Ijumaa, 8 Agosti 2014

JINSI YA KUJENGA TABIA YA USOMAJI VITABU

Usomaji wa vitabu imekuwa ni nguzo thabiti ya kupata taarifa kwa watu wengi sana .Faida za usomaji wa vitabu  na jinsi ya kusoma kwa kuelewa nakufaulu nimekwisha eleza katika mada husika waweza kubofya link nilizozitaja.Kunachangamoto kubwa inayosumbua  watu wengi nayo ni kukosa  tabia ya usomaji wa vitabu.

Tabia ya usomaji vitabu sio kitu kinachotengenezwa mara moja bali hujengwa kwa muda mrefu kwa kuzingatia hatua kadhaa na baadhi yake ni kama  ifuatavyo.

Kila siku duniani kuna mambo mapya na yanayohitaji ufafanuzi wa kina.Pamoja na kuwepo kwa vyombo vya habari lakini bado jukumu la kujifahamisha kwa kina kuhusu mambo mapya ni lakwako.jenga mazoea ya  kutafuta taarifa za kina kupitia vitabu kwa kila jambo jipya hata kama ni dogo.Kwa kufanya hivyo utapata faida lukiki zitakazo kufanya kila siku kutafuta taarifa mpya na hivyo kua ni tabia yako.

Faida utakazopata ni pamoja na,
      ·         Kuepushwa na upotoshaji au uyumbishwaji  hasa kwa mambo muhimu,
      ·         Kua na ufahamu mkubwa juu ya mambo mengi yanayotakiwa na jamii mfano mambo ya sheria,afya,kilimo,uchumi,biashara,siasa nk,
      ·        Kua kivutio kikubwa kwa watu hasa linapokuja swala la kuelimishana,
      ·     Kujawa na mifano iliyo hai hasa linapofikia swala la kufanya maamuzi magumu.Pamoja na faida nyinginezo.

Kufanya hivyo kuna weza kukukutanisha na mambo mazuri yatakayofanya iwe ni tabia yako.Kama utajenga mazoea ya kusoma kila maandishi yaliyo mbele yako iwe ni kitabuni ,ukutani au mahala pengine popote basi huo ndiyo utakuwa mwanzo wa kujengeka kwa tabia ya usomaji vitabu.Kama hutaweza kusoma hata tangazo lenye maneno 36 tu basi ni vigumu sana kuweza kusoma kitabu chenye maneno  2000 au zaidi.Ni lazima uanze kujenga mazoea ya kusoma vitu vichache na mwishowe itakuwa ndiyo tabia yako ya kila siku.

Kusoma kilichosomwa na wengi kutakusaidia kuanza kujiamini katika usomaji wako na kwa sehemu kubwa ufahamu wako kufanana na kundi la wasomaji wengine.Kitendo hicho kitakufanya kuanza kupata wanachama au kufahamiana na wasomaji wengine wa vitabu watakaozidi kukushawishi kusoma vingine zaidi.Kwa kadiri utakavyo soma na kusoma ndivyo utakavyokuwa na tabia ya kusoma na kusoma.

Kuna watu ambao hawajawahi kufika maktaba kwa miaka mingi sana tangu walipohitimu masomo yao ya ngazi flani. Tena kuna wengine ambao hawajui hata maktaba inafananaje.Mara utakapofika maktaba utakutana na utitiri wa vitabu vyenye mada mbalimbali za kuvutia.Mada nyingine ni zile zenye majibu ya maswali yetu muhimu ambayo tumekua tukiulizana kila kukicha.

Mfano wa mada hizo ni zile zinazohusiana na dunia na mazingira tunayoishi,teknolojia na maendeleo yake,Chanzo cha magonjwa mbalimbali na matibabu yake,Historia za mambo muhimu duniani, uafafanuzi wa mambo mbalimbali ya kisiasa na kidiplomasia,Elimu ya malezi na uongozaji bora wa kifamilia na ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ya kisaikolojia.

Kadiri utakavyoendelea kutembelea maktaba ndivyo utakavyozidi kutamani kufahamu mengi kwa kutamanishwa na vichwa vya mada zilizomo kwenye vitabu.Mwishowe utajikuta umejenga tabia ya usomaji wa vitabu.Nashukuru kwa kuwa pamoja nami nakutakia usomaji mwema wa vitabu.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni