji wa vitabu na maandishi mengine UNAWEZA:-

1.UTAKUSAIDIA KUFANYA MAGEUZI YA KIFIKRA AMBAYO KILA MTU HUYAPITIA

Kila mwanadamu ili awe na manufaa kwake mwenyewe na kwa jamii inayomzunguka, lazima apitie mageuzi ya kifikra.Mageuzi haya ndiyo yale yanayofanya binadamu awe tofauti kabisa na vile alivyokua mwanzo na kumnufaisha yeye, kizazi kilichopo na kinachokuja.Kwa sehemu kubwa mageuzi hayo hufanywa bila kupangiliwa yaani (AUTOMATICALLY) ikitegemea na aina za taarifa zinazoingia katika ufahamu wake.Maana yake ndiyo kusema LETE TAARIFA TULETE MAGEUZI, ACHA KULETA TAARIFA TUBAKI KAMA TULIVYO. 


Taarifa nyingi ziko katika vitabu,majarida,makala,matamko ya kiserikari,katika mitandao nk.Hivyo ni muhimu kuchangamkia taarifa hizo ili kupitia hizo tuleta mageuzi ya haraka katika maisha yetu. 

2.  KUKURUDISHA KWENYE NAFASI YA MALENGO YAKO MAKUU.

Nafikiri kuwa kila mtu ana malengo makuu katika maisha yake, Iwe kwa kupangilia au bila kupangilia.Maana yake ni kuwa hata kama hukupanga kuwa na malengo makuu basi mwenendo wa maisha utakupangia malengo makuu.Kilichopo ni kwamba wengi wetu hatujawahi kupata nafasi ya kuainisha malengo yetu makuu na kuyawekea mipango  mahususi.Kufuatia hilo mwenendo wa dunia umetupangia malengo makuu.

Kwa walio wengi malengo makuu yamekuwa yakibadilika badilika kwa kadiri maisha yanavyobadilika.Mfano kama mtu amekuwa hana wazifa wowote serikalini,  anaweza kuweka malengo ya kutafuta wazifa huo na kuutumia kusaidia watu wanyonge.Mara aupatapo na kujiona anaweza kuamua lolote na akasikilizwa, malengo makuu yanaweza kubadilika na kuwa kudhulumu wanyonge haohao ili kuwa tajiri.

Kwasababu hiyo kupitia vitabu na maandishi mengine inaweza kuwa ni njia bora ya kuyafikia malengo makuu katika maisha.Pia inaweza kuwa ni njia bora ya kupata elimu ya kujipangia malengo makuu au kurejea kwenye malengo hayo.

Mfano kama wewe ni msomaji wa vitabu vya dini, katiba na sheria,hutahitaji tena matamko ya Rais na viongozi wa serikali kuhusu haki za binadamu.Wala hutahitaji daktari akutembelee nyumbani kwako kukukumbusha kanuni za afya kama utakuwa tayari umeshasoma majarida yanayohusu kanuni za afya bora.Kwa wale wanaopenda kujiendeleza kielimu hawatakuwa na wasiwasi wa kupotoshwa kuhusu kozi wanazochagua kusoma, kwa kuwa watakuwa wanauelewa mpana kuhusiana na hatima ya fani wanayochukua.

Kwa vyovyote vile usomaji utakupa taarifa nyingi zinazohusiana na kile unachokikusudia au unachofanya  maishani na namna unavyoweza kukifanikisha; haiamkini pamoja na mifano ya watu waliothubutu. Usahihi ulionao na upotofu ulionao utajipambanua pale tu unapopata taarifa sahihi kuhusu mahala ulipo na njia unayoitumia kufikia lengo lako kuu.Kumbuka kufunga goli si bidii tu ya kucheza bali ni pamoja na  kufuata sheria za mchezo na unavyojielekeza kwenye goli .Vitabu vinanafasi kubwa ya kukuonyesha sheria za mchezo na namna ya kujielekeza kwenye goli .Hayo na mengine mengi unayapata kupitia vitabu na maandishi mengine.

3. KUKUFANYA KUA MTU HALISIA
Njia rahisi ya kuishi maisha halisi ni pamoja na kusoma vitabu.Mtu anaweza kujiuliza unawezaje kuishi maisha halisi kwa kusoma vitabu?.Kumbuka kuwa ,kuna dazani ya watu leo wanaoishi maisha ya kukopi tu kutokana na ukosefu wa taarifa sahihi na muhimu kwa maisha yao.Bila shaka umeshawahi kumwona daktari anayemtibu mtu aliyeathirika na sigara angali kuwa yeye mwenyewe ni mvutaji wa sigara na ameshindwa kuacha. 

Wakati mwingine unaweza kumwona kiongozi katika jamii akiwaonya watu kuacha kutumia madawa ya kulevya wakati yeye mwenyewe ni mtumiaji.Unaweza kuona wanachokiishi ni tofauti kabisa na wanachakizungumza.kwa daktari alichohitaji ni taarifa ya namna ya kuacha uvutaji na kiongozi ni jinsi ya kuacha madawa.kwa namna nyingine tunaweza kusema wanaishi wasichokikusudia.

 Wote wawili wanaufahamu mpana juu ya madhara ya matumizi ya vitu hivyo  na hata namna ya kuyatibu madhara hayo.Wanachokikosa ni taarifa sahihi ya namna wanavyoweza kuondokana na matumizi ya vitu hivyo haramu.Taarifa nyingi za kujitoa katika uvutaji wa sigara na madawa ya kulevya ziko katika maandishi kila mahali.

Msomaji wa vitabu hubaki halisi kwa namna anavyoishi,maelezo yake na hata mifano anayoitoa.Yote hayo hutokana na kuwa na hifadhi kubwa ya taarifa sahihi alizonazo katika fikra zake. Kwa maelezo mengine ni kusema kuwa, kushindwa kokote ni kutokana na kukosa taarifa za kutosha kuhusiana na kilichoshindikana.

4. KUKUWEZESHA KATIKA KUCHAGUA MTU WA MFANO KATIKA MAISHA YAKO

Mtu wa mfano ni muhimu sana japo si lazima katika maisha ya kila binadamu (role-model).Kwa wengi huyu ndiye amekuwa dira katika mchakato wa kufanikisha malengo maalumu katika maisha.

Japo wanafalsafa wanasema kuwa binadamu anaweza kujifunza ukamilifu kutoka kwa MUNGU ambaye ndiye mfano wa ukamilifu kutokana na ukamilifu alionao.Lakini unaweza kujazwa nguvu zaidi kuufikia ukamilifu huo kupitia wanadamu wenzako wanaopitia njia zile zile unazozipitia wewe.

Kwa msomaji wa mara kwa mara wa vitabu hachukui muda mrefu kukutana na mtu wa mfano kwa maisha yake.Hiyo inatokana na kuwa ,historia za watu muhimu na mambo mengi huwa katika maandishi tena kwa kujirudiarudia. Kwa maana hiyo inakupasa kujenga tabia ya usomaji wa vitabu na maandishi mengine ambayo ndiyo njia rahisi ya kujikusanyia taarifa kwa wakati tunaouhitaji.

5. KUKUPA MAWAZO NA TAARIFA BILA KUKUTANA NA WATU

Kwa namna ya pekee sana unaweza kutumia usomaji wa vitabu na maandishi mengine kupata mawazo mapya na taarifa mbalimbali bila kukutana na mtu yeyote.Kama hutatumia njia hii ya usomaji utalazimika kuwatafuta watu wakupatie taarifa na mawazo mapya kila siku.Ukweli ni kwamba utakuwa umejidhurumu vya kutosha kwa kuwa hutakuwa na uwezo wa kukutana na watu wengi, tena wale unaowahitaji katika maswala muhimu.Vivyohivyo si rahisi kuwafikia wote kutokana na umbali, muda na sababu nyinginezo.

Kitu muhimu unachoweza ni kijifunza mbinu hii inayoyotumiwa kwa karne nyingi sasa kujipatia taarifa na mawazo mapya kila siku.Mbinu hiyo ni usomaji wa vitabu na maandishi mengine .Bila shaka hutapoteza muda tena na utaanza leo kutumia njia hii ya usomaji kujipatia kila aina ya taarifa hapa duniani. kila la heri.


JINSI YA KUJENGA TABIA YA USOMAJI VITABU

Usomaji wa vitabu imekuwa ni nguzo thabiti ya kupata taarifa kwa watu wengi sana .Faida za usomaji wa vitabu  na jinsi ya kusoma kwa kuelewa nakufaulu nimekwisha eleza katika mada husika waweza kubofya link nilizozitaja.Kunachangamoto kubwa inayosumbua  watu wengi nayo ni kukosa  tabia ya usomaji wa vitabu.

Tabia ya usomaji vitabu sio kitu kinachotengenezwa mara moja bali hujengwa kwa muda mrefu kwa kuzingatia hatua kadhaa na baadhi yake ni kama  ifuatavyo.

Kila siku duniani kuna mambo mapya na yanayohitaji ufafanuzi wa kina.Pamoja na kuwepo kwa vyombo vya habari lakini bado jukumu la kujifahamisha kwa kina kuhusu mambo mapya ni lakwako.jenga mazoea ya  kutafuta taarifa za kina kupitia vitabu kwa kila jambo jipya hata kama ni dogo.Kwa kufanya hivyo utapata faida lukiki zitakazo kufanya kila siku kutafuta taarifa mpya na hivyo kua ni tabia yako.

Faida utakazopata ni pamoja na,
      ·         Kuepushwa na upotoshaji au uyumbishwaji  hasa kwa mambo muhimu,
      ·         Kua na ufahamu mkubwa juu ya mambo mengi yanayotakiwa na jamii mfano mambo ya sheria,afya,kilimo,uchumi,biashara,siasa nk,
      ·        Kua kivutio kikubwa kwa watu hasa linapokuja swala la kuelimishana,
      ·     Kujawa na mifano iliyo hai hasa linapofikia swala la kufanya maamuzi magumu.Pamoja na faida nyinginezo.

Kufanya hivyo kuna weza kukukutanisha na mambo mazuri yatakayofanya iwe ni tabia yako.Kama utajenga mazoea ya kusoma kila maandishi yaliyo mbele yako iwe ni kitabuni ,ukutani au mahala pengine popote basi huo ndiyo utakuwa mwanzo wa kujengeka kwa tabia ya usomaji vitabu.Kama hutaweza kusoma hata tangazo lenye maneno 36 tu basi ni vigumu sana kuweza kusoma kitabu chenye maneno  2000 au zaidi.Ni lazima uanze kujenga mazoea ya kusoma vitu vichache na mwishowe itakuwa ndiyo tabia yako ya kila siku.

Kusoma kilichosomwa na wengi kutakusaidia kuanza kujiamini katika usomaji wako na kwa sehemu kubwa ufahamu wako kufanana na kundi la wasomaji wengine.Kitendo hicho kitakufanya kuanza kupata wanachama au kufahamiana na wasomaji wengine wa vitabu watakaozidi kukushawishi kusoma vingine zaidi.Kwa kadiri utakavyo soma na kusoma ndivyo utakavyokuwa na tabia ya kusoma na kusoma.

Kuna watu ambao hawajawahi kufika maktaba kwa miaka mingi sana tangu walipohitimu masomo yao ya ngazi flani. Tena kuna wengine ambao hawajui hata maktaba inafananaje.Mara utakapofika maktaba utakutana na utitiri wa vitabu vyenye mada mbalimbali za kuvutia.Mada nyingine ni zile zenye majibu ya maswali yetu muhimu ambayo tumekua tukiulizana kila kukicha.

Mfano wa mada hizo ni zile zinazohusiana na dunia na mazingira tunayoishi,teknolojia na maendeleo yake,Chanzo cha magonjwa mbalimbali na matibabu yake,Historia za mambo muhimu duniani, uafafanuzi wa mambo mbalimbali ya kisiasa na kidiplomasia,Elimu ya malezi na uongozaji bora wa kifamilia na ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ya kisaikolojia.

Kadiri utakavyoendelea kutembelea maktaba ndivyo utakavyozidi kutamani kufahamu mengi kwa kutamanishwa na vichwa vya mada zilizomo kwenye vitabu.Mwishowe utajikuta umejenga tabia ya usomaji wa vitabu.Nashukuru kwa kuwa pamoja nami nakutakia usomaji mwema wa vitabu.



Jumapili, 22 Juni 2014

HOW YOU CAN READ FOR BETTER UNDERSTANDING AND PASSING EXAMS


Many people have discussed this topic, but many emphasized on  reader’s circumstances like time for reading, reader’s willingness,place for reading  etc. My emphasis will be specifically on reading  itself which is the source of understanding and passing exams.

The fundamental concept of reading for better understanding and passing, is actually upon  what and how you read and does not depend upon the reader’s surroundings or situation. Remember, we are reading what have been written by human and not angels, therefore we do not require all of them. We need only unique ideas from them which are boon (useful) to our mentality growth.


 The major purpose of reading is strengthening our mentality by absorbing those unique ideas from authors. mentality  is our best capacity of intelligence we use for reasoning and defining things.

Philosophically many will comply with me that, raeding is a better way for accumulating new ideas though there are many ways. Furthermore  the conception of reading is based on strengthening our thoughts for imbibing the knowledge from authors .This is definitely different from colleting  abundant of things from books to mind for
answering examination.

Thank you for being along with me on this preface, now I beg you to continue getting new ideas in your better reading and passing exams.

      1.       PICK UP MAIN IDEAS OF THE AUTHOR

Iam insisting you to take fully attention on this section because this is where the basis of our topic determined.
When I recommend you to pick up main ideas of the author, I mean you must be curious to know the intention or liability of the author’s topic .This will help you not to be confused by the prolonged topic or author’s writing style. You ought to be very keen on your reading concerning with clarifying author’s  main ideas(unique ideas) because that is what your thoughts need.


             STAPES TO FOLLOW IN CLARIFYING MAIN IDEAS FROM AUTHOR.

 A.  UNDERSTAND EVERY SENTENCE OR EVERY WORD IF POSSIBLE IN A TOPIC

It will help you in making  general review for particular topic with no difficulties from what you have read. Many readers are found themselves into reading difficulties for not understanding what they have read .With their reading willingness consume more energy in studying but finally no new ideas obtained due to lack of understanding what is said in a topic.

There are several helpful tools concerned with this like dictionary and more as I have discussed them in section (vii)

B.      EXAMINE YOUR COMPREHENSION  ON A TOPIC YOU READ

Immediately after ending up reading the topic or part of it, close up text book and ask yourself a simple question. What are major facts of the topic?. Now you can describe them comprehensively or in a prepared piece of  paper  by using your familiar language.
Briefly write down what you read then turn back to text book to satisfy yourself that you have managed to collect all main ideas from the author. This will give you more curiousness on the concerned topic since you will be ambitious to know your mistakes in a trial brief. The briefing will help you only being familiar with  the topic whereas  you will be ready for next stape.

Mind you that; many readers end up at this stage and involve into answering questions instead of moving forward  into next stage which is more important than questions6. Questions ends up only at school but mentality is within us always thus building it stronger and stronger should be prioritized.

      C.      LIST ALL MAIN IDEAS OF THE AUTHOR AND DESCRIBE THEM BY YOUR OWN WORDS

This is the specific important stage for gathering new ideas in your reading. Arrange the new ideas acquired from a topic as it is in this HIV topic example.

*meaning of HIV
*HIV transmission
*HIV prevention

Let us assume that these are main ideas revealed in a long HIV topic. Then you can explain as much as you can with the authors language if possible without misconception. Use effectively all main ideas available in the topic starting from the beginning up to the end.

Finally make sure that you have succeeded collecting all main ideas. If not settle for a little moment and then re-start  .

This process will enable you to make the topic being almost yours and not only author’s. From there you will be ready for questions or any presentation of the topic.This is what is known as the reading for better  understanding and passing exams. For sure your mentality is absolutely changed.Besides that you can contribute with your own views in a subjet. Now the subject  is not temporally  tied in your mind that  can accidently drop down and crash but it is the part of your comprehension. Now clearly you can explain about the topic with your own words and not author’s ones.

II. READ ONE TOPIC AT A TIME

Reading more than one topic at a time may affect efficiency of your mind then disable you to commit it to memory. I recommend  that,  having  only one topic at a time is more effective way for reading.


III. REVIEW  THE NOTES PREPARED BY YOURSELF
Reviewing your own prepared  notes is more important because it will help you to easily keep in memories  what you have read from the particular subject. Most of we readers tend to have funny reading. We directly hit on somebody’s  notes  or text book for cramming  without digesting them so that they become absorbable then finally being  part of our comprehension .   Don’t  waste  your time for impelling yourself assimilating somebody’s conception before converting it to become your imagination .


IV. REVIEW THE SAME SUBJECT FROM OTHER AUTHORS

Now being experienced with the subject, you can review it from other authors. That will make you competent on the subject that you can independently describe and observe with some research on it. 

V. KEEP THE TIME WHEN READING

Iam not optimistic to what time is suitable for reading . some recommend that the suitable time for reading  is eight O’clock to ten O’clock evening . Some recommend  four O’clock to ten O’clock morning.
I don’t want to argue with them but I believe somebody can read/study at any time except he/she is totally  tired .


You are required not to involve into any business out of reading. Many loose attention for their reading when they simultaneously reading while chatting, talking, watching news, listening to beats/music etc. This causes them to loose most of their new obtained ideas when considering what is going on out of reading. Eventually it makes their general review to become unexpected.

VI. AVOID OVERNIGHT STUDYING

 Overnight studying style is encouraged by wrong notion and is totally  pessimistic. For the sake of drawing attention to their learners, some old teachers could claim to have overnight studies during their schooling age.

It is unhopeful using this way because it may confuse you since you
will have no time to clarify major facts from what you are reading. That is due to a number of topics being read at a time without having time for distinguishing and analyzing main factors. Consequently you will not be able to make the new information become part of your knowledge.

VII. USE THE CORRECT DEVICES/TOOLS  IN YOUR READING /STUDY

There are number of DIVICES/tools that can make your study become luxury so that you can study while enjoying it. The  following are some useful tools for reading.

COMPUTER 


You can find a computer and install some useful softwares for studying .These softwares are like ADOBE READER, PDF-SUITE, PDF CREATER, GOOGLE DRIVE and more alike.They may help you to convert format of your files and easily save them online with GOOGLE DRIVE through your GOOLE ACCOUNT or ADOBE ACROBAT ACCOUNT. 

That is an extra benefit once your files in your computer or elsewhere are damaged or stolen.You can possibly  access them online through even your mobile. Apart from that, adobe program can be enhanced to raed aloud for you and you becoming  a listener.

You can install different dictionaries according to your needs. microsoft office has been so useful software for both scholars and officers therefore you can install a very suitable version for your studies.
By using your  computer you can share your notes and questions with your friends  by using window installed in it as fast as you want .

Once you become disabled or blind with your computer you can still progress with your reading or studies. You can use some application programs like speech recognition,Dragon naturally speaking,TalkItTypeIt etc which after editing  some commands, you can speak and your computer can type for you.

You can click (jinsi ya kusoma kwakusikiliza adobe in Kiswahili) and learn from pictures how you can use adobe to read from listening to your computer.



These tools can store electronic memories like pictures, voice and writings according to the capacity of your tool. You can carry as many pages as for the year for your studies depending on the capacity of your flash or disc. All of these can be used at any computer or laptop anywhere you find them.
Mind you that; these tools once they are damaged can’t be able to show the stored data therefore it’s better to store the same data in another tool for it’s safety.
  


Many of the smart phone or tablets can play major role in our studies or reading especially when we are far from home. What you can do to those who don’t have window phone,is to download the application program online that can function in many android phones. These applications may help you to open PDF and XPS format  files that will have been stored in your phone memory or memory card attached to your phone. Also can help opening files stored online.

Some application program with easy functionality in android phone are android pdf viewer,quickoffice and e-book droid  .You can also download other application like online dictionary,Wikipedia  which can be helpful for giving you instant translation to the new vocabularies.



It is very important for somebody with substantial desire for understanding and passing exams to have this tool or one alike. Dictionary will help you to translate new vocabularies used by author  instead of asking from another person.

By using this aid to your reading, Iam sure you will be benefited a lot. Now you will not continue With your common reading style but the most constructive like one obove.



  


Jumapili, 15 Juni 2014

SABABU ZA KUFELI MTIHANI


Baada ya kutatua tatizo la uandikishwaji  wa wanafunzi wapya mashuleni na vyuoni  kila mwaka, karibu duniani kote,Hivi sasa kumeibuka tatizo jipya la kufeli mitihani.Tatizo hili ambalo wengine kwa kuogopa neno matatizo  wamelibatiza jina changamoto, limekuwa kubwa karibu duniani kote.

Kwa ufupi karibu kila mahali duniani uandikishwaji (udahili) wa wanafunzi wapya umeongezeka.

Mfano mzuri ni kwa Tanzania ambayo ni moja ya nchi ya mfano kusini mwa jangwa la sahara. Ilitimiza dira ya maendeleo ya dunia ya elimu ya mwaka 2025 kwa kufikia uandikishaji wa 103% hapo mwaka 2012.Vile vile takwimu za banki ya dunia zinaonyesha kuwa mpaka kufikia mwaka 2010 ilifikia 95.4% ya uandikishaji wa wanafunzi kwa shule za msingi toka chini ya asilimia 60% mwaka 2000.

TAKWIMU KWA UFUPI

Mafanikio hayo sio kwa Tanzania tu, bali zipo na nchi nyingine zilizofanya vizuri katika uandikishaji wa watoto shule . Miongoni mwa nchi hizo ni

ARMENIA 114 mwaka 2009,    AUSTRALIA 100% mwaka 2009,

BAHAMAS, THE 103% mwaka 2009 ambayo ilishuka 1% mwaka uliofuata,

BANGLADESH 105% mwaka 2009,   GHANA 100% mwaka 2013,

GERMAN 100% mwaka 2009,   CHINA 100% mwaka 2009,

GUYANA 108% mwaka 2009, UNITED STATES 100% mwaka 2009 na kushuka 2% mwaka 2012.

kwa nchi za afrika mashariki

KENYA 98% mwaka 2009 na hakuna takwimu kwa miaka iliyofuata,

UGANDA 102% mwaka 2011,

BURUNDI 99% mwaka 2012,

RWANDA 103% mwaka 2009 na kushuka 1% mwaka 2012.

Takwimu hizi ni kwa mujibu wa bank ya dunia kwa watoto wenye umri wa kwenda shule.
Kutokana na kuongezeka kwa uandikishwaji wa watoto shule za msingi hata sekondari na vyuo vimepata ongezeko kubwa la wanafunzi wapya kila mwaka.Isingetosha kutazama takwimu kwakua sio mada yake.

TATIZO LA KUFELI MITIHANI.

Tatizo hili limekuwa ni kubwa sana na kuwaathili  wazazi ,walezi ,walimu ,serikali na hata  wanafunzi wenyewe.Ukubwa wa tatizo umesababishwa na wadau wenyewe wa elimu ikiwamo wanafunzi.Mbaya zaidi ni kwamba katika kushughulikia hili tumejikita zaidi katika mambo ambayo yako nje ya uwezo wetu na sio yaliyo ndani ya uwezo wetu.

Leo ukimuuliza mtu kwa nini wanafunzi wanafeli mitihani? Atakujibu kirahisi tu kuwa madawati hayatoshi.mwingine atakwambia walimu hawatoshi.
Ninachotaka kusema ni kuwa hata kama kila mtu atakaa kwenye kiti chake darasani na kupata mwalimu wa kumfundisha peke yake, kunauwezekano bado wa kupata watu wanaofeli mitihani. Najua utashangaa kidogo kwa maelezo hayo yaliyo kinyume kabisa na mawazo ya wengi.Ila utanielewa katika kipengele kinachofuata.

KWA NINI WATU WANAFELI MTIHANI

Tatizo kuu la watu kufeli mtihani ni kutoelewa walichojifunza au kuelewa kwa kiasi kidogo sana.Kutoelewa kunatokana na sababu kadhaa ambazo zimeorodheshwa hapo chini tafadhali pitia kwa umakini.

1.UWEZO MDOGO WA KUELEWA HARAKA

Kila mtu hapa duniani ana akili,tena akili za kutosha, isipokuwa kwa wale wenye magonjwa yanayohusiana na akili.Kusema hivyo ni kwamba kila mtu anauwezo wa kufaulu mtihani, ilimradi tu kama alipata nafasi ya kujifunza.

Watu wenye uwezo mdogo wa kuelewa haraka huwa wanafeli kutokana na kutopata muda wa kutosha kueleweshwa.Kundi hili lina idadi kubwa sana ya watu mashuleni kuliko wale wanaoelewa haraka.Kwa kawaida mwalimu hutumia dakika zisizozidi 40 darasani akifundisha.Ni dhahili kuwa muda huu hautoshi kufanya kila kitu kinachomwezesha mwanafunzi kubaki ameelewa 100%.Hivyo kundi la hawa wanafunzi wasioelewa haraka hubaki na pengo la kuelewa kila siku wanapotoka darasani.

Wakati bado wanashughulikia pengo lao ili wafanane na wale wenzao walioelewa,  hujikuta wakikabiliwa na mitihani.Matokeo yake hujikuta wakijibu mtihani ama kwa jinsi wanavyoelewa wao au kwa kubahatisha, hivyo kufeli mtihani.

SULUHISHO.

Ni vizuri kujikagua hasa kwa wale wanafunzi wakubwa, kama unatatizo la kutoelewa haraka.Utafahamu kirahisi kama unatatizo hilo kwa kujipima na wenzako ambao mnajifunza pamoja kwa kuona wakiwa wameelewa na wewe ukiwa bado.Pia unaweza kujipima kwa kujiuliza maswali madogo madogo yanayohusiana na ulichojifunza kuona kama unaweza kujijibu. Pia kwa wale wenye watoto unaweza kumpima  kwa kumlinganisha na watoto wengine au kwa maswali madogo madogo.

Utatuzi sio kwenda ( kumpeleka mtoto)  tuition, kwani hata huko unaweza kukumbana na tatizo lilelile.Cha kufanya ni kutumia muda mrefu zaidi kujifunza kitu kilekile hata kama ni kwa mwalimu yuleyule mpaka uelewe.Hapo ndipo utakapoona unafaulu.kumbuka hata ulipoanza kujifunza kusema  ungali mdogo, ulikosea kila neno ,lakini kila siku ulirudia maneno yaleyale mpaka sasa huhitaji hata kujikumbusha unapotaka kuyatumia.


2. ULEMAVU
Kama mwanafunzi hajakaguliwa sawasawa kuhusiana na ulemavu na kuhudumiwa kipekee ,kunauwezekano mkubwa wa kufeli mtihani.ulemavu ambao una madhara makubwa sana katika ufaulu ni pamoja na ulemavu wa akili,uoni hafifu na kutosikia vizuri.Kuna baadhi ya wanafunzi wenye uoni hafifu au kutosikia vizuri wasiojulikana na walimu wao.Kwasababu ya kutojulikana kwao hujikuta wakijifunza kwa mashaka tu mpaka mwalimu  anamaliza kufundisha  darasani.Matokeo yake hujikuta wakiwa hawajaelewa mpaka mitihani inapowakuta.

SULUHISHO

Ni vema kujikagua au kumkagua mwanafunzi kama ana matatizo niliyokwisha yataja.Endapo kama unamatatizo hayo au mojawapo basi ni vema kuhakiki kuwa hayaathili kuelewa kwako.Kama yana athili basi tumia njia inayokufanya uelewe na sio kubaki na deni la kutoelewa kila utokapo darasani.

3.UWEZO MDOGO WA KUCHUKULIANA NA MAZINGIRA

Mwanafunzi mwenye uwezo mdogo wa kuchukuliana na mazingira, anaweza kuelewa taratibu au kutoelewa kabisa na kujikuta akifanya vibaya katika mitihani yake.Hapa ndipo unapokuja ule usemi ninaoupenda sana usemao kile usichoweza kukizuia kiepuke.

Mazingira yanaweza  kumuathili mwanafunzi endapo kama hatoelewa nini cha kufanya wakati yanapofikia hatua ya kuathili uelewa wake darasani.
Hapa ndipo unapoweza kuona tofauti .Kwamba mwanafunzi anayeishi katika mazingira magumu au kutoka familia yenye kipato kidogo na vyenzo chache za kujifunzia anafaulu mtihani, lakini Yule mwenye kila kitu anafeli.Yote inatokana na uwezo wa kifikra alionao mwanafunzi katika kukabiliana na mazingira kama hayo.Uwezo huu huwa ni wa kibinafsi zaidi na sio ule unaotokana na mafunzo maalumu.


Mazingira yenye athali yanaweza kuwa uchumi duni,uhaba wa walimu au wakufunzi,umbali wa shule au chuo,uwezo mdogo wa walimu au wakufunzi kufundisha,nyenzo chache za kujifunzia au  kufanya mazoezi (practicals),changamoto za kirika (mapenzi,starehe).Hivi vyote ni vikwazo katika kuelewa kwa mwanafunzi shuleni.

SULUHISHO

Kama kunamazingira yeyote yanayokufanya au yanayomfanya mwanafunzi kushindwa kuelewa darasani au kwingineko, jambo la kwanza ni kuyaepuka.Ikiwa ni umbali tafuta kukaa karibu na shule/ chuo,kama ni uwezo  duni wa walimu au wakufunzi tafuta wakufunzi,kama ni nyenzo chache jifunze kutumia zilizopo au zinazopatikana kwingineko.

Tafuta na kuelewa kama udhaifu  wa kuelewa kwako  darasani  unasababishwa na mazingira uliyonayo. mazingira usiyoweza kuyakabili unachofanya ni kuyaepuka .Kuepuka ni njia rahisi sana katika mapambano yeyote yale.Nafikiri endapo kama utapewa miujiza ya kuweza kukwepa masumbwi yoyote hapa duniani, basi ungelijitosa katika mashindano ya masumbwi ya pesa nyingi kwa kutegemea uwezo wako wa kukwepa masumbwi.Ungefanya hivyo kwa kuwa usingetegemea kupangua au kuhimili kipigo cha konde lolote kutoka kwa mshindani wako kwa kuwa unauwezo wa ajabu wa kukwepa makonde.

Endapo mazingira uliyonayo hayaepukiki basi njia ya pili ni kujenga nayo urafiki ili uyatumie kwa manufaa yako.Anza kujenga ukakamavu wa kuishi katika mazingira ambayo huyapendi ili yasiharibu uelewa wako darasani.

Sote tunafahamu kuwa gerezani ni mahala penye maisha magumu sana ,lakini mfungwa anaweza kuishi miaka 30 na zaidi.

Sote tukisikia mlipuko wa bomu au risasi tunakimbia hovyo ,lakini askari anaweza kukaa vitani na milipuko hiyo mpaka atakapopata amri ya mkuu wake kuondoka ili asifukuzwe jeshini.

Sote tunafahamu kuwa ni vigumu kwa binadamu yeyote kukaa macho usiku mzima bila kulala, lakini leo tuna mamilioni ya watu duniani wanaokesha kwa hiari yao viwandani ili mwisho wa mwezi waweze kujipatia kipato.

Kwasababu hiyo hata wewe unaweza kujenga ukakamavu wa hiari kukabiliana na mazingira uliyonayo ili yasipunguze uelewa wako darasani .Kwa kuzingatia ushauri huu nina imani sasa hautafeli tena mtihani na utakuwa msaada kwa wengine.


Usikose ku “ LIKE” page yetu ya facebook ujipatie masasisho mapya kila yanaporushwa kwenye mtandao. karibu. https://www.facebook.com/pages/Free-tuition/260313704137723?ref_type=bookmark

Alhamisi, 12 Juni 2014

BOOKS SERVICE ANYWERE YOU ARE


Now books are available wherever you are . No matter which kind of book you are looking for and where did you saw it, through our contacts we can bring it where you are . 

For now, available books are HARD COPIES and E-BOOKS.You can get Hard copies for all kind of books,  but for E-BOOKS only few (skills books).

KIND OF BOOKS AVAILABLE ARE,

GENERALITIES,

PHYLOSOPHY & PSYCHOLOGY,

SOCIAL SCIENCE,

LANGUAGE,

NATURAL SCIENCE & MATHEMATICS,

TECHNOLOGY ( APLIED SCIENCE),

THE ART,

LITERATURE & RHETORIC,

GEOGRAPHY & HISTORY.

Price will be announced on our facebook page therefore” LIKE” our facebook page to get updates all the time .You can get  wholesale  and retail regardless to the distance of your district or region from DAR ES SALAAM. 

Since it’s not easy to announce all books price, you can communicate with us through our contacts.

Mobile : 0758 73 17 13
Mobile  : 0653 67 00 13

We are located at ,  ILALA/ DAR ES SALAAM / TANZANIA

HUDUMA YA VITABU MPAKA NYUMBANI


Sasa vitabu vinapatikana popote ulipo.Bila kujali ni kitabu cha aina gani na ulikiona wapi, kupitia mawasiliano yetu utaletewa popote ulipo.

Vitabu vinavyopatikana kwa sasa  ni Hard copies na E-books.Hard copies ni kwa aina zote za vitabu  na E-Books ni kwa baadhi ya vitabu (short skills books).Unaweza kujipatia kwa jumla na rejareja bila kujali wilaya au mkoa unaoishi .

Aina ni zote , ikiwamo

GENERALITIES,

PHYLOSOPHY & PSYCHOLOGY,

SOCIAL SCIENCE,

LANGUAGE,

NATURAL SCIENCE & MATHEMATICS,

TECHNOLOGY ( APLIED SCIENCE),

THE ART,

LITERATURE & RHETORIC,

GEOGRAPHY & HISTORY.

BEI YETU ITAKUWA IKITANGAZWA KWENYE UKURASA WETU WA FACE BOOK. HIVYO LIKE UKURASA WETU UPATE TAARIFA MPYA KILA WAKATI .KWA KUWA NI VIGUMU KUTANGAZA BEI YA KILA KITABUWASILIANA NASI KUPITIA  MAWASILIANO YAFUATAYO,


Simu    : 0758 73 17 13

Simu    : 0653 67 00 13


TUKO  ILALA/ DAR ES SALAAM/ TANZANIA