Jumanne, 27 Mei 2014

MBINU ZA USHINDANI KATIKA ELIMU


Bila hata kumeza mate naweza kusema kuwa hata katika elimu kuna mbinu za kiushindani. Na ushindani huu ni ule unaopatikana ndani ya darasa na hata baada ya kuhitimu kiwango fulani cha elimu.Ndani ya darasa ni kuwa kinara kwa  kujipatia ufaulu unaoridhisha na nje ya darasa ni ule ufanisi anaokuwa nao muhitimu katika utendaji wake.

Ukosefu wa mbinu hizo unaweza kukusababishia kushindwa vibaya darasani na hata baada ya kumaliza shule au chuo.Vilevile ningependa kusema kuwa,mbinu hizi ni za ujumla na zina muhusu mtu yeyote anayesoma ngazi yeyote ya elimu iwe rasmi au si rasmi. Pia zina muhusu hata Yule anayetarajia kujiunga na elimu wakati wowote.

1.     KUWA WA KWANZA KUPATA TAARIFA ZINAZO KUHUSU


Taarifa ni muhimu kwa kila mtu.Lakini muhimu zaidi ni zile zinazo kuhusu, mfano kama wewe ni mwanamichezo basi utakuwa hufanyi busara kama kila kukicha utakuwa ukitafuta habari za siasa.Ni wazi kuwa hazitakuwa na tija sana katika uwanamichezo wako japo zitakusaidia.

Vivyo hivyo kwa mwanafunzi au kwa mwana kisomo yeyote ,unalazimika kuwa wa kwanza kupata taarifa zinazo kuhusu kuliko mtu mwingine yeyote.kufanya hivyo kutakusaidia kujua kinachoendelea katika elimu,mabadiliko mapya,fursa mpya za elimu,changamoto,na mwelekeo  wa elimu yako kwa ujumla.Taarifa hizi utazipata kupitia vyanzo vyote vya habari ikiwamo mitandao, na jamii iliyokuzunguka.

Manufaa utakayoyapata ni pamoja na ufahamu wa kutosha kuhusu elimu (awareness),kujipanga haraka kama kuna mabadiliko mapya au changamoto,kuwa wakwanza kupata fursa kama zipo,kuendana na wakati (up-to-date).Kwa sababu hiyo wewe ndiye utakaye kuwa kinara katika mkondo  wako wa elimu na  mwamuzi wa hatima ya elimu yako na si mazingira.

2.     USIRIDHIKE KUONGOZA DARASANI

Kuridhika kuongoza kundi dogo la darasa lako kunaweza kuleta matokeo mabaya sana mwisho wa safari ya elimu yako.Hapa ningeomba nitumie msemo mmoja ambao nimekuwa napenda sana kuutumia (don’t run faster to be the first but the best) usikimbie zaidi ili kuwa wakwanza bali kuwa bora kuliko wote.

Wakati mwingine katika mtiririko wako wa elimu unaweza kukutana na watu ambao uwezo wao wa kuelewa ni wa kiwango cha chini sana, hivyo kukufanya wewe kuwazidi kimatokeo kila kukicha.Kinacho kupasa kufanya ni kujipima kimatokeo na alama za juu kabisa za ufaulu hata kama umekuwa ukiwazidi  wenzako mlio kundi moja.

3.     JITAHIDI KUA BORA KULIKO KIWANGO CHA ELIMU YAKO

Hapa nina maana kuwa uelewa utakao kua nao uwe zaidi ya elimu uliyopata darasani.Elimu tunayoipata darasani hata iwe ya degree ngapi ,ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji makubwa ya elimu inayotakiwa katika maisha yetu.Na kwasababu hiyo ndiyo maana hata kama umesoma vipi bado kutakuwa na uhitaji wa elimu ya ziada ili kukidhi sehemu kubwa  ya mahitaji muhimu ya kimaisha.

Sasa, ili kumudu ushindani wa elimu na wewe kuwa bora kuliko ilivyo kawaida inategemea ni  jinsi gani utakavyokuwa ukijielimisha zaidi kuliko kutegemea kuelimishwa tuu darasani.

Kutofanya hivyo ndiyo kusema kuwa tutakuwa na kundi kubwa la watu wenye viwango vya juu vya elimu lakini linapokuja swala la uelewa na ufanisi kiutendaji ni kitendawili.

*Tunakua na wahitimu wengi wa darasa la saba lakini kiwango chao cha uelewa  na ufanisi kinafanana na cha  darasa la pili.
*Tunakua na wahitimu wengi wa form four lakini kiwango chao cha uelewa kinafanana na cha darasa la saba.
*Tunakua na wahitimu wengi wa kidato cha sita lakini uelewa wao na ufanisi unafanana na form two.
*Tunakua na wahitimu wengi wa vyuo lakini uelewa wao unafanana na ule ambao angekuwa nao muhitimu wa form four.

Vivyo hivyo wakati mwingine inakupa shida kusikia kuwa mtu fulani ana degree mbili na kadhalika,yaani alivyo kwa ujumla wake hafanani na kiwango cha elimu aliyonayo.Hafanani kwa jinsi anavyoamua mambo,hafanani kutokana na matokeo ya kiutendaji anayoyapata,hafanani kwa jinsi anavyojieleza,hafanani kwa jinsi anavyojitambua,wala hafanani kwa jinsi anavyochangia katika jamii.

Nashauri kuwa , jitahidi kubadilisha hali hii yaani iwe hivi:-
 kwa muhitimu wa darasa la saba ue na uelewa kama wa muhitimu wa form four na zaidi; yaani ikitokea mtu hakupata nafasi ya kukuuliza adhanie kuwa wewe ni muhitimu wa kidato cha nne au zaidi.


Kwa wale wa degree moja jijenge kiasi kitakachofanya mtu afikirie kuwa pengine  una mbili au zaidi.


form four na six angalau mtu akijichanganya ahisi kuwa labda ni muhitimu wa chuo au degree kwa jinzi ulivyojitahidi kukuza Thamani ya elimu yako kwa kujielimisha binafsi kila kukicha.


Kufanya hivyo kutakupa  Manufaa ya kuwa mtawala wa kiwango cha elimu uliyoifikia  na kama utapimwa kwa kigezo cha elimu husika, basi wewe utakuwa uko mbali kupita kiasi.Hata hivyo,hiyo ndiyo itakuwa mundu wa kutakatisha njia kuelekea mafanikio kupitia elimu uliyoipata.

4.     EPUKA DHANA POTOFU ZINAZOHUSU ELIMU

Mada hii ya dhana potofu kuhusu elimu  nimeizungumzia kirefu katika mada inayosema MBINU ZA KUEPUKA DHANA POTOFU DHIDI YA ELIMU ukipata nafasi unaweza kusoma mwenyewe.
Kifupi naweza kusema kuwa kumekuwa na dhana nyingi potofu zinazohusu elimu ambazo unahitaji kuzifahamu mapema na kuziepuka.Baadhi ya dhana hizo ni kama ifuatavyo,

       Ipo dhana inayosema kuwa wahitimu wa elimu ya sasa hawana wanacho kielewa hivyo hawana tija kwa jamii.Kitu ambacho si kweli kwasababu ushahidi umeonyesha kuwa darasa la saba,form four na six wote wamefanya vizuri  jeshini,polisi ,magereza,viwandani,super markets,mashanbani,kwenye biashara ndogo na kati na maeneo mengine kwa kupata mafunzo kidogo tu ya kuwawezesha kumudu shughuli zao.Tena cha kushangaza zaidi wengine wamemudu bila hata mafunzo yeyote ya ziada.

2       Kuna dhana kuwa wahitimu wa vyuo wengi hawana uwezo katika uzalishaji.Wakati dhana hii ikiendelea kukuzwa ndiyo kwanza hivi sasa kigezo kikubwa katika soko la ajira za maofisini ni angalau degree moja.Hii inaonyesha kuwa sio kweli kwamba hawana uwezo bali wengi wao wanzagaa mtaani na pale wasipo hitajika kwa kukusa cha kufanya.

3       Ipo dhana kuwa ukisoma sana hutapata kazi .Dhana hii imewafanya watu wengi kuvunjika moyo wa kuweka mikakati ya elimu ya kufika mbali kwa kudhani kuwa haitawasaidia sana,eti kwamba ukisoma sana waajiri watakuogopa.

      Dhana hii sio kweli kwa kuwa ushahidi umeonyesha kuwa waliosoma sana ndiyo wenye fursa kubwa zaidi katika soko la ajira.Vivyo hivyo hata katika swala zima la  ufanisi wa kazi ,mtu mwenye elimu kubwa zaidi ndiye mwenye ufanisi mkubwa zaidi katika utendaji.

Hii iko hivi; mtu mwenye kiwango kidogo cha elimu namfananisha na mashine yenye nyenzo chache na zisizo na ubora; inayotumia nguvu nyingi na kupata matokeo kidogo.Mfano inaweza kuwa ni mashine inayo tumia mafuta mengi ,inafanya kazi taratibu na ubora wa kazi ni hafifu. Mtu  mwenye kiwango kikubwa cha elimu namfananisha na mashine iliyoboreshwa na kuwekewa nyenzo nyingi zinazoweza kufanya kazi haraka na kwa urahisi na kwa kiwango cha hali ya juu, hivyo kuleta matokeo makubwa.

 Hilo unaweza ukaliona  mahospitalini kwa madaktari bingwa,kwa watafiti wa kilimo,wanafalsafa,saikolojia,wanasheria,mainjinia,wahadhili vyuoni nk.


Sio lazima kuwa ukisoma basi utalazimika kuajiriwa,bali unaweza kuitumia fursa ya elimu uliyoipata kwa kutengeneza ajira binafsi na za wengine.
Kuna dhana nyingine nyingi potofu ambazo zinaweza kukuvunja morali wa kutafuta elimu zaidi ambazo isingekuwa rahisi kuzitaja hapa, bila shaka utazisoma katika mada husika .

5.     EPUKA KUFIKIRI KUJA KUWA NANI BALI KUFANYA NINI.

Jiepushe kabisa na fikra za kizamani za kuja kuwa waziri,mbunge,meneja katika maofisi makubwa,na vitu vinavyofanana na ubosi ubosi.Ondoa fikirani mwako taswira za kimwonekano  bali za kiutendaji. Kumbuka hatusomi ili tuje kuwa nani bali kuja kufanya nini.sahau kuhusu kuwa mwalimu bali  kufundisha,sahau kuhusu kuja kuwa daktari bali kutibu watu,sahau kuhusu kuja kuwa afisa kilimo bali kulima,sahau kuhusu kuja kuwa meneja biashara bali kufanya biashara nk.Ili uwe na ushindani wa kutosha katika elimu ni pale unapo jidhatiti kuja kufanya nini baada ya kuhitimu masomo yako.

Kitendo cha  kufikiri kufanya nini na si kuja kuwa nani kitakuongezea bidii ya kujifunza na kujijengea uwezo binafsi juu ya kile unachojifunza.Kumbuka nafasi yako ya kujifunza ni ile unapokuwa darasa na  baada ya kuhitimu kinachofuata ni uzalishaji.Na wajibu wa kuzalisha utakuwa ni wako wala si wa mtu mwingine.

6.     FAHAMU KUHUSU NGAZI YA ELIMU INAYOFUATA

      1.       JIFAHAMISHE KUHUSU UTAKACHOTAKIWA KUJIFUNZA  BAADA YA UNACHOJIFUNZA SASA
     kitendo hicho kitakusaidia kukupa mwanga wa kule unakokwenda kitaaluma na kukupa ufahamu wa ziada juu ya unachosoma.Utakapofika kujifunza itakuwa sawa na mtu anayefanya safari ya kurudi yaani si mgeni tena na anachofundishwa.


      2.       PATA TAARIFA WAPI INAPATIKANA ELIMU UNAYOITAKA
      Hapa ni pamoja na kuhudhuria makongamano ya elimu,kutafuta taarifa kutoka vyuoni na kwingineko.
      Ni ajabu iliyoje kuona mtu anamaliza kidato cha sita hajui  asome kozi gani,chuo gani,na kwa sifa gani.Vivyo hivyo kwa darasa la saba, zifahamu shule zinazotoa elimu ya sekondari na mahali ziliko na mahali pengine panapotoa elimu kama hiyo.

kwa wanafunzi wa kidato cha nne ni lazima ujiweke tayari kujua shule zinazotoa elimu ya A’level, vyuo vinavyotoa kozi mbalimbali , sifa za kujiunga ikiwamo kozi zinazotolewa.Sio busara kudhani kuwa unaweza  kuja kusoma kozi yeyote tuu, kitu ambacho kitakufanya kujiingiza katika kozi zisizoendana na kipaji chako. Ili kujielimisha zaidikuhusu swala hili unaweza ku bofya mada hii JINZI YA KUTAMBUA KIPAJI CHAKO.


kwa wale watu wa vyuo ni muhimu kujifahamisha mapema ni kozi gani zitakazo kufaa baadaye na zinapatikanaje kwa hatua inayofuata.

      3.       PATA TAARIFA YA SOKO LA AJIRA KABLA HUJAJIUNGA NA KOZI
            Utafiti juu ya soko la ajira ni muhimu na hii itakusaidia kujua changamoto zilizopo na kama soko la ajira hakuna utajiweka tayari kulitengeneza.

(Note)Katika utafiti wa soko la ajira pata taarifa sahihi kutoka kwa watu wanaohusika na soko husika na si kuuliza uliza kwa kila mtu.
     4.       SHIRIKIANA NA WATU WENYE MAENDELEO MAZURI KITAALUMA
     Shirikiana na watu ambao utanufaika kielimu kutoka kwao na wale wale wenye mwelekeo wa kile unachokitafuta.
Kwa mbinu hizi chache ninaimani zitakuongezea nguvu katika ushindani wa elimu na hivyo utakuwa sio muhitimu tu bali muhitimu bora kwa manufaa yako na kwa jamii iliyokuzunguka.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni