Jumapili, 13 Aprili 2014

JINSI YA KUSOMA KWA KUSIKILIZA UKITUMIA ADOBE READER




Hatua ya 1.

Install adobe Reader kwa wale wasio na program hii kwenye Computer zao.
Ni vyema ku install toleo jipya zaidi .unaweza kudouload kutoka kwenye mtandao au kutoka kwenye kifaa chochote kilichohifadhi program hii.Unaweza kujipatia program hiyo bure mfano kwenye Link hii.    http://www.adobe.com/products/reader.html

Hatua ya 2

Badili format ya faili zako kuwa katika mfumo wa PDF file ili uweze kuyafungua kwa kutumia program hiyo.Somo hilo sio mahala pake tutalizungumzia kwenye mada yake.

Hatua ya 3

Fungua faili yeyote yenye format ya PDF Kwenye Computer yako.Mfano





Hatua ya 4

Katika menyu bar ya faili lako bofya ( View )





Hatua ya 5

Kwenye Drop down menyu itakayotokea elekeza poiter (kamshale)  yako kwenye Highlight (Read out loud) Itakayofungua drop down menyu ndogo.





Hatua ya 6

Kwenye drop down menyu ndogo bofya (Activate read out loud) Kuwezesha program kuanza kusoma faili lako.




Hatua ya 7

Bofya mara mbili mwisho wa  herufi,neno,sentence,paragrafu,au hata ukurasa na neno hilo au ukurasa huo utazungushiwa kingo kisha moja kwa moja utaanza kusikiliza 
kilichoandikwa.



Mfano mwingine



Hatua ya 8

Kama hutapenda kuendelea na kusikiliza rudi tena kwenye menyu kisha utakapo elekeza pointer (kamshale) yako kwenye Read out loud utaona maelekezo kwenye Drop down menyu ndogo kama ifuatavyo.kisha chagua unachotaka ikiwa ni,

kusitisha Deactivate Read out Loud ,
kusoma ukurasa Read this page only,
kusoma document nzima  Read To End of Document,
Kustop au Kusimama kwa muda, Pause and Stop



Hatua ya 9

Unaweza kutumia kicharazio chako (keyboard) Kwa kufuata maelekezo yaliyo katika picha baada ya Ku activate program.


Nakutakia usomaji mwema.kama unamaoni au swali usisite kuandika katika mwisho wa mada hii karibu.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni