Jumanne, 8 Aprili 2014

MAMBO MATATU YA KUEPUKA


Najua wewe ni rafiki yangu,kaka yangu ,ndugu yangu,nk.Kutokana na hilo sina budi kukushirikisha katika mambo ambayo kidogo nimeyaona kuwa yanahitaji taadhari ya hali ya juu kidogo.

1. EPUKA FASHON MPYA IJULIKANAYO KAMA ADULT BABY (INFANTILISM)
Japo ukiwauliza wanasaikologia kuhusu Infantilism watakupa majibu tofauti sana na hiki ninachokwenda kukizungumza.Lakini cha ajabu sana tatizo hili limegeuzwa fashion.

Fashion hii ya mtindo wa maisha imeanza kupata umaarufu katika miaka ya hivi karibuni.kama tafsiri ya neno hilo la kiingereza lilivyo infantilism linalotokana na neno INFANT lenye maana ya mtoto aliye katika umri mdogo kati ya miaka 5-7, Ni kwamba mtu huyo anajizoeza kuishi kwa kutumia tabia za watoto wa umri huo.Kitendo cha kuishi kwa kutumia tabia za watoto wa umri huu mdogo ndicho kinachoitwa INFANTILISM.

Katika maisha haya mtu hutumia staili zote za maisha za mtoto mdogo. wengine wamekwenda mbali zaidi hata kuvaa pampers za watoto kama unavyoweza kuona katika picha hizo hapo chini.



Kama unataka kuona picha zaidi unaweza kutembelea link hii http://www.oddee.com/item_98448.aspx&sa=U&ei=tvBQUYCgFqTA0gH9poGwCg&ved=0CC0QFjAF&usg=AFQjCNFmXyNGg5MHWQggOc9PipmuEtVDxA.Hata hivyo baadhi ya mitandao imehamasisha maisha hayo kwa kutoa hata mbinu kama ilivyo katika mtandao wa KNOW HOW ( http://www.wikihow.com/Act-Like-a-Baby-Again)

Sababu za kufanya hivyo ni nyingi kutegemea mtu na mtu.Lakini wengi wao wamekuwa wakidai kuwa kufanya hivyo imewapunguzia bugdha za kimaisha kwa kuwa maisha yamekuwa Very complicated (yanasumbua) vitu vinapanda bei ,tecknologia inaongezeka,uzazi unasumbua,nk ambapo binadamu anahitaji kufanya kila linalowezekana ili kwenda sawa na dunia.

Wengine wamedai kuwa wanaofanya hivyo ni kutokana na namna walivyo,yaani ni watu ambao wana hurka ya kupendelea zaidi maisha ya kitoto na hufurahia zaidi kuishi maisha hayo kuliko maisha ya kiutu uzima .

FAIDA. Kuenjoi maisha bila msongo wa mawazo hasa kwa zama hizi za maisha ni pesa.

HASARA.
A. KUENDELEA KURUDI NYUMA KIFIKRA.
Najua miongoni mwetu wapo wanaopenda kuiga mambo bila kutafakari kwa kina.Binadamu lazima awajibike kujibu maswali yote magumu asipofanya hivyo hakuna mtu mwingine wa kufanya hivyo.

Tusikubali kukaa na wanyonyaji hawa katika dunia hii.Hawataki kufikiri,hawataki kushiriki kujibu maswali magumu,Hawataki kuzaa,Hawataki kushirikiana na watu waliopevuka na Hawana mchango mkubwa kiuzalishaji.

Kama kila mtu akitaka kuwa Adult baby nani ataendeleza dunia wakati wote tutakuwa tumeshikilia chupa za kunyonyea maziwa mdomoni na kuchezea midoli. Napendekeza watu hawa tuwaambukize fikra zilizopevuka wawe na mchango duniani.

B. UCHUMI WA DUNIA KUANGUKA
Tukumbuke kuwa dunia inamzigo mkubwa sana wa kubeba, kama tusipokuwa makini utatuangukia na kutudidimiza milele kwa kuwa hakuna kiumbe kingine chenye uwezo zaidi ya binadamu isipokuwa Mungu.Na Mungu kwasababu hakututuma kufanya ujinga huu hatowajibika kwa lolote.

Mzigo ninaouzungumzia hapa ni wa wagonjwa,walemavu wa aina zote madawa ya kulevya,akili,viungo,nk.Mzigo mwingine ni watoto,wazee,watu wasio na elimu,masikini nk.

Katika mtandao unaofahamika kama WORD DISABLED (http://www.disabled-world.com/disability/statistics/) umewahi kutoa tasmini ya walemavu kufikia kiasi cha milioni 650 katika nchi zinazoendelea duniani.Hiyo ni sawa na asilimia 10 ya watu wote duniani ambayo ni bilioni 7.

Kwa mujibu wa mtandao huohuo katika kila watu 5, 1 ni mlemavu kwa marekani peke yake. Na kwa mujibu wa social security administration ya inchini humo kuwa 33% ya wamarekani watakuwa na ulemavu wanapofikisha umri wa miaka ishirini kazini (http://www.disabled-world.com/)

MZIGO MWINGINE NI WAZEE .Huu ni mzigo wa kudumu ambao kwa mujibu wa taarifa za tar 8/april 2014 za mtandao wa 

http://www.telegraph.co.uk/earth/greenpolitics/population/5872109/Worlds-elderly-to-overtake-number-of-infants.html 

wazee wa umri wa miaka isiyopungua 65 wanakadiriwa kufikia Bilioni 1.3 miaka arobaini ijayo.Na wazee wa umri wa miaka zaidi ya 85 idadi yao ndiyo inayoongezeka haraka kuliko idadi ya watu wengine wowote.

Ukumbuke kuwa hawa wazee huhitaji Pension,matibabu na huduma nyinginezo.

WATOTO
Hawa nao ni mzigo kwa mujibu wa takwimu za benk ya dunia mwaka 2012 watoto chini ya umri wa miaka 15 ni asilimia 26 ya watu wote duniani sawa na bilioni 1 .82 ya watu wote .

Na kwa taarifa tu ni kwamba uzazi unaongezeka kwa kasi sana hasa kwa nchi za afrika ;inakadiriwa ifikapo mwaka 2050 idadi ya waafrika itakuwa mara mbili ya ilivyo hivi sasa ambapo inakadiriwa kufikia bilioni 2.4 . 

Tazama WORLD DATA SHEET  http://www.prb.org/Publications/Datasheets/2013/2013-world-population-data-sheet/data-sheet.aspx

Watu wenye umri wa kufanya kazi kati ya vijana na wazee duniani kwa mujibu wa WORLD BANK ni 52% sawa na watu billion 3.64 ambao katika nchi kama United Arab Emiretes yenye watu zaidi ya milioni 92 wanao fanya kazi ni 17% sawa na milioni 15.64.

Jiulize swali bado tunahitaji kuongeza mizigo mingine ya kujitakia? HATUHITAJI WATU WANAOITWA ADULT BABIES.

2. EPUKA KITU KINACHOITWA SECOND LIFE
Hii ni dizaini mpya ya maisha inayopata umaarufu sana duniani .Na imetumika kama sehemu ya kufanyia RECREATION (MAPUMZIKO YA AKILI) .Maisha haya ni ya kielektronik yanayoendeshwa kwa kutumia program za kompyuta.

Program hizi huwekwa kwenye internet ili mtu aweze kuzitumia atakavyo.Mtu anaweza kuanzisha familia yake mpya itakayokuwa na maisha ayatakayo ikiwa ni ya kijijini au mjini ,vilevile anaweza kuifanya ikawa ni familia nusu mnyama na nusu binadamu.

Katika maisha haya unaweza kuchagua kuwa singo au mtu uliye na mpenzi au mke.Pia zimeanzishwa programu za wanafunzi ambazo si maarufu sana.

Katika program hizo unaweza kubuni makazi na kila kitu unachokitaka kwaajili ya maisha yako au pengine na familiya yako .Kwa kutumia internet unaweza kuishi humo na kufanya kilakitu ambacho ungefanya katika maisha yako halisi kwa kutumia picha za kiwango cha hali ya juu na sauti zilizomo katika program hizo .

MADHARA.
A. Programu hizi zimekaa kimapenzi zaidi hivyo zitakufanya kufikiria ngono kila wakati.
B. Zinaweza kuvunja ndoa yako kwa kuhamisha fikra zako kwenda second life.
C. Zitakuchukulia muda wako wa maendeleo
D. Zitakuondolea uwajibikaji kwa kupenda kuishi maisha ya pichapicha tu.

3. EPUKA KUBEBA MIDOLI (TOYS )
Huu ndiyo mtindo wa zamani zaidi wa kimaisha kuliko hii mingine.Wapo watu wanaodai kuwa huu ni utamaduni wa magharibi.Lakini baadhi ya wanaobeba midoli hii hasa ile ya watoto bandia wanapohojiwa hutoa sababu zifuatazo.

A. Huwasaidi kuwafariji wanapopoteza watoto wao wanaowapenda
B. Huwafariji hasa wanapokuwa hawakufanikiwa kupata watoto
C. Huwasaidia kupunguza hamu ya kuwa na mtoto

Naamini kila utakayemuuliza atakupa sababu yake na baadaye utagundua kuwa hakuna cha umagharibi wala cha umashariki ni swala la kujiendekeza na ubinafsi tu ndiyo unaotawala.

Midoli hii kwa wengine hasa wale wazoefu inawagharimu fedha nyingi kwa kuibadilisha badilisha ili kukata kiu yao. Mfano hii ni midoli inayouzwa kiasi ya pound 200.



Wengi wao hulazimika kununua toy carriers ambazo huuzwa kwenye supamarket mbalimbali dunia nzima.Hulazimika kuingia gharama yeyote ili mradi tu kiu yao ya kulea au kutunza mtoto huyo au mdoli huyo iishe.

Ninachotaka kusema ni kuwa, kwanza shwala hili linatokana na ubinafsi na kutojua thamani tuliyonayo binadamu.Na kama ni utamaduni wa kimagharibi basi unatokana na mazoea mabaya ambayo kizazi hadi kizazi kimerithishwa ambapo nalazimika kusema ni moja ya MILA POTOFU.

Binadamu anamajukumu makubwa sana na thamani yake ni kubwa sana wala hafanani kabisa na kubeba mdoli yaani toys.Mwenyezi mungu ameweka uwezo mkubwa sana ndani yetu na ametupa majukumu makubwa sana.Majukumu hayo ni pamoja na kuzaa,na kuhudumia viumbe hai vyote vilivyopo duniani.

Acha kutoa muda wako kuhudumia midoli na vitu visivyo na faida tuwaachie watoto ambao hawana majukumu yeyote wafanye kazi hiyo. Ebu ona huyu

http://www.mirror.co.uk/news/real-life-stories/the-fake-babies-craze-meet-the-women-786454

Kama unashida ya mtoto wako wengi ambao hawana mama na wanaweza kukuchangamsha wakiwa na full sensitivity.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni